Nibariki

By Guardian Angel

Lyrics

Kuna wakati ambao nilijiona duni sana 

Kuna wakati ambao nilijidharau sana 

Kuna wakati ambao nilijiona chini sana 

Kumbe machoni pa Mungu tofauti sana 

Kumbe machoni pa Mungu tofauti sana 


Kuna wakati ambao walio na shida kama wewe watakucheka 

Kuna wakati ambao uliodhani ni marafiki watakutoka 

Kuna wakati ambao utadhani Mungu amekuacha 

Kumbe ya Mungu ni mengi, mengi sana 

Kumbe ya Mungu ni mengi, mengi sana 


Nipe kibali nibariki, nibariki niwashuhudie 

Nipe fedha nimiliki, nimiliki nikutumikie 

Mungu wangu nibariki, nibariki niwashuhudie 

Nipe fedha nimiliki, nimiliki nikutumikie 


Rap: 

Wakikucheki kibandani na kumbe yeye amekuchora kiganjani 

Maisha yako yako duni namna gani na kumbe yeye amekuseti ubaoni 

Kuja enda nami mpaka mwisho kile ? kamili 

Maisha yangu kamili, mentaly emotionaly physically 

Better financially ... 


Nipe kibali nibariki, nibariki niwashuhudie 

Nipe fedha nimiliki, nimiliki nikutumikie 

Mungu wangu nibariki, nibariki niwashuhudie 

Nipe fedha nimiliki, nimiliki nikutumikie