Lyrics Page

Ebenezer Nani Kama Wewe

By Paul Mwai

6,928 views Jun 6, 2026 updated

Moyoni mwangu Yahweh nashukuru sana
Kwa wema wako na fadhili zako kwangu za milele
Matendo yako maishani mwangu ya tisha Jehovah
Natamani nifanane nawe Messiah Siku zote
Usiye badilika na wakati Elohim u mwema

Ebenezer nani kama wewe nainama mbele zako Wewe ni Mungu
Ebenezer nani kama wewe nainama mbele zako Wewe ni Mungu

Natamani nifanane nawe usiyebadilika
Uaminifu wako Adonai wa milele na milele,
Toka utotoni mwangu umekuwa mwema sana
Umbali umenileta Yahweh hakuna mwingine kama wewe

Ebenezer nani kama wewe nainama mbele zako Wewe ni Mungu
Ebenezer nani kama wewe nainama mbele zako Wewe ni Mungu

Kwa nehema yako Adonai, umeihifadhi roho yangu
Wengi tulizaliwa nao na wengi sasa wamefariki
Wengine hawakujui Yahweh Mungu mwenye enzi na uzima,
Lakini kwa nehema yako Shamaah umenipa uhai niishi

Ebenezer nani kama wewe nainama mbele zako Wewe ni Mungu
Ebenezer nani kama wewe nainama mbele zako Wewe ni Mungu

Wewe uliye nena na Samweli, hutamdharau mwanadamu,
usiye tazama maumbile, yake wewe Mungu wa haki,
Umbali umenileta Yahweh, Ebeneezer wewe ndiye Mungu,
Mungu mwenye enzi na uzima, uinuliwe milele yote.

Ebenezer nani kama wewe nainama mbele zako Wewe ni Mungu
Ebenezer nani kama wewe nainama mbele zako Wewe ni Mungu

Umekuwa mwema Imanueli, mwaminifu
Wewe ndiwe pumzi ya imani yangu nakuabudu
Umekuwa mwema Imanueli, mwaminifu
Wewe ndiwe pumzi ya imani yangu nakuabudu

Ebenezer means The Stone of Help

Official Video

Save Your Favorites

Create a free account to save songs, build your personal library, and connect with the Zion community.

Create Free Account

Join the Zion Community

Create a free account to save your favorite lyrics, submit song suggestions, and connect with fellow worshippers.

No spam. Unsubscribe anytime.