Tangu siku hiyo aliponijia,
Akae moyoni mwangu.
Sina giza tena, ila mwanga pia,
Kwa Yesu, Mwokozi wangu.
Amani moyoni mwangu,
Kwa Yesu, Mwokozi wangu.
Sina shaka kamwe
Kwa sababu yeye Yu nami moyoni mwangu.
Sina haja tena ya kutanga-tanga,
Ndiye Kiongozi changu.
Dhambi zangu zote zimeondolewa,
Na Yesu Mwanawe Mungu.
Amani moyoni mwangu,
Kwa Yesu, Mwokozi wangu.
Sina shaka kamwe
Kwa sababu yeye
Yu nami moyoni mwangu.
Matumaini yangu ni ya hakika,
Katika Mwokozi wangu.
Hofu zangu na hamu zimeondoka,
Kwa kuwa ninaye Yesu.
Amani moyoni mwangu,
Kwa Yesu, Mwokozi wangu.
Sina shaka kamwe
Kwa sababu yeye...
Yu nami moyoni mwangu.
Siogopi tena nikiitwa kufa,
Yu nami daima Yesu.
Mlango wa mbingu ni Yesu Mwokozi,
?Tapita humo kwa damu.
Amani moyoni mwangu,
Kwa Yesu, Mwokozi wangu.
Sina shaka kamwe
Kwa sababu yeye...
Yu nami moyoni mwangu.
Nitaketi na Yesu huko milele,
Nimsifu Mwokozi wangu.
Nina raha moyoni majira yote,
Kwa Yesu Mwanawe Mungu.
Amani moyoni mwangu,
Kwa Yesu, Mwokozi wangu.
Sina shaka kamwe
Kwa sababu yeye...
Yu nami moyoni mwangu.
24 Amani Moyoni Mwangu Tangu Siku hiyo Aliponijia
Benson Kitiechi's song is a Swahili gospel piece about the peace and assurance found in Jesus Christ. The lyrics express gratitude for salvation, the removal of sin, and the certainty of eternal life. The singer declares that since Jesus came into their heart, there is no darkness, only light, and no fear of death because Jesus is always with them. The song emphasizes unwavering faith, hope, and the joy of being led by Christ. It reflects a personal testimony of transformation and the comfort of knowing that Jesus is the guide and Savior, promising a future in heaven.