Matendo ya Mitume Mlango 14 Acts
Matendo ya Mitume 14:1 Acts 14:1
Ikawa huko Ikonio wakaingia pamoja katika sinagogi la Wayahudi; na kwa vile walivyonena, kundi kubwa la Wayahudi na la Wayunani wakaamini.
Matendo ya Mitume 14:2 Acts 14:2
Walakini Wayahudi wasioamini wakawataharakisha watu wa Mataifa na kuwatia nia mbaya juu ya ndugu.
Matendo ya Mitume 14:3 Acts 14:3
Basi wakakaa huko wakati mwingi, wakinena kwa ushujaa katika Bwana, aliyelishuhudia neno la neema yake, akiwajalia ishara na maajabu yatendeke kwa mikono yao.
Matendo ya Mitume 14:4 Acts 14:4
Lakini jamii ya watu wa mjini wakafarakana; hawa walikuwa upande wa Wayahudi, na hawa upande wa Mitume.
Matendo ya Mitume 14:5 Acts 14:5
Hata palipotokea shambulio la watu wa Mataifa na Wayahudi pamoja na wakubwa wao juu yao, kuwatenda jeuri na kuwapiga kwa mawe,
Matendo ya Mitume 14:6 Acts 14:6
wao wakapata habari wakakimbilia Listra na Derbe, miji ya Likaonia, na nchi zilizo kando kando;
Matendo ya Mitume 14:7 Acts 14:7
wakakaa huko, wakiihubiri Injili.
Matendo ya Mitume 14:8 Acts 14:8
Na huko Listra palikuwa na mtu mmoja, dhaifu wa miguu, kiwete tangu tumboni mwa mamaye, ambaye hajaenda kabisa.
Matendo ya Mitume 14:9 Acts 14:9
Mtu huyo alimsikia Paulo alipokuwa akinena; ambaye akamkazia macho na kuona ya kuwa ana imani ya kuponywa,
Matendo ya Mitume 14:10 Acts 14:10
akasema kwa sauti kuu, Simama kwa miguu yako sawasawa. Akasimama upesi akaenda.
Matendo ya Mitume 14:11 Acts 14:11
Na makutano walipoona aliyoyafanya Paulo wakapaza sauti zao, wakisema kwa Kilikaonia, Miungu wametushukia kwa mifano ya wanadamu.
Matendo ya Mitume 14:12 Acts 14:12
Wakamwita Barnaba, Zeu, na Paulo, Herme, kwa sababu ndiye aliyekuwa mnenaji.
Matendo ya Mitume 14:13 Acts 14:13
Kuhani wa Zeu ambaye hekalu lake lilikuwa mbele ya mji, akaleta ng'ombe na taji za maua hata malangoni, akitaka kutoa dhabihu pamoja na makutano.
Matendo ya Mitume 14:14 Acts 14:14
Walakini mitume Barnaba na Paulo, walipopata habari, wakararua nguo zao, wakaenda mbio wakaingia katika makutano, wakipiga kelele,
Matendo ya Mitume 14:15 Acts 14:15
wakisema, Akina bwana, mbona mnafanya haya? Sisi nasi tu wanadamu hali moja na ninyi; twawahubiri habari njema, ili mgeuke na kuyaacha mambo haya ya ubatili na kumwelekea Mungu aliye hai, aliyeumba mbingu na nchi na bahari na vitu vyote vilivyomo;
Matendo ya Mitume 14:16 Acts 14:16
ambaye zamani zilizopita aliwaacha mataifa yote waende katika njia zao wenyewe.
Matendo ya Mitume 14:17 Acts 14:17
Lakini hakujiacha pasipo ushuhuda, kwa kuwa alitenda mema, akiwapeni mvua kutoka mbinguni, na nyakati za mavuno, akiwashibisha mioyo yenu chakula na furaha.
Matendo ya Mitume 14:18 Acts 14:18
Na kwa maneno hayo wakawazuia makutano kwa shida, wasiwatolee dhabihu.
Matendo ya Mitume 14:19 Acts 14:19
Lakini Wayahudi wakafika toka Antiokia na Ikonio, wakawashawishi makutano hata wakampiga kwa mawe Paulo, wakamburuta nje ya mji, wakidhania ya kuwa amekwisha kufa.
Matendo ya Mitume 14:20 Acts 14:20
Lakini wanafunzi walipokuwa wakimzunguka pande zote, akasimama, akaingia ndani ya mji; na siku ya pili yake akatoka, akaenda zake pamoja na Barnaba mpaka Derbe.
Matendo ya Mitume 14:21 Acts 14:21
Hata walipokwisha kuihubiri Injili katika mji ule, na kupata wanafunzi wengi, wakarejea mpaka Listra na Ikonio na Antiokia,
Matendo ya Mitume 14:22 Acts 14:22
wakifanya imara roho za wanafunzi na kuwaonya wakae katika ile Imani, na ya kwamba imetupasa kuingia katika ufalme wa Mungu kwa njia ya dhiki nyingi.
Matendo ya Mitume 14:23 Acts 14:23
Na walipokwisha kuwachagulia wazee katika kila kanisa, na kuomba pamoja na kufunga, wakawaweka katika mikono ya Bwana waliyemwamini.
Matendo ya Mitume 14:24 Acts 14:24
Wakapita kati ya Pisidia wakaingia Pamfilia.
Matendo ya Mitume 14:25 Acts 14:25
Na baada ya kuhubiri lile neno katika Perge wakatelemka mpaka Atalia.
Matendo ya Mitume 14:26 Acts 14:26
Na kutoka huko wakaabiri kwenda Antiokia. Huko ndiko walikoombewa neema ya Mungu kwa ile kazi waliyokwisha kuitimiza.
Matendo ya Mitume 14:27 Acts 14:27
Hata walipofika wakalikutanisha kanisa, wakawaeleza mambo yote aliyoyafanya Mungu pamoja nao, na ya kwamba amewafungulia Mataifa mlango wa imani.
Matendo ya Mitume 14:28 Acts 14:28
Wakaketi huko wakati usiokuwa mchache, pamoja na wanafunzi.