Matendo ya Mitume Mlango 18 Acts
Matendo ya Mitume 18:1 Acts 18:1
Baada ya mambo hayo, Paulo akatoka Athene akafika Korintho.
Matendo ya Mitume 18:2 Acts 18:2
Akamwona Myahudi mmoja, jina lake Akila, mzalia wa Ponto; naye amekuja kutoka nchi ya Italia siku za karibu, pamoja na Prisila mkewe, kwa sababu Klaudio amewaamuru Wayahudi wote watoke Rumi, naye akafikilia kwao;
Matendo ya Mitume 18:3 Acts 18:3
na kwa kuwa kazi yao ya ufundi ilikuwa moja, akakaa kwao, wakafanya kazi pamoja, kwa maana walikuwa mafundi wa kushona hema.
Matendo ya Mitume 18:4 Acts 18:4
Akatoa hoja zake katika sinagogi kila sabato, akajaribu kuwavuta Wayahudi na Wayunani.
Matendo ya Mitume 18:5 Acts 18:5
Hata Sila na Timotheo walipotelemka kutoka Makedonia, Paulo akasongwa sana na lile neno, akiwashuhudia Wayahudi ya kwamba Yesu ni Kristo.
Matendo ya Mitume 18:6 Acts 18:6
Walipopingamana naye na kumtukana Mungu, akakung'uta mavazi yake, akawaambia, Damu yenu na iwe juu ya vichwa vyenu; mimi ni safi; tangu sasa nitakwenda kwa watu wa Mataifa.
Matendo ya Mitume 18:7 Acts 18:7
Akaondoka huko akaingia katika nyumba ya mtu mmoja jina lake Tito Yusto, mcha Mungu, ambaye nyumba yake ilikuwa mpaka mmoja na sinagogi.
Matendo ya Mitume 18:8 Acts 18:8
Na Krispo, mkuu wa sinagogi, akamwamini Bwana pamoja na nyumba yake yote. Wakorintho wengi waliposikia, waliamini, wakabatizwa.
Matendo ya Mitume 18:9 Acts 18:9
Bwana akamwambia Paulo kwa maono usiku, Usiogope, bali nena, wala usinyamaze,
Matendo ya Mitume 18:10 Acts 18:10
kwa kuwa mimi ni pamoja nawe, wala hapana mtu atakayekushambulia ili kukudhuru; kwa maana mimi nina watu wengi katika mji huu.
Matendo ya Mitume 18:11 Acts 18:11
Akakaa huko muda wa mwaka mmoja na miezi sita akifundisha kati yao neno la Mungu.
Matendo ya Mitume 18:12 Acts 18:12
Hata Galio alipokuwa liwali wa Akaya, Wayahudi wakamwinukia Paulo kwa nia moja, wakamleta mbele ya kiti cha hukumu,
Matendo ya Mitume 18:13 Acts 18:13
wakisema Mtu huyu huwavuta watu ili wamwabudu Mungu kinyume cha sheria.
Matendo ya Mitume 18:14 Acts 18:14
Na Paulo alipotaka kufunua kinywa chake, Galio akawaambia Wayahudi, Kama lingekuwa jambo la dhuluma au la hila mbaya, enyi Wayahudi, ingekuwa haki mimi kuchukuliana nanyi;
Matendo ya Mitume 18:15 Acts 18:15
bali ikiwa ni hoja juu ya maneno na majina na sheria yenu, liangalieni ninyi wenyewe, maana mimi sitaki kuwa mwamuzi wa mambo hayo.
Matendo ya Mitume 18:16 Acts 18:16
Akawafukuza waondoke mbele ya kiti cha hukumu.
Matendo ya Mitume 18:17 Acts 18:17
Nao wote wakamshika Sosthene, mkuu wa sinagogi, wakampiga mbele ya kiti cha hukumu. Wala Galio hakuyaona mambo hayo kuwa ni kitu.
Matendo ya Mitume 18:18 Acts 18:18
Baada ya hayo Paulo akazidi kukaa huko siku nyingi, kisha akaagana na ndugu akaabiri kwenda Shamu; na Prisila na Akila wakaenda pamoja naye, alipokwisha kunyoa kichwa chake huko Kenkrea; maana alikuwa ana nadhiri.
Matendo ya Mitume 18:19 Acts 18:19
Wakafika Efeso, akawaacha huko. Yeye mwenyewe akaingia katika sinagogi, akahojiana na Wayahudi.
Matendo ya Mitume 18:20 Acts 18:20
Walipomtaka akae wakati mwingi zaidi, hakukubali;
Matendo ya Mitume 18:21 Acts 18:21
bali aliagana nao, akisema, Nitarejea kwenu tena, Mungu akinijalia. Akatweka, akatoka Efeso,
Matendo ya Mitume 18:22 Acts 18:22
na alipokwisha kushuka Kaisaria, akapanda juu, akawasalimu kanisa, kisha akatelemkia Antiokia.
Matendo ya Mitume 18:23 Acts 18:23
Hata akiisha kukaa huko siku kadha wa kadha akaondoka, akapita kati ya nchi ya Galatia na Frigia, mji kwa mji, akiwathibitisha wanafunzi.
Matendo ya Mitume 18:24 Acts 18:24
Basi Myahudi mmoja, jina lake Apolo, mzalia wa Iskanderia, mtu wa elimu, akafika Efeso; naye alikuwa hodari katika maandiko.
Matendo ya Mitume 18:25 Acts 18:25
Mtu huyo alikuwa amefundishwa njia ya Bwana; na kwa kuwa roho yake ilikuwa ikimwaka, alianza kunena na kufundisha kwa usahihi habari za Yesu; naye alijua ubatizo wa Yohana tu.
Matendo ya Mitume 18:26 Acts 18:26
Akaanza kunena kwa ujasiri katika sinagogi; hata Prisila na Akila walipomsikia wakamchukua kwao, wakamweleza njia ya Bwana kwa usahihi zaidi.
Matendo ya Mitume 18:27 Acts 18:27
Na alipotaka kuvuka bahari aende mpaka Akaya, ndugu wakamhimiza, wakawaandikia wale wanafunzi wamkaribishe, naye alipofika akawasaidia sana wale waliokwisha kuamini kwa neema ya Mungu.
Matendo ya Mitume 18:28 Acts 18:28
Kwa maana aliwashinda Wayahudi kabisa kabisa mbele ya watu wote, akionyesha kwa maneno ya maandiko ya kuwa Yesu ni Kristo.