Matendo ya Mitume Mlango 2 Acts

Matendo ya Mitume 2:1 Acts 2:1

Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja.

Matendo ya Mitume 2:2 Acts 2:2

Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi.

Matendo ya Mitume 2:3 Acts 2:3

Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao.

Matendo ya Mitume 2:4 Acts 2:4

Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka.

Matendo ya Mitume 2:5 Acts 2:5

Na walikuwako Yerusalemu Wayahudi wakikaa, watu watauwa, watu wa kila taifa chini ya mbingu.

Matendo ya Mitume 2:6 Acts 2:6

Basi sauti hii iliposikiwa makutano walikutanika, wakashikwa na fadhaa, kwa kuwa kila mmoja aliwasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe.

Matendo ya Mitume 2:7 Acts 2:7

Wakashangaa wote, wakastaajabu wakiambiana, Tazama, hawa wote wasemao si Wagalilaya?

Matendo ya Mitume 2:8 Acts 2:8

Imekuwaje basi sisi kusikia kila mtu lugha yetu tuliyozaliwa nayo?

Matendo ya Mitume 2:9 Acts 2:9

Warparthi na Wamedi na Waelami, nao wakaao Mesopotamia, Uyahudi na Kapadokia, Ponto na Asia,

Matendo ya Mitume 2:10 Acts 2:10

Frigia na Pamfilia, Misri na pande za Libia karibu na Kirene, na wageni watokao Rumi, Wayahudi na waongofu,

Matendo ya Mitume 2:11 Acts 2:11

Wakrete na Waarabu; tunawasikia hawa wakisema kwa lugha zetu matendo makuu ya Mungu.

Matendo ya Mitume 2:12 Acts 2:12

Wakashangaa wote wakaingiwa na shaka, wakiambiana, Maana yake nini mambo haya?

Matendo ya Mitume 2:13 Acts 2:13

Wengine walidhihaki, wakisema, wamelewa kwa mvinyo mpya.

Matendo ya Mitume 2:14 Acts 2:14

Lakini Petro akasimama pamoja na wale kumi na mmoja, akapaza sauti yake, akawaambia, Enyi watu wa Uyahudi, na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, lijueni jambo hili, mkasikilize maneno yangu.

Matendo ya Mitume 2:15 Acts 2:15

Sivyo mnavyodhani; watu hawa hawakulewa, kwa maana ni saa tatu ya mchana;

Matendo ya Mitume 2:16 Acts 2:16

lakini jambo hili ni lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii Yoeli,

Matendo ya Mitume 2:17 Acts 2:17

Itakuwa siku za mwisho, asema Mungu, nitawamwagia watu wote Roho yangu, na wana wenu na binti zenu watatabiri; na vijana wenu wataona maono; na wazee wenu wataota ndoto.

Matendo ya Mitume 2:18 Acts 2:18

Naam, na siku zile nitawamwagia watumishi wangu wanaume na wanawake Roho yangu, nao watatabiri.

Matendo ya Mitume 2:19 Acts 2:19

Nami nitatoa ajabu katika mbingu juu, na ishara katika nchi chini, damu na moto, na mvuke wa moshi.

Matendo ya Mitume 2:20 Acts 2:20

Jua litageuka kuwa giza, na mwezi kuwa damu, kabla ya kuja ile siku ya Bwana iliyo kuu na iliyo dhahiri.

Matendo ya Mitume 2:21 Acts 2:21

Na itakuwa kila atakayeliitia jina la Bwana ataokolewa.

Matendo ya Mitume 2:22 Acts 2:22

Enyi waume wa Israeli, sikilizeni maneno haya: Yesu wa Nazareti, mtu aliyedhihirishwa kwenu na Mungu kwa miujiza na ajabu na ishara, ambazo Mungu alizifanya kwa mkono wake kati yenu, kama ninyi wenyewe mnavyojua;

Matendo ya Mitume 2:23 Acts 2:23

mtu huyu alipotolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa, na kwa kujua kwake tangu zamani, ninyi mkamsulibisha kwa mikono ya watu wabaya, mkamwua;

Matendo ya Mitume 2:24 Acts 2:24

ambaye Mungu alimfufua, akiufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao.

Matendo ya Mitume 2:25 Acts 2:25

Maana Daudi ataja habari zake, Nalimwona Bwana mbele yangu siku zote, Kwa kuwa yuko upande wa mkono wangu wa kuume, nisitikisike.

Matendo ya Mitume 2:26 Acts 2:26

Kwa hiyo moyo wangu ukapendezewa, ulimi wangu ukafurahi; Tena mwili wangu nao utakaa katika matumaini.

Matendo ya Mitume 2:27 Acts 2:27

Kwa maana hutaiacha roho yangu katika kuzimu; Wala hutamtoa Mtakatifu wako aone uharibifu.

Matendo ya Mitume 2:28 Acts 2:28

Umenijuvisha njia za uzima; Utanijaza furaha kwa uso wako.

Matendo ya Mitume 2:29 Acts 2:29

Waume, ndugu zangu, mniwie radhi, niseme kwa ujasiri mbele yenu habari za baba yetu mkuu, Daudi, ya kuwa alifariki akazikwa, na kaburi lake liko kwetu hata leo.

Matendo ya Mitume 2:30 Acts 2:30

Basi kwa kuwa ni nabii, akijua ya kuwa Mungu amemwapia kwa kiapo, ya kwamba katika uzao wa viuno vyake atamketisha mmoja katika kiti chake cha enzi;

Matendo ya Mitume 2:31 Acts 2:31

yeye mwenyewe akitangulia kuyaona haya, alitaja habari za kufufuka kwake Kristo, ya kwamba roho yake haikuachwa kuzimu, wala mwili wake haukuona uharibifu.

Matendo ya Mitume 2:32 Acts 2:32

Yesu huyo Mungu alimfufua, na sisi sote tu mashahidi wake.

Matendo ya Mitume 2:33 Acts 2:33

Basi yeye, akiisha kupandishwa hata mkono wa kuume wa Mungu, na kupokea kwa Baba ile ahadi ya Roho Mtakatifu, amekimwaga kitu hiki mnachokiona sasa na kukisikia.

Matendo ya Mitume 2:34 Acts 2:34

Maana Daudi hakupanda mbinguni; bali yeye mwenyewe anasema, Bwana alimwambia Bwana wangu, Keti upande wa mkono wangu wa kuume.

Matendo ya Mitume 2:35 Acts 2:35

Hata nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.

Matendo ya Mitume 2:36 Acts 2:36

Basi nyumba yote ya Israeli na wajue yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo mliyemsulibisha kuwa Bwana na Kristo.

Matendo ya Mitume 2:37 Acts 2:37

Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

Matendo ya Mitume 2:38 Acts 2:38

Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

Matendo ya Mitume 2:39 Acts 2:39

Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie.

Matendo ya Mitume 2:40 Acts 2:40

Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi.

Matendo ya Mitume 2:41 Acts 2:41

Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu.

Matendo ya Mitume 2:42 Acts 2:42

Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali.

Matendo ya Mitume 2:43 Acts 2:43

Kila mtu akaingiwa na hofu; ajabu nyingi na ishara zikafanywa na mitume.

Matendo ya Mitume 2:44 Acts 2:44

Na wote walioamini walikuwa mahali pamoja, na kuwa na vitu vyote shirika,

Matendo ya Mitume 2:45 Acts 2:45

wakiuza mali zao, na vitu vyao walivyokuwa navyo, na kuwagawia watu wote kama kila mtu alivyokuwa na haja.

Matendo ya Mitume 2:46 Acts 2:46

Na siku zote kwa moyo mmoja walidumu ndani ya hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, na kushiriki chakula chao kwa furaha na kwa moyo mweupe,

Matendo ya Mitume 2:47 Acts 2:47

wakimsifu Mungu, na kuwapendeza watu wote. Bwana akalizidisha kanisa kila siku kwa wale waliokuwa wakiokolewa.