Mambo ya Walawi Mlango 24 Leviticus
Mambo ya Walawi 24:1 Leviticus 24:1
Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
Mambo ya Walawi 24:2 Leviticus 24:2
Waagize wana wa Israeli kwamba wakuletee mafuta ya zeituni safi ya kupondwa kwa ajili ya ile nuru, ili hiyo taa iwake daima.
Mambo ya Walawi 24:3 Leviticus 24:3
Hapo nje ya pazia la ushahidi, ndani ya hema ya kukutania, Haruni ataitengeza tangu jioni hata asubuhi mbele za Bwana daima; ni amri ya milele katika vizazi vyenu.
Mambo ya Walawi 24:4 Leviticus 24:4
Atazitengeza hizo taa katika kile kinara kilicho safi mbele za Bwana daima.
Mambo ya Walawi 24:5 Leviticus 24:5
Nawe utatwaa unga mwembamba, na kuoka mikate kumi na miwili ya huo unga; sehemu za kumi mbili za efa, zitakuwa katika mkate mmoja.
Mambo ya Walawi 24:6 Leviticus 24:6
Nawe iweke mistari miwili, mikate sita kwa kila mstari, juu ya hiyo meza safi, mbele za Bwana.
Mambo ya Walawi 24:7 Leviticus 24:7
Nawe utatia ubani safi juu ya kila mstari, ili uwe ukumbusho kwa hiyo mikate, sadaka ya kusongezwa kwa Bwana kwa moto.
Mambo ya Walawi 24:8 Leviticus 24:8
Kila siku ya Sabato ataipanga mbele za Bwana daima; ni kwa ajili ya wana wa Israeli, agano la milele.
Mambo ya Walawi 24:9 Leviticus 24:9
Nayo itakuwa ya Haruni na wanawe; nao wataila katika mahali patakatifu; kwa sababu kwake ni takatifu sana katika sadaka zisongezwazo kwa Bwana kwa moto, kwa amri ya milele.
Mambo ya Walawi 24:10 Leviticus 24:10
Ikawa mwana wa mwanamke wa Kiisraeli, ambaye babaye alikuwa Mmisri, akatokea kati ya wana wa Israeli; na huyo mwana wa mwanamke wa Kiisraeli, na Mwisraeli mmoja, wakapigana pamoja ndani ya marago;
Mambo ya Walawi 24:11 Leviticus 24:11
kisha huyo mwana wa mwanamke wa Kiisraeli akalikufuru hilo Jina, na kuapiza; nao wakamleta kwa Musa. Na jina la mamaye alikuwa akiitwa Shelomithi, binti ya Dibri, wa kabila ya Dani.
Mambo ya Walawi 24:12 Leviticus 24:12
Nao wakamtia kifungoni, ili wapate kuambiwa neno litakalotoka kinywani pa Bwana.
Mambo ya Walawi 24:13 Leviticus 24:13
Na Bwana akasema na Musa, na kumwambia,
Mambo ya Walawi 24:14 Leviticus 24:14
Mtoe huyo aliyeapiza nje ya marago; na wale wote waliomsikia na waweke mikono yao kichwani mwake, kisha mkutano wote na wamwue kwa kumpiga kwa mawe.
Mambo ya Walawi 24:15 Leviticus 24:15
Nawe nena na wana wa Israeli na kuwaambia, Mtu awaye yote atakayemlaani Mungu wake atachukua dhambi yake.
Mambo ya Walawi 24:16 Leviticus 24:16
Na yeye atakayelikufuru jina la Bwana hakika atauawa; mkutano wote watamwua kwa kumpiga kwa mawe; kama ni mgeni, kama ni mzalia, hapo atakapolikufuru jina la Bwana atauawa.
Mambo ya Walawi 24:17 Leviticus 24:17
Na mtu ampigaye mtu hata akafa, lazima atauawa;
Mambo ya Walawi 24:18 Leviticus 24:18
na atakayempiga mnyama hata akafa atalipa; uhai kwa uhai.
Mambo ya Walawi 24:19 Leviticus 24:19
Na mtu akimtia mwenziwe kilema; vile vile kama alivyofanya, naye atafanyiwa vivyo;
Mambo ya Walawi 24:20 Leviticus 24:20
jeraha kwa jeraha, jicho kwa jicho, jino kwa jino; vile vile kama alivyomtia mtu kilema, naye atalipwa vivyo.
Mambo ya Walawi 24:21 Leviticus 24:21
Na mtu amwuaye mnyama atalipa; na yeye atakayemwua binadamu atauawa.
Mambo ya Walawi 24:22 Leviticus 24:22
Mtakuwa na sheria moja tu, kwa huyo aliye mgeni, na kwa mzalia; kwa kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.
Mambo ya Walawi 24:23 Leviticus 24:23
Musa akanena na wana wa Israeli, nao wakamtoa huyo aliyeapiza nje ya marago, wakamwua kwa kumpiga kwa mawe. Wana wa Israeli wakafanya kama Bwana alivyomwagiza Musa.