Mambo ya Walawi Mlango 18 Leviticus
Mambo ya Walawi 18:1 Leviticus 18:1
Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
Mambo ya Walawi 18:2 Leviticus 18:2
Nena wewe na wana wa Israeli, uwaambie, Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.
Mambo ya Walawi 18:3 Leviticus 18:3
Nanyi msifanye matendo kama yale ya nchi ya Misri mliyokaa; wala msifanye matendo kama yale ya nchi ya Kanaani, nitakayowapeleka; wala msiende katika amri zao hao.
Mambo ya Walawi 18:4 Leviticus 18:4
Mtazifanya hukumu zangu, nanyi mtazishika amri zangu, ili mwenende katika hizo; mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.
Mambo ya Walawi 18:5 Leviticus 18:5
Kwa ajili ya hayo mtazishika amri zangu na hukumu zangu; ambazo mtu akizitumia ataishi kwa hizo; mimi ndimi Bwana.
Mambo ya Walawi 18:6 Leviticus 18:6
Mtu ye yote aliye wa kwenu asimkaribie mwenziwe aliye wa jamaa yake ya karibu ili kumfunua utupu; mimi ndimi Bwana.
Mambo ya Walawi 18:7 Leviticus 18:7
Utupu wa baba yako, wala utupu wa mama yako, usifunue, maana ndiye mama yako; usifunue utupu wake.
Mambo ya Walawi 18:8 Leviticus 18:8
Utupu wa mke wa baba yako, usifunue; maana, ni utupu wa baba yako.
Mambo ya Walawi 18:9 Leviticus 18:9
Utupu wa umbu lako, binti ya baba yako, au binti ya mama yako, kwamba alizaliwa nyumbani mwenu au kwamba alizaliwa kwengine, utupu wa hao usifunue.
Mambo ya Walawi 18:10 Leviticus 18:10
Utupu wa binti ya mwanao mume, au wa binti ya binti yako, utupu wao hao usifunue; kwa kuwa ndio utupu wako mwenyewe.
Mambo ya Walawi 18:11 Leviticus 18:11
Utupu wa binti ya mkewe baba yako, aliyezaliwa na baba yako, yeye ni umbu lako, usifunue utupu wake.
Mambo ya Walawi 18:12 Leviticus 18:12
Usifunue utupu wa umbu lake baba yako; maana, yeye ni jamaa aliye karibu.
Mambo ya Walawi 18:13 Leviticus 18:13
Usifunue utupu wa umbu la mama yako; maana, yeye ni jamaa ya mama yako ya karibu.
Mambo ya Walawi 18:14 Leviticus 18:14
Usifunue utupu wa ndugu ya baba yako, usimkaribie mkewe huyo; yeye ni shangazi lako.
Mambo ya Walawi 18:15 Leviticus 18:15
Usifunue utupu wa mkweo mwanamke; yeye ni mke wa mwanao; usifunue utupu wake huyo.
Mambo ya Walawi 18:16 Leviticus 18:16
Usifunue utupu wa mke wa nduguyo; maana, ni utupu wa nduguyo.
Mambo ya Walawi 18:17 Leviticus 18:17
Usifunue utupu wa mwanamke na binti yake; usimtwae binti ya mwanawe mume, au binti ya binti yake, ili kufunua utupu wake; hao ni jamaa ya karibu; ni uovu mkuu.
Mambo ya Walawi 18:18 Leviticus 18:18
Wala usitwae mwanamke pamoja na nduguye, awe mtesi wake, na kufunua utupu wake, huyo wa pili atakapokuwa yu hai.
Mambo ya Walawi 18:19 Leviticus 18:19
Nawe usimkaribie mwanamke kufunua utupu wake wakati wa kutengwa kwa ajili ya unajisi wake.
Mambo ya Walawi 18:20 Leviticus 18:20
Usilale na mke wa mwenzio, ukajitia unajisi naye.
Mambo ya Walawi 18:21 Leviticus 18:21
Nawe usitoe kizazi chako cho chote na kuwapisha kwa Moleki, wala usilinajisi jina la Mungu wako; mimi ndimi Bwana.
Mambo ya Walawi 18:22 Leviticus 18:22
Usilale na mwanamume mfano wa kulala na mwanamke; ni machukizo.
Mambo ya Walawi 18:23 Leviticus 18:23
Wala usilale na mnyama ye yote, ili kujitia unajisi kwake; wala mwanamke asisimame mbele ya mnyama ili kulala naye; ni uchafuko.
Mambo ya Walawi 18:24 Leviticus 18:24
Msijitie unajisi katika mambo hayo hata mojawapo; kwa maana hizo taifa nitakazozitoa mbele zenu zimekuwa najisi kwa mambo hayo yote;
Mambo ya Walawi 18:25 Leviticus 18:25
na hiyo nchi imekuwa najisi; kwa ajili ya hayo naipatiliza uovu wake juu yake, na hiyo nchi yatapika wenyeji wake na kuwatoa.
Mambo ya Walawi 18:26 Leviticus 18:26
Kwa hiyo mtazishika amri zangu na hukumu zangu, wala msifanye machukizo hayo mojawapo; yeye aliye mzalia, wala mgeni aketiye kati yenu;
Mambo ya Walawi 18:27 Leviticus 18:27
(kwa kuwa hao watu wa nchi wameyafanya machukizo haya yote, hao waliotangulia mbele zenu, na hiyo nchi imekuwa najisi;)
Mambo ya Walawi 18:28 Leviticus 18:28
ili kwamba hiyo nchi isiwatapike na ninyi pia, hapo mtakapoitia unajisi, kama ilivyoitapika hiyo taifa iliyotangulia mbele yenu.
Mambo ya Walawi 18:29 Leviticus 18:29
Kwani mtu awaye yote atakayefanya machukizo hayo mojawapo, nafsi hizo zitakazoyafanya zitakatiliwa mbali na watu wao.
Mambo ya Walawi 18:30 Leviticus 18:30
Kwa ajili ya hayo yashikeni mausia yangu, ili kwamba msifanye kabisa desturi hizi zichukizazo mojawapo, zilizotangulia kufanywa mbele zenu, wala msijitie unajisi katika mambo hayo; mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.