1 Mambo ya Nyakati Mlango 14 1st Chronicles
1 Mambo ya Nyakati 14:1 1stChronicles 14:1
Naye Hiramu, mfalme wa Tiro, akatuma wajumbe kwa Daudi, akampelekea na mierezi, na waashi, na maseremala, ili wamjengee nyumba.
1 Mambo ya Nyakati 14:2 1stChronicles 14:2
Daudi akajua ya kwamba Bwana amemweka imara ili amiliki juu ya Israeli, kwa kuwa milki yake imeinuka kwa ajili ya watu wake Israeli.
1 Mambo ya Nyakati 14:3 1stChronicles 14:3
Tena Daudi akazidi kuoa wake huko Yerusalemu; akazidi Daudi kuzaa wana na binti.
1 Mambo ya Nyakati 14:4 1stChronicles 14:4
Na haya ndiyo majina ya watoto aliozaliwa huko Yerusalemu; Shamua, na Shobabu, na Nathani, na Sulemani;
1 Mambo ya Nyakati 14:5 1stChronicles 14:5
na Ibhari, na Elishua, na Elpeleti;
1 Mambo ya Nyakati 14:6 1stChronicles 14:6
na Noga, na Nefegi, na Yafia;
1 Mambo ya Nyakati 14:7 1stChronicles 14:7
na Elishama, na Eliada, na Elifeleti.
1 Mambo ya Nyakati 14:8 1stChronicles 14:8
Na waliposikia hao Wafilisti ya kwamba Daudi ametiwa mafuta ili awe mfalme juu ya Israeli wote, Wafilisti wote wakapanda kumtafuta Daudi; naye Daudi akasikia, akatoka nje kupigana nao.
1 Mambo ya Nyakati 14:9 1stChronicles 14:9
Basi hao Wafilisti walikuwa wamekuja na kuteka nyara katika bonde la Warefai.
1 Mambo ya Nyakati 14:10 1stChronicles 14:10
Daudi akamwuliza Mungu, kusema, Je! Nipande juu ya Wafilisti! Utawatia mikononi mwangu? Naye Bwana akamwambia, Panda; kwa kuwa nitawatia mikononi mwako.
1 Mambo ya Nyakati 14:11 1stChronicles 14:11
Basi wakapanda mpaka Baal-perasimu, Daudi naye akawapiga huko; Daudi akasema, Bwana amewafurikia adui zangu kwa mkono wangu, kama mafuriko ya maji. Basi wakapaita mahali pale jina lake Baal-perasimu.
1 Mambo ya Nyakati 14:12 1stChronicles 14:12
Nao wakaiacha miungu yao huko; naye Daudi akaamuru, ikateketezwa kwa moto.
1 Mambo ya Nyakati 14:13 1stChronicles 14:13
Lakini hao Wafilisti wakateka nyara tena mara ya pili bondeni.
1 Mambo ya Nyakati 14:14 1stChronicles 14:14
Na Daudi akamwuliza Mungu tena; naye Mungu akamwambia, Hutapanda kuwafuata; uwageukie mbali, ukawajie huko kuielekea miforsadi.
1 Mambo ya Nyakati 14:15 1stChronicles 14:15
Kisha itakuwa utakapoisikia sauti ya kwenda katika vilele vya miforsadi, ndipo utakapokwenda nje vitani; kwa maana ndipo Mungu ametoka mbele yako, awapige jeshi la Wafilisti.
1 Mambo ya Nyakati 14:16 1stChronicles 14:16
Daudi akafanya kama vile Mungu alivyomwamuru; wakawapiga jeshi la Wafilisti toka Geba mpaka Gezeri.
1 Mambo ya Nyakati 14:17 1stChronicles 14:17
Sifa za Daudi zikafika nchi zote; naye Bwana akawaletea mataifa yote hofu yake.