1 Mambo ya Nyakati Mlango 3 1st Chronicles

1 Mambo ya Nyakati 3:1 1stChronicles 3:1

Basi hawa ndio wana wa Daudi, aliozaliwa huko Hebroni; Amnoni, mzaliwa wa kwanza, mwana wa Ahinoamu, Myezreeli; wa pili, Danieli, wa Abigaili, Mkarmeli;

1 Mambo ya Nyakati 3:2 1stChronicles 3:2

wa tatu, Absalomu, mwana wa Maaka, binti Talmai, mfalme wa Geshuri; wa nne, Adoniya, mwana wa Hagithi;

1 Mambo ya Nyakati 3:3 1stChronicles 3:3

wa tano, Shefatia, wa Abitali; wa sita, Ithreamu, kwa Egla, mkewe.

1 Mambo ya Nyakati 3:4 1stChronicles 3:4

Sita alizaliwa huko Hebroni; na huko akamiliki miaka saba na miezi sita; na huko Yerusalemu akamiliki miaka thelathini na mitatu.

1 Mambo ya Nyakati 3:5 1stChronicles 3:5

Na hawa alizaliwa huko Yerusalemu; Shamua, na Shobabu, na Nathani, na Sulemani, wanne, wana wa Bathsheba, binti Eliamu;

1 Mambo ya Nyakati 3:6 1stChronicles 3:6

na Ibhari, na Elishua, na Elipeleti;

1 Mambo ya Nyakati 3:7 1stChronicles 3:7

na Noga, na Nefegi, na Yafia;

1 Mambo ya Nyakati 3:8 1stChronicles 3:8

na Elishama, na Eliada, na Elifeleti, watu kenda.

1 Mambo ya Nyakati 3:9 1stChronicles 3:9

Hao wote walikuwa wana wa Daudi, mbali na wana wa masuria; na Tamari alikuwa umbu lao.

1 Mambo ya Nyakati 3:10 1stChronicles 3:10

Na mwanawe Sulemani alikuwa Rehoboamu; na mwanawe huyo alikuwa Abiya; na mwanawe huyo ni Asa; na mwanawe huyo ni Yehoshafati;

1 Mambo ya Nyakati 3:11 1stChronicles 3:11

na mwanawe huyo ni Yehoramu; na mwanawe huyo ni Ahazia; na mwanawe huyo ni Yoashi;

1 Mambo ya Nyakati 3:12 1stChronicles 3:12

na mwanawe huyo ni Amazia; na mwanawe huyo ni Uzia; na mwanawe huyo ni Yothamu;

1 Mambo ya Nyakati 3:13 1stChronicles 3:13

na mwanawe huyo ni Ahazi; na mwanawe huyo ni Hezekia; na mwanawe huyo ni Manase;

1 Mambo ya Nyakati 3:14 1stChronicles 3:14

na mwanawe huyo ni Amoni; na mwanawe huyo ni Yosia.

1 Mambo ya Nyakati 3:15 1stChronicles 3:15

Na wana wa Yosia walikuwa hawa; Yohana mzaliwa wa kwanza, wa pili Yehoyakimu, wa tatu Sedekia, wa nne Shalumu.

1 Mambo ya Nyakati 3:16 1stChronicles 3:16

Na wana wa Yehoyakimu ni hawa; mwanawe Yekonia, na mwanawe Sedekia.

1 Mambo ya Nyakati 3:17 1stChronicles 3:17

Na wana wa Yekonia, huyo aliyechukuliwa mateka; mwanawe Shealtieli,

1 Mambo ya Nyakati 3:18 1stChronicles 3:18

na Malkiramu, na Pedaya, na Shenazari, na Yekamia, na Hoshama, na Nedabia.

1 Mambo ya Nyakati 3:19 1stChronicles 3:19

Na wana wa Pedaya; Zerubabeli, na Shimei; na wana wa Zerubabeli; Meshulamu na Hanania; na Shelomithi alikuwa umbu lao;

1 Mambo ya Nyakati 3:20 1stChronicles 3:20

na Hashuba, na Oheli, na Berekia, na Hasadia, na Yushab-Hesedi, watu watano.

1 Mambo ya Nyakati 3:21 1stChronicles 3:21

Na wana wa Hanania; Pelatia na Yeshaya; na wana wa Refaya, na wana wa Arnani, na wana wa Obadia, na wana wa Shekania.

1 Mambo ya Nyakati 3:22 1stChronicles 3:22

Na wana wa Shekania ni hawa; Shemaya, na wana wa Shemaya; Hatushi, na Igali, na Baria, na Nearia, na Shafati, watu sita.

1 Mambo ya Nyakati 3:23 1stChronicles 3:23

Na wana wa Nearia; Elioenai, na Hezekia, na Azrikamu, watu watatu.

1 Mambo ya Nyakati 3:24 1stChronicles 3:24

Na wana wa Elioenai; Hodavia, na Eliashibu, na Pelaya, na Akubu, na Yohana, na Delaya, na Anani, watu saba.