1 Mambo ya Nyakati Mlango 18 1st Chronicles
1 Mambo ya Nyakati 18:1 1stChronicles 18:1
Ikawa baadaye, Daudi akawapiga Wafilisti, akawashinda, akautwaa Gathi na vijiji vyake mikononi mwa Wafilisti.
1 Mambo ya Nyakati 18:2 1stChronicles 18:2
Akapiga Moabu; na hao Wamoabi wakawa watumwa wa Daudi wakaleta zawadi.
1 Mambo ya Nyakati 18:3 1stChronicles 18:3
Tena Daudi akampiga Hadadezeri, mfalme wa Soba, mpaka Hamathi, alipokwenda kujisimamishia mamlaka yake kwenye mto wa Frati.
1 Mambo ya Nyakati 18:4 1stChronicles 18:4
Daudi akampokonya magari elfu, na wapanda farasi saba elfu, na askari waendao kwa miguu ishirini elfu; Daudi akawakata mshipa farasi wote wa magari, ila wa magari mia akawaweka.
1 Mambo ya Nyakati 18:5 1stChronicles 18:5
Na Washami wa Dameski walipokuja wamsaidie Hadadezeri, mfalme wa Soba, Daudi akapiga katika hao Washami watu ishirini na mbili elfu.
1 Mambo ya Nyakati 18:6 1stChronicles 18:6
Ndipo Daudi akaweka ngome katika Shamu ya Dameski; nao Washami wakawa watumwa wa Daudi, wakaleta zawadi. Naye Bwana akampa Daudi kushinda kila alikokwenda.
1 Mambo ya Nyakati 18:7 1stChronicles 18:7
Tena Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizovaliwa na watumishi wa Hadadezeri akazileta Yerusalemu.
1 Mambo ya Nyakati 18:8 1stChronicles 18:8
Tena toka Tibhathi, na toka Berothai, miji ya Hadadezeri, Daudi akatwaa shaba nyingi mno, aliyofanyizia Sulemani ile bahari ya shaba, na zile nguzo, na vile vyombo vya shaba.
1 Mambo ya Nyakati 18:9 1stChronicles 18:9
Hata aliposikia Tou, mfalme wa Hamathi, ya kuwa Daudi amewapiga jeshi lote la Hadadezeri, mfalme wa Soba,
1 Mambo ya Nyakati 18:10 1stChronicles 18:10
akampeleka mwanawe Hadoramu kwa mfalme Daudi, ili kumsalimia, na kumbarikia, kwa sababu alikuwa amepigana na Hadadezeri, na kumpiga; kwa maana Hadadezeri alikuwa amepigana vita juu ya Tou; naye akaleta vyombo vya dhahabu, na fedha, na shaba, vya namna zote.
1 Mambo ya Nyakati 18:11 1stChronicles 18:11
Hivi pia mfalme Daudi akavifanya wakfu kwa Bwana, pamoja na hiyo fedha na dhahabu, aliyoteka nyara kwa mataifa yote; kwa Edomu, na kwa Moabu, na kwa wana wa Amoni, na kwa Wafilisti, na kwa Amaleki.
1 Mambo ya Nyakati 18:12 1stChronicles 18:12
Tena Abishai, mwana wa Seruya, akawapiga wa Waedomi katika Bonde la Chumvi watu kumi na nane elfu.
1 Mambo ya Nyakati 18:13 1stChronicles 18:13
Akaweka ngome katika Edomu; na Waedomi wote wakawa watumwa wa Daudi. Naye Bwana akampa Daudi kushinda, kila alikokwenda.
1 Mambo ya Nyakati 18:14 1stChronicles 18:14
Basi Daudi akatawala juu ya Israeli wote; akawafanyia hukumu na haki watu wake wote.
1 Mambo ya Nyakati 18:15 1stChronicles 18:15
Na Yoabu mwana wa Seruya akawa juu ya jeshi; na Yehoshafati mwana wa Ahiludi mwenye kuandika tarehe.
1 Mambo ya Nyakati 18:16 1stChronicles 18:16
Na Sadoki mwana wa Ahitubu, na Ahimeleki mwana wa Abiathari, walikuwa makuhani; na Shausha mwandishi;
1 Mambo ya Nyakati 18:17 1stChronicles 18:17
na Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa juu ya Wakerethi na Wapelethi; na wana wa Daudi walikuwa wakuu kumzunguka mfalme.