1 Mambo ya Nyakati Mlango 2 1st Chronicles
1 Mambo ya Nyakati 2:1 1stChronicles 2:1
Hawa ndio wana wa Israeli; Reubeni, na Simeoni, na Lawi, na Yuda, na Isakari, na Zabuloni;
1 Mambo ya Nyakati 2:2 1stChronicles 2:2
na Dani, na Yusufu, na Benyamini, na Naftali, na Gadi, na Asheri.
1 Mambo ya Nyakati 2:3 1stChronicles 2:3
Wana wa Yuda; Eri, na Onani, na Shela; ambao hao watatu alizaliwa na binti Shua, Mkanaani. Naye Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mbaya machoni pa Bwana; naye akamwua.
1 Mambo ya Nyakati 2:4 1stChronicles 2:4
Na Tamari, mkwewe, akamzalia Peresi, na Zera. Wana wote wa Yuda ni watano.
1 Mambo ya Nyakati 2:5 1stChronicles 2:5
Wana wa Peresi; Hesroni, na Hamuli.
1 Mambo ya Nyakati 2:6 1stChronicles 2:6
Na wana wa Zera; Zabdi, na Ethani, na Hemani, na Kalkoli, na Darda; hao wote ni watano.
1 Mambo ya Nyakati 2:7 1stChronicles 2:7
Na wana wa Karmi; Akani, yule mwenye kutaabisha Israeli, aliyekosa katika kitu kilichowekwa wakfu.
1 Mambo ya Nyakati 2:8 1stChronicles 2:8
Na wana wa Ethani; Azaria.
1 Mambo ya Nyakati 2:9 1stChronicles 2:9
Tena wana wa Hesroni aliozaliwa; Yerameeli, na Ramu, na Kalebu.
1 Mambo ya Nyakati 2:10 1stChronicles 2:10
Na Ramu akamzaa Aminadabu; na Aminadabu akamzaa Nashoni, mkuu wa wana wa Yuda;
1 Mambo ya Nyakati 2:11 1stChronicles 2:11
na Nashoni akamzaa Salmoni; na Salmoni akamzaa Boazi;
1 Mambo ya Nyakati 2:12 1stChronicles 2:12
na Boazi akamzaa Obedi; na Obedi akamzaa Yese;
1 Mambo ya Nyakati 2:13 1stChronicles 2:13
na Yese akamzaa Eliabu, mzaliwa wake wa kwanza, na wa pili Abinadabu, na wa tatu Shama;
1 Mambo ya Nyakati 2:14 1stChronicles 2:14
na wa nne Nethaneli, na wa tano Radai;
1 Mambo ya Nyakati 2:15 1stChronicles 2:15
na wa sita Ozemu, na wa saba Daudi;
1 Mambo ya Nyakati 2:16 1stChronicles 2:16
na maumbu yao ni Seruya, na Abigaili. Na wana wa Seruya walikuwa, Abishai, na Yoabu, na Asaheli; hao watatu.
1 Mambo ya Nyakati 2:17 1stChronicles 2:17
Na Abigaili akamzaa Amasa; na babaye Amasa ni Yetheri, Mwishmaeli.
1 Mambo ya Nyakati 2:18 1stChronicles 2:18
Basi Kalebu, mwana wa Hesroni, akazaliwa wana na mkewe Azubu, na Yeriothi, na hawa ndio wanawe wa kiume; Yesheri, na Shobabu, na Ardoni.
1 Mambo ya Nyakati 2:19 1stChronicles 2:19
Akafa Azuba, naye Kalebu akamtwaa Efrathi, aliyemzalia Huri.
1 Mambo ya Nyakati 2:20 1stChronicles 2:20
Naye Huri akamzaa Uri; na Uri akamzaa Besaleli.
1 Mambo ya Nyakati 2:21 1stChronicles 2:21
Na baadaye Hesroni akamwingilia binti wa Makiri, babaye Gileadi; ambaye alimtwaa alipokuwa mwenye miaka sitini; naye akamzalia Segubu.
1 Mambo ya Nyakati 2:22 1stChronicles 2:22
Na Segubu akamzaa Yairi, aliyekuwa mwenye miji ishirini na mitatu katika nchi ya Gileadi.
1 Mambo ya Nyakati 2:23 1stChronicles 2:23
Na Geshuri na Aramu wakawapokonya miji ya Yairi, pamoja na Kenathi na miji yake, jumla yote miji sitini. Hao wote ni wana wa Makiri, babaye Gileadi.
1 Mambo ya Nyakati 2:24 1stChronicles 2:24
Tena, baada ya kufa kwake Hesroni huko Kalebu-Efrata, ndipo Abia, mkewe Hesroni, alipomzalia Ashuri, babaye Teboa.
1 Mambo ya Nyakati 2:25 1stChronicles 2:25
Na wana wa Yerameeli, mzaliwa wa kwanza wa Hesroni, walikuwa Ramu, mzaliwa wa kwanza, na Buna, na Oreni, na Ozemu; kwa Ahiya.
1 Mambo ya Nyakati 2:26 1stChronicles 2:26
Naye Yerameeli alikuwa na mke mwingine, jina lake Atara; yeye alikuwa mamaye Onamu.
1 Mambo ya Nyakati 2:27 1stChronicles 2:27
Na wana wa Ramu, mzaliwa wa kwanza wa Yerameeli, walikuwa Maasi, na Yamini, na Ekeri.
1 Mambo ya Nyakati 2:28 1stChronicles 2:28
Na wana wa Onamu walikuwa Shamai, na Yada; na wana wa Shamai; Nadabu, na Abishuri.
1 Mambo ya Nyakati 2:29 1stChronicles 2:29
Na mkewe Abishuri aliitwa jina lake Abihaili; naye akamzalia Abani, na Molidi.
1 Mambo ya Nyakati 2:30 1stChronicles 2:30
Na wana wa Nadabu; Seledi, na Apaimu; walakini Seledi alikufa hana watoto.
1 Mambo ya Nyakati 2:31 1stChronicles 2:31
Na wana wa Apaimu; Ishi. Na wana wa Ishi; Sheshani. Na wana wa Sheshani; Alai.
1 Mambo ya Nyakati 2:32 1stChronicles 2:32
Na wana wa Yada, nduguye Shamai; Yetheri, na Yonathani; naye Yetheri akafa hana watoto.
1 Mambo ya Nyakati 2:33 1stChronicles 2:33
Na wana wa Yonathani; Pelethi, na Zaza. Hao ndio wana wa Yerameeli.
1 Mambo ya Nyakati 2:34 1stChronicles 2:34
Basi huyo Sheshani alikuwa hana wana wa kiume, ila binti. Naye Sheshani alikuwa na mtumwa, Mmisri, jina lake akiitwa Yarha.
1 Mambo ya Nyakati 2:35 1stChronicles 2:35
Basi akamwoza binti yake aolewe na Yarha, mtumwa wake; naye akamzalia Atai.
1 Mambo ya Nyakati 2:36 1stChronicles 2:36
Na Atai akamzaa Nathani; na Nathani akamzaa Zabadi;
1 Mambo ya Nyakati 2:37 1stChronicles 2:37
na Zabadi akamzaa Eflali; na Eflali akamzaa Obedi;
1 Mambo ya Nyakati 2:38 1stChronicles 2:38
na Obedi akamzaa Yehu; na Yehu akamzaa Azaria;
1 Mambo ya Nyakati 2:39 1stChronicles 2:39
na Azaria akamzaa Helesi; na Helesi akamzaa Eleasa
1 Mambo ya Nyakati 2:40 1stChronicles 2:40
na Eleasa akamzaa Sismai; na Sismai akamzaa Shalumu;
1 Mambo ya Nyakati 2:41 1stChronicles 2:41
na Shalumu akamzaa Yekamia; na Yekamia akamzaa Elishama.
1 Mambo ya Nyakati 2:42 1stChronicles 2:42
Na wana wa Kalebu, nduguye Yerameeli, walikuwa Mesha, mzaliwa wake wa kwanza, aliyekuwa babaye Zifu; na wana wa Maresha, babaye Hebroni.
1 Mambo ya Nyakati 2:43 1stChronicles 2:43
Na wana wa Hebroni; Kora, na Tapua, na Rekemu, na Shema.
1 Mambo ya Nyakati 2:44 1stChronicles 2:44
Naye Shema akamzaa Rahamu, babaye Yorkeamu; na Rekemu akamzaa Shamai.
1 Mambo ya Nyakati 2:45 1stChronicles 2:45
Na mwana wake Shamai alikuwa Maoni; na Maoni alikuwa babaye Bethsuri.
1 Mambo ya Nyakati 2:46 1stChronicles 2:46
Naye Efa, suria yake Kalebu, alimzaa Harani, na Mosa, na Gazezi; naye Harani akamzaa Gazezi.
1 Mambo ya Nyakati 2:47 1stChronicles 2:47
Na wana wa Yadai; Regemu, na Yothamu, na Geshani, na Peleti, na Efa, na Shaafu.
1 Mambo ya Nyakati 2:48 1stChronicles 2:48
Naye Maaka, suria yake Kalebu, akamzalia Sheberi, na Tirhana.
1 Mambo ya Nyakati 2:49 1stChronicles 2:49
Tena akamzaa Shaafu, babaye Madmana; na Sheva babaye Makbena; na babaye Gibea; naye binti Kalebu alikuwa Aksa.
1 Mambo ya Nyakati 2:50 1stChronicles 2:50
Hao walikuwa wana wa Kalebu. Wana wa Huri, mzaliwa wa kwanza wa Efrathi; Shobali, babaye Kiriath-Yearimu;
1 Mambo ya Nyakati 2:51 1stChronicles 2:51
Salma, babaye Bethlehemu; na Harefu, babaye Beth-gaderi.
1 Mambo ya Nyakati 2:52 1stChronicles 2:52
Naye Shobali, babaye Kiriath-Yearimu, alikuwa na wana; Haroe, na nusu ya Wamenuhothi.
1 Mambo ya Nyakati 2:53 1stChronicles 2:53
Na jamaa za Kiriath-Yearimu; Waithri, na Waputhi, na Washumathi, na Wamishrai; katika hao walitoka Wasorathi, na Waeshtaoli.
1 Mambo ya Nyakati 2:54 1stChronicles 2:54
Na wana wa Salma; Bethlehemu, na Wanetofathi, Atroth-beth-Yoabu, na nusu ya Wamenuhothi, na Wazori.
1 Mambo ya Nyakati 2:55 1stChronicles 2:55
Na jamaa za waandishi waliokaa Yabesi; Watirathi, na Washimeathi, na Wasukathi. Hao ndio Wakeni, waliotoka kwake Hamathi, babaye mbari ya Rekabu.