1 Mambo ya Nyakati Mlango 7 1st Chronicles

1 Mambo ya Nyakati 7:1 1stChronicles 7:1

Na wana wa Isakari; Tola, na Puva, na Yashubu, na Shimroni, wanne.

1 Mambo ya Nyakati 7:2 1stChronicles 7:2

Na wana wa Tola; Uzi, na Refaya, na Yerieli, na Yamai, na Ibsamu, na Shemueli, wakuu wa mbari za baba zao, yaani, wa Tola; watu hodari wa vita katika vizazi vyao; hesabu yao katika siku za Daudi ilikuwa watu ishirini na mbili elfu na mia sita.

1 Mambo ya Nyakati 7:3 1stChronicles 7:3

Na wana wa Uzi; Izrahia; na wana wa Izrahia; Mikaeli, na Obadia, na Yoeli, na Ishia, watano; wote wakuu.

1 Mambo ya Nyakati 7:4 1stChronicles 7:4

Na pamoja nao, katika vizazi vyao, sawasawa na mbari za baba zao, walikuwapo vikosi vya jeshi la vita, watu thelathini na sita elfu; kwa kuwa wake zao na watoto wao walikuwa wengi.

1 Mambo ya Nyakati 7:5 1stChronicles 7:5

Na ndugu zao katika jamaa zote za Isakari, watu hodari wa vita, wakihesabiwa kwa vizazi vyao, walikuwa watu themanini na saba elfu.

1 Mambo ya Nyakati 7:6 1stChronicles 7:6

Wana wa Benyamini; Bela, na Bekeri, na Yediaeli, watatu.

1 Mambo ya Nyakati 7:7 1stChronicles 7:7

Na wana wa Bela; Esboni, na Uzi, na Uzieli, na Yerimothi, na Iri, watano; wakuu wa mbari za baba zao, watu hodari wa vita; nao wakahesabiwa kwa vizazi vyao watu ishirini na mbili elfu na thelathini na wanne.

1 Mambo ya Nyakati 7:8 1stChronicles 7:8

Na wana wa Bekeri; Zemira, na Yoashi, na Eliezeri, na Elioenai, na Omri, na Yeremothi, na Abiya, na Anathothi, na Alemethi. Hao wote ndio wana wa Bekeri.

1 Mambo ya Nyakati 7:9 1stChronicles 7:9

Nao wakahesabiwa kwa vizazi vyao, katika vizazi vyao, wakuu wa mbari za baba zao, watu hodari wa vita, jumla yao watu ishirini elfu na mia mbili.

1 Mambo ya Nyakati 7:10 1stChronicles 7:10

Na wana wa Yediaeli; Bilhani; na wana wa Bilhani; Yeushi, na Benyamini, na Ehudi, na Kenaana, na Zethani, na Tarshishi, na Ahishahari.

1 Mambo ya Nyakati 7:11 1stChronicles 7:11

Hao wote ndio wana wa Yediaeli, sawasawa na wakuu wa mbari za baba zao, watu hodari wa vita, kumi na saba elfu na mia mbili, wawezao kwenda vitani katika jeshi.

1 Mambo ya Nyakati 7:12 1stChronicles 7:12

Tena Shupimu, na Hupimu, wana wa Iri; na Hushimu, wana wa Aheri.

1 Mambo ya Nyakati 7:13 1stChronicles 7:13

Wana wa Naftali; Yaseeli, na Guni, na Yeseri, na Shilemu; wana wa Bilha.

1 Mambo ya Nyakati 7:14 1stChronicles 7:14

Wana wa Manase; Asrieli, ambaye suria yake, Mwarami, alimzalia, akamzalia na Makiri babaye Gileadi;

1 Mambo ya Nyakati 7:15 1stChronicles 7:15

naye Makiri akatwaa mke kwa Hupimu na Shupimu, ambao umbu lao aliitwa Maaka; na wa pili akaitwa jina lake Selofehadi; na Selofehadi alikuwa na binti.

1 Mambo ya Nyakati 7:16 1stChronicles 7:16

Na Maaka mkewe Makiri, akamzalia mwana, akamwita jina lake Pereshi; na jina la nduguye aliitwa Shereshi; na wanawe walikuwa Ulamu, na Rakemu.

1 Mambo ya Nyakati 7:17 1stChronicles 7:17

Na wana wa Ulamu; Bedani. Hao ndio wana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase.

1 Mambo ya Nyakati 7:18 1stChronicles 7:18

Na umbu lake, Hamolekethi, akamzaa Ish-hodu, na Abiezeri, na Mala.

1 Mambo ya Nyakati 7:19 1stChronicles 7:19

Na wana wa Shemida walikuwa Ahiani, na Shekemu, na Liki, na Aniamu.

1 Mambo ya Nyakati 7:20 1stChronicles 7:20

Na wana wa Efraimu; Shuthela, na mwanawe huyo ni Beredi, na mwanawe huyo ni Tahathi, na mwanawe huyo ni Ekada, na mwanawe huyo ni Tahathi;

1 Mambo ya Nyakati 7:21 1stChronicles 7:21

na mwanawe huyo ni Zabadi, na mwanawe huyo ni Shuthela; na Ezeri na Ekadi, ambao watu wa Gathi, wenyeji wa nchi, waliwaua, kwa sababu walishuka ili kuzipokonya ng'ombe zao.

1 Mambo ya Nyakati 7:22 1stChronicles 7:22

Na Efraimu, baba yao, akaomboleza siku nyingi, wakaja nduguze ili kumfariji.

1 Mambo ya Nyakati 7:23 1stChronicles 7:23

Naye akamwingilia mkewe, naye akachukua mimba na kuzaa mwana, akamwita jina lake Beria, kwa sababu mna mabaya nyumbani mwake.

1 Mambo ya Nyakati 7:24 1stChronicles 7:24

Na binti yake alikuwa Sheera, ambaye alijenga Beth-horoni, wa chini na wa juu, na Uzen-sheera.

1 Mambo ya Nyakati 7:25 1stChronicles 7:25

Mwanawe ni Refa, na Reshefu, na mwanawe huyo ni Tela, na mwanawe huyo ni Tahani;

1 Mambo ya Nyakati 7:26 1stChronicles 7:26

na mwanawe huyo ni Ladani, na mwanawe huyo ni Amihudi, na mwanawe huyo ni Elishama;

1 Mambo ya Nyakati 7:27 1stChronicles 7:27

na mwanawe huyo ni Nuni, na mwanawe huyo ni Yoshua.

1 Mambo ya Nyakati 7:28 1stChronicles 7:28

Na hizi ndizo hozi zao na makao yao; Betheli na vijiji vyake, na upande wa mashariki Naara, na upande wa magharibi Gezeri na vijiji vyake; na Shekemu pia na vijiji vyake, hata Aza na vijiji vyake;

1 Mambo ya Nyakati 7:29 1stChronicles 7:29

na mipakani mwa wana wa Manase; Beth-sheani na vijiji vyake; na Taanaki na vijiji vyake; na Megido na vijiji vyake; na Dori na vijiji vyake. Katika miji hiyo walikaa wana wa Yusufu, mwana wa Israeli.

1 Mambo ya Nyakati 7:30 1stChronicles 7:30

Wana wa Asheri; Imna, na Ishva, na Ishvi, na Beria, na umbu lao, Sera.

1 Mambo ya Nyakati 7:31 1stChronicles 7:31

Na wana wa Beria; Heberi, na Malkieli, aliyekuwa babaye Birzaithi.

1 Mambo ya Nyakati 7:32 1stChronicles 7:32

Na Heberi akamzaa Yafleti, na Shomeri, na Hothamu, na umbu lao, Shua.

1 Mambo ya Nyakati 7:33 1stChronicles 7:33

Na wana wa Yafleti; Pasaki, na Bimhali, na Ashvathi. Hao ndio wana wa Yafleti.

1 Mambo ya Nyakati 7:34 1stChronicles 7:34

Na wana wa Shomeri; Ahi, na Roga, na Yehuba, na Aramu.

1 Mambo ya Nyakati 7:35 1stChronicles 7:35

Na wana wa nduguye Helemu; Sofa, na Imna, na Sheleshi, na Amali.

1 Mambo ya Nyakati 7:36 1stChronicles 7:36

Wana wa Sofa; Sua, na Harneferi, na Shuali, na Beri, na Imra;

1 Mambo ya Nyakati 7:37 1stChronicles 7:37

na Bezeri, na Hodu, na Shama, na Shilsha, na Ithrani, na Beera.

1 Mambo ya Nyakati 7:38 1stChronicles 7:38

Na wana wa Yetheri; Yefune, na Pispa, na Ara.

1 Mambo ya Nyakati 7:39 1stChronicles 7:39

Na wana wa Ula; Ara, na Hanieli na Risia.

1 Mambo ya Nyakati 7:40 1stChronicles 7:40

Hao wote ndio wana wa Asheri, wakuu wa mbari za baba zao, watu wateule, hodari wa vita, wakuu wa mashehe. Na hesabu yao waliojumlishwa kwa vizazi vyao kwenda vitani walikuwa watu ishirini na sita elfu.