1 Mambo ya Nyakati Mlango 10 1st Chronicles
1 Mambo ya Nyakati 10:1 1stChronicles 10:1
Basi Wafilisti wakapigana juu ya Israeli; nao watu wa Israeli wakakimbia mbele ya Wafilisti, wakaanguka wameuawa katika mlima Gilboa.
1 Mambo ya Nyakati 10:2 1stChronicles 10:2
Nao Wafilisti wakamfuatia sana Sauli na wanawe; Wafilisti wakawaua Yonathani, na Abinadabu, na Malkishua, wana wa Sauli.
1 Mambo ya Nyakati 10:3 1stChronicles 10:3
Tena vita vilikuwa vikali sana juu ya Sauli, na wapiga upinde wakampata; hata akafadhaika sana kwa sababu ya wapiga upinde.
1 Mambo ya Nyakati 10:4 1stChronicles 10:4
Ndipo Sauli akamwambia yule mchukua silaha zake, Futa upanga wako, unichome nao, wasije watu hawa wasiotahiriwa wakanisimanga. Lakini huyo mchukua silaha zake akakataa; kwa sababu aliogopa sana. Basi Sauli akautwaa upanga wake, akauangukia.
1 Mambo ya Nyakati 10:5 1stChronicles 10:5
Na mchukua silaha zake alipoona ya kuwa Sauli amekufa, yeye naye akauangukia upanga wake, akafa.
1 Mambo ya Nyakati 10:6 1stChronicles 10:6
Hivyo Sauli akafa, na wanawe watatu; na nyumba yake yote wakafa pamoja.
1 Mambo ya Nyakati 10:7 1stChronicles 10:7
Kisha watu wote wa Israeli, waliokuwa huko bondeni, walipoona ya kuwa wamekimbia, na ya kuwa Sauli na wanawe wamekufa, wakaiacha miji yao, wakakimbia; nao Wafilisti wakaenda wakakaa humo.
1 Mambo ya Nyakati 10:8 1stChronicles 10:8
Hata ikawa siku ya pili yake Wafilisti walipokwenda kuwateka nyara hao waliouawa, walimwona Sauli na wanawe wameanguka juu ya mlima Gilboa.
1 Mambo ya Nyakati 10:9 1stChronicles 10:9
Wakamvua mavazi, wakamtwalia kichwa, na silaha zake, kisha wakapeleka wajumbe kwenda nchi ya Wafilisti pande zote, ili kutangaza habari kwa sanamu zao, na kwa watu.
1 Mambo ya Nyakati 10:10 1stChronicles 10:10
Wakaziweka silaha zake nyumbani mwa miungu yao, wakakikaza kichwa chake nyumbani mwa Dagoni.
1 Mambo ya Nyakati 10:11 1stChronicles 10:11
Na watu wote wa Yabesh-gileadi waliposikia hayo yote Wafilisti waliyomtenda Sauli,
1 Mambo ya Nyakati 10:12 1stChronicles 10:12
wakainuka mashujaa wote, wakautwaa mwili wake Sauli, na miili ya wanawe, wakaileta Yabeshi, wakaizika mifupa yao chini ya mwaloni huko Yabeshi, nao wakafunga muda wa siku saba.
1 Mambo ya Nyakati 10:13 1stChronicles 10:13
Basi Sauli alikufa kwa sababu ya kosa lake alilomkosa Bwana, kwa sababu ya neno la Bwana, asilolishika; na tena kwa kutaka shauri kwa mwenye pepo wa utambuzi, aulize kwake,
1 Mambo ya Nyakati 10:14 1stChronicles 10:14
asiulize kwa Bwana; kwa hiyo akamwua, na ufalme akamgeuzia Daudi, mwana wa Yese.