1 Mambo ya Nyakati Mlango 16 1st Chronicles
1 Mambo ya Nyakati 16:1 1stChronicles 16:1
Wakaliingiza sanduku la Mungu, na kuliweka katikati ya hema aliyoipiga Daudi kwa ajili yake; wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Mungu.
1 Mambo ya Nyakati 16:2 1stChronicles 16:2
Na Daudi alipokwisha kuitoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani, akawabariki watu kwa jina la Bwana.
1 Mambo ya Nyakati 16:3 1stChronicles 16:3
Kisha akawagawia kila mtu wa Israeli, waume kwa wake, kila mtu mkate wa ngano, na kipande cha nyama, na mkate wa zabibu.
1 Mambo ya Nyakati 16:4 1stChronicles 16:4
Akawaagiza baadhi ya Walawi kwamba watumike mbele ya sanduku la Bwana, wamfanyie ukumbusho, na shukrani, na sifa, Bwana, Mungu wa Israeli;
1 Mambo ya Nyakati 16:5 1stChronicles 16:5
Asafu mkuu wao, na wa pili wake Zekaria, na Yeieli, na Shemiramothi, na Yehieli, na Matithiya, na Eliabu, na Benaya, na Obed-edomu, na Yeieli, wenye vinanda na vinubi; naye Asafu mwenye kupiga matoazi;
1 Mambo ya Nyakati 16:6 1stChronicles 16:6
nao makuhani Benaya na Yahazieli wenye baragumu daima, mbele ya sanduku la agano la Mungu.
1 Mambo ya Nyakati 16:7 1stChronicles 16:7
Ndipo siku hiyo Daudi alipoagiza kwanza kumshukuru Bwana, kwa mkono wa Asafu na nduguze.
1 Mambo ya Nyakati 16:8 1stChronicles 16:8
Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake; Wajulisheni watu matendo yake.
1 Mambo ya Nyakati 16:9 1stChronicles 16:9
Mwimbieni, mwimbieni kwa zaburi; Zitafakarini ajabu zake zote.
1 Mambo ya Nyakati 16:10 1stChronicles 16:10
Jisifuni kwa jina lake takatifu; Na ufurahi moyo wao wamtafutao Bwana.
1 Mambo ya Nyakati 16:11 1stChronicles 16:11
Mtakeni Bwana na nguvu zake; Utafuteni uso wake siku zote.
1 Mambo ya Nyakati 16:12 1stChronicles 16:12
Zikumbukeni ajabu zake alizozifanya; Miujiza yake na hukumu za kinywa chake;
1 Mambo ya Nyakati 16:13 1stChronicles 16:13
Enyi wazao wa Israeli, mtumishi wake, Enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
1 Mambo ya Nyakati 16:14 1stChronicles 16:14
Yeye, Bwana, ndiye Mungu wetu; Duniani mwote mna hukumu zake.
1 Mambo ya Nyakati 16:15 1stChronicles 16:15
Likumbukeni agano lake milele, Neno lile aliloviamuru vizazi elfu.
1 Mambo ya Nyakati 16:16 1stChronicles 16:16
Agano alilofanya na Ibrahimu, Na uapo wake kwa Isaka;
1 Mambo ya Nyakati 16:17 1stChronicles 16:17
Alilomthibitishia Yakobo kuwa amri, Na Israeli liwe agano la milele.
1 Mambo ya Nyakati 16:18 1stChronicles 16:18
Akisema, Nitakupa wewe nchi ya Kanaani, Iwe urithi wenu mliopimiwa;
1 Mambo ya Nyakati 16:19 1stChronicles 16:19
Mlipokuwa watu wawezao kuhesabiwa; Naam, watu wachache na wageni ndani yake.
1 Mambo ya Nyakati 16:20 1stChronicles 16:20
Wakatanga-tanga toka taifa hata taifa, Toka ufalme mmoja hata kwa watu wengine.
1 Mambo ya Nyakati 16:21 1stChronicles 16:21
Hakumwacha mtu awaonee; Hata wafalme aliwakemea kwa ajili yao;
1 Mambo ya Nyakati 16:22 1stChronicles 16:22
Akisema, Msiwaguse masihi wangu, Wala msiwadhuru nabii zangu.
1 Mambo ya Nyakati 16:23 1stChronicles 16:23
Mwimbieni Bwana, nchi yote; Tangazeni wokovu wake siku kwa siku.
1 Mambo ya Nyakati 16:24 1stChronicles 16:24
Wahubirini mataifa habari za utukufu wake, Na watu wote habari za maajabu yake.
1 Mambo ya Nyakati 16:25 1stChronicles 16:25
Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kusifiwa sana; Na wa kuhofiwa kuliko miungu yote.
1 Mambo ya Nyakati 16:26 1stChronicles 16:26
Maana miungu yote ya watu si kitu; Lakini Bwana ndiye aliyezifanya mbingu.
1 Mambo ya Nyakati 16:27 1stChronicles 16:27
Heshima na adhama ziko mbele zake; Nguvu na furaha zipo mahali pake.
1 Mambo ya Nyakati 16:28 1stChronicles 16:28
Mpeni Bwana, enyi jamaa za watu, Mpeni Bwana utukufu na nguvu.
1 Mambo ya Nyakati 16:29 1stChronicles 16:29
Mpeni Bwana utukufu wa jina lake; Leteni sadaka, mje mbele zake; Mwabuduni Bwana kwa uzuri wa utakatifu;
1 Mambo ya Nyakati 16:30 1stChronicles 16:30
Tetemekeni mbele zake, nchi yote.
1 Mambo ya Nyakati 16:31 1stChronicles 16:31
Mbingu na zifurahi, nchi na ishangilie; Na waseme katika mataifa, Bwana ametamalaki;
1 Mambo ya Nyakati 16:32 1stChronicles 16:32
Bahari na ivume na vyote viijazavyo; Mashamba na yashangilie na vyote vilivyomo;
1 Mambo ya Nyakati 16:33 1stChronicles 16:33
Ndipo miti yote ya mwituni iimbe kwa furaha,
1 Mambo ya Nyakati 16:34 1stChronicles 16:34
Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
1 Mambo ya Nyakati 16:35 1stChronicles 16:35
Nanyi mkaseme, Ee Mungu wa wokovu wetu, utuokoe, Utukusanye kwa kututoa katika mataifa, Tulishukuru jina lako takatifu, Tuzifanyie shangwe sifa zako.
1 Mambo ya Nyakati 16:36 1stChronicles 16:36
Na ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele hata milele. Na watu wote wakasema, Amina; wakamhimidi Bwana.
1 Mambo ya Nyakati 16:37 1stChronicles 16:37
Basi akawaacha huko, mbele ya sanduku la agano la Bwana, Asafu na nduguze, ili watumike mbele ya sanduku daima, kila siku kama ilivyokuwa kazi yake.
1 Mambo ya Nyakati 16:38 1stChronicles 16:38
Naye Obed-edomu, pamoja na ndugu zao, sitini na wanane; Obed-edomu na mwana wa Yeduthuni, na Hosa, wawe mabawabu;
1 Mambo ya Nyakati 16:39 1stChronicles 16:39
na Sadoki kuhani, na nduguze makuhani, mbele ya maskani ya Bwana katika mahali pa juu palipokuwa huko Gibeoni,
1 Mambo ya Nyakati 16:40 1stChronicles 16:40
ili kumtolea Bwana sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa daima asubuhi na jioni, naam, sawasawa na yote yaliyoandikwa katika torati ya Bwana, aliyowaamuru Israeli;
1 Mambo ya Nyakati 16:41 1stChronicles 16:41
na pamoja nao Hemani na Yeduthuni, na wale wengine waliochaguliwa, waliotajwa majina yao, ili kumshukuru Bwana, kwa kuwa fadhili zake ni za milele;
1 Mambo ya Nyakati 16:42 1stChronicles 16:42
na pamoja nao Hemani na Yeduthuni wenye baragumu na matoazi, kwa hao watakaovumisha sauti, na vinanda kwa ajili ya hizo nyimbo za Mungu; na hao wana wa Yeduthuni wawepo mlangoni.
1 Mambo ya Nyakati 16:43 1stChronicles 16:43
Kisha watu wote wakaenda zao kila mtu nyumbani kwake; naye Daudi akarudi ili awabariki watu wa nyumbani mwake.