2 Samweli Mlango 22 2nd Samuel
Basi Daudi akamwambia Bwana maneno ya wimbo huu, siku ile Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake zote, na mkononi mwa Sauli;
akasema, Bwana ndiye jabali langu, na ngome yangu, na mwokozi wangu, naam, wangu;
Mungu wa mwamba wangu, nitamwamini yeye; Ngao yangu, na pembe ya wokovu wangu, mnara wangu, na makimbilio yangu; Mwokozi wangu, waniokoa na jeuri.
Nitamwita Bwana astahiliye kusifiwa; Hivyo nitaokoka na adui zangu.
Maana mawimbi ya mauti yalinizunguka, Mafuriko ya uovu yakanitia hofu.
Kamba za kuzimu zilinizunguka; Mitego ya mauti ikanikabili.
Katika shida yangu nalimwita Bwana, Naam, nikamlalamikia Mungu wangu;
Ndipo nchi ilipotikisika na kutetemeka, Misingi ya mbinguni ikasuka-suka Na kutikisika, kwa sababu alikuwa na ghadhabu.
Kukapanda moshi kutoka puani mwake, Moto ukatoka kinywani mwake ukala; Makaa yakawashwa nao.
2 Samweli 22:10 2ndSamuel 22:10
Aliziinamisha mbingu akashuka; Kukawa na giza kuu chini ya miguu yake.
2 Samweli 22:11 2ndSamuel 22:11
Akapanda juu ya kerubi akaruka; Naam, alionekana juu ya mabawa ya upepo.
2 Samweli 22:12 2ndSamuel 22:12
Akafanya giza hema zake za kumzunguka, Makusanyiko ya maji, mawingu makuu ya mbinguni.
2 Samweli 22:13 2ndSamuel 22:13
Toka mwangaza uliokuwa mbele zake Makaa ya moto yakawashwa.
2 Samweli 22:14 2ndSamuel 22:14
Bwana alipiga radi toka mbinguni, Naye Aliye juu akaitoa sauti yake.
2 Samweli 22:15 2ndSamuel 22:15
Akapiga mishale, akawatawanya; Umeme, naye akawatapanya.
2 Samweli 22:16 2ndSamuel 22:16
Ndipo ilipoonekana mikondo ya bahari, Misingi ya ulimwengu ikafichuliwa, Kwa kukemea kwake Bwana, Kwa mvumo wa pumzi ya puani mwake.
2 Samweli 22:17 2ndSamuel 22:17
Alipeleka kutoka juu, akanishika; Akanitoa katika maji mengi;
2 Samweli 22:18 2ndSamuel 22:18
Akaniokoa na adui yangu mwenye nguvu, Na wale walionichukia; Maana walikuwa na nguvu kuliko mimi.
2 Samweli 22:19 2ndSamuel 22:19
Walinikabili siku ya msiba wangu; Lakini Bwana alikuwa tegemeo langu.
2 Samweli 22:20 2ndSamuel 22:20
Akanitoa akanipeleka panapo nafasi; Aliniponya kwa kuwa alipendezwa nami.
2 Samweli 22:21 2ndSamuel 22:21
Bwana alinitendea sawasawa na haki yangu; Sawasawa na usafi wa mikono yangu akanilipa.
2 Samweli 22:22 2ndSamuel 22:22
Maana nimezishika njia za Bwana, Wala sikumwasi Mungu wangu.
2 Samweli 22:23 2ndSamuel 22:23
Maana hukumu zake zote zilikuwa mbele yangu; Na kwa habari za amri zake, sikuziacha.
2 Samweli 22:24 2ndSamuel 22:24
Nami nalikuwa mkamilifu kwake, Nikajilinda na uovu wangu.
2 Samweli 22:25 2ndSamuel 22:25
Basi Bwana amenilipa sawasawa na haki yangu; Sawasawa na usafi wa mikono yangu mbele zake.
2 Samweli 22:26 2ndSamuel 22:26
Kwa mtu mwenye fadhili utakuwa mwenye fadhili Kwa mkamilifu utajionyesha kuwa mkamilifu;
2 Samweli 22:27 2ndSamuel 22:27
Kwake ajitakasaye utajionyesha kuwa mtakatifu; Na kwa mpotovu utajionyesha kuwa mkaidi.
2 Samweli 22:28 2ndSamuel 22:28
Na watu wanaoonewa wewe utawaokoa; Ila macho yako ni juu ya wenye kiburi, uwadhili.
2 Samweli 22:29 2ndSamuel 22:29
Kwa kuwa wewe u taa yangu, Ee Bwana; Na Bwana ataniangazia giza langu.
2 Samweli 22:30 2ndSamuel 22:30
Maana kwa msaada wako nafuatia jeshi; Kwa msaada wa Mungu wangu naruka ukuta.
2 Samweli 22:31 2ndSamuel 22:31
Mungu njia yake ni kamilifu; Ahadi ya Bwana imehakikishwa; Yeye ndiye ngao yao Wote wanaomkimbilia.
2 Samweli 22:32 2ndSamuel 22:32
Maana ni nani aliye Mungu, ila Bwana? Ni nani aliye mwamba, ila Mungu wetu?
2 Samweli 22:33 2ndSamuel 22:33
Mungu ndiye ngome yangu yenye nguvu; Naye huwaongoza wakamilifu katika njia yake.
2 Samweli 22:34 2ndSamuel 22:34
Huifanya miguu yangu kuwa kama ya kulungu; Na kunisimamisha mahali pangu pa juu.
2 Samweli 22:35 2ndSamuel 22:35
Ananifundisha mikono yangu vita; Hata mikono yangu yaupinda upinde wa shaba.
2 Samweli 22:36 2ndSamuel 22:36
Nawe umenipa ngao ya wokovu wako; Na unyenyekevu wako umenikuza.
2 Samweli 22:37 2ndSamuel 22:37
Umezifanyizia nafasi hatua zangu, Wala miguu yangu haikuteleza.
2 Samweli 22:38 2ndSamuel 22:38
Nimewafuatia adui zangu, na kuwaangamiza; Wala sikurudi nyuma hata walipokomeshwa.
2 Samweli 22:39 2ndSamuel 22:39
Nami nimewakomesha na kuwapiga-piga wasiweze kusimama; Naam, wameanguka chini ya miguu yangu.
2 Samweli 22:40 2ndSamuel 22:40
Maana umenifunga mshipi wa nguvu kwa vita; Umenitiishia chini yangu walioniondokea.
2 Samweli 22:41 2ndSamuel 22:41
Naam, adui zangu umewafanya wanipe visogo, Ili niwakatilie mbali wanaonichukia.
2 Samweli 22:42 2ndSamuel 22:42
Walitazama, lakini hakuna wa kuokoa; Walimwita Bwana, lakini hakuwajibu.
2 Samweli 22:43 2ndSamuel 22:43
Ndipo nikawaponda kama mavumbi ya nchi, Nikawakanyaga kama matope ya njiani, nikawatawanya.
2 Samweli 22:44 2ndSamuel 22:44
Nawe umeniokoa na mashindano ya watu wangu; Umenihifadhi niwe kichwa cha mataifa; Watu nisiowajua watanitumikia.
2 Samweli 22:45 2ndSamuel 22:45
Wageni watanijia wakinyenyekea; Kwa kusikia tu habari zangu, Mara watanitii.
2 Samweli 22:46 2ndSamuel 22:46
Wageni nao watatepetea, Watatoka katika ngome zao wakitetemeka.
2 Samweli 22:47 2ndSamuel 22:47
Bwana ndiye aliye hai; Na ahimidiwe mwamba wangu; Na atukuzwe Mungu wa mwamba wa wokovu wangu;
2 Samweli 22:48 2ndSamuel 22:48
Naam, Mungu anipatiaye kisasi, Na kuwatweza watu chini yangu,
2 Samweli 22:49 2ndSamuel 22:49
Na kunileta nje nitoke kwa adui zangu; Naam, waniinua juu yao walioniinukia; Waniponya na mtu wa jeuri.
2 Samweli 22:50 2ndSamuel 22:50
Basi, Bwana, nitakushukuru kati ya mataifa, Nami nitaliimbia jina lako.
2 Samweli 22:51 2ndSamuel 22:51
Ampa mfalme wake wokovu mkuu; Amfanyia fadhili masihi wake Daudi na mzao wake ,hata milele.