1 Wakorintho Mlango 16 1st Corinthians
1 Wakorintho 16:1 1stCorinthians 16:1
Kwa habari ya ile changizo kwa ajili ya watakatifu, kama vile nilivyoamuru makanisa ya Galatia, nanyi fanyeni vivyo.
1 Wakorintho 16:2 1stCorinthians 16:2
Siku ya kwanza ya juma kila mtu kwenu na aweke akiba kwake, kwa kadiri ya kufanikiwa kwake; ili kwamba michango isifanyike hapo nitakapokuja;
1 Wakorintho 16:3 1stCorinthians 16:3
nami nitakapofika nitawatuma kwa nyaraka wale mtakaowachagua, wachukue hisani yenu mpaka Yerusalemu.
1 Wakorintho 16:4 1stCorinthians 16:4
Na kama ikifaa niende na mimi, watasafiri pamoja nami.
1 Wakorintho 16:5 1stCorinthians 16:5
Lakini nitakuja kwenu, nikiisha kupita kati ya Makedonia; maana napita kati ya Makedonia.
1 Wakorintho 16:6 1stCorinthians 16:6
Labda nitakaa kwenu; naam, labda wakati wote wa baridi, mpate kunisafirisha ko kote nitakakokwenda.
1 Wakorintho 16:7 1stCorinthians 16:7
Maana sipendi kuonana nanyi sasa, katika kupita tu, kwa sababu nataraji kukaa kwenu muda kidogo, Bwana akinijalia.
1 Wakorintho 16:8 1stCorinthians 16:8
Lakini nitakaa Efeso hata Pentekoste;
1 Wakorintho 16:9 1stCorinthians 16:9
kwa maana nimefunguliwa mlango mkubwa wa kufaa sana, na wako wengi wanipingao.
1 Wakorintho 16:10 1stCorinthians 16:10
Lakini, Timotheo akija, angalieni akae kwenu pasipo hofu; maana anaifanya kazi ya Bwana vile vile kama mimi mwenyewe;
1 Wakorintho 16:11 1stCorinthians 16:11
basi mtu ye yote asimdharau, lakini msafirisheni kwa amani, ili aje kwangu; maana ninamtazamia pamoja na ndugu zetu.
1 Wakorintho 16:12 1stCorinthians 16:12
Lakini kwa habari za Apolo, ndugu yetu, nalimsihi sana aende kwenu pamoja na hao ndugu; ambaye si mapenzi yake kwenda sasa; lakini atakuja atakapopata nafasi.
1 Wakorintho 16:13 1stCorinthians 16:13
Kesheni, simameni imara katika Imani, fanyeni kiume, mkawe hodari.
1 Wakorintho 16:14 1stCorinthians 16:14
Mambo yenu yote na yatendeke katika upendo.
1 Wakorintho 16:15 1stCorinthians 16:15
Tena ndugu, nawasihi; (mnawajua watu wa nyumbani mwa Stefana kwamba ni malimbuko ya Akaya, nao wamejitia katika kazi ya kuwahudumu watakatifu);
1 Wakorintho 16:16 1stCorinthians 16:16
watiini watu kama hawa, na kila mtu afanyaye kazi pamoja nao, na kujitaabisha.
1 Wakorintho 16:17 1stCorinthians 16:17
Nami nafurahi kwa sababu ya kuja kwao Stefana na Fortunato na Akaiko; maana hawa wamenikirimia kwa wingi yale niliyopungukiwa kwenu.
1 Wakorintho 16:18 1stCorinthians 16:18
Maana wameniburudisha roho yangu, na roho zenu pia; basi wajueni sana watu kama hao.
1 Wakorintho 16:19 1stCorinthians 16:19
Makanisa ya Asia wawasalimu. Akila na Priska wawasalimu sana katika Bwana, pamoja na kanisa lililoko ndani ya nyumba yao.
1 Wakorintho 16:20 1stCorinthians 16:20
Ndugu wote wawasalimu. Salimianeni kwa busu takatifu.
1 Wakorintho 16:21 1stCorinthians 16:21
Hii ni salamu yangu Paulo kwa mkono wangu mwenyewe.
1 Wakorintho 16:22 1stCorinthians 16:22
Mtu awaye yote asiyempenda Bwana, na awe amelaaniwa. Maran atha.
1 Wakorintho 16:23 1stCorinthians 16:23
Neema ya Bwana Yesu na iwe pamoja nanyi.
1 Wakorintho 16:24 1stCorinthians 16:24
Pendo langu na liwe pamoja nanyi nyote katika Kristo Yesu.