1 Wakorintho Mlango 11 1st Corinthians
1 Wakorintho 11:1 1stCorinthians 11:1
Mnifuate mimi kama mimi ninavyomfuata Kristo.
1 Wakorintho 11:2 1stCorinthians 11:2
Basi nawasifu, kwa sababu mmenikumbuka katika mambo yote, nanyi mmeyashika yale mapokeo vile vile kama nilivyowatolea.
1 Wakorintho 11:3 1stCorinthians 11:3
Lakini nataka mjue ya kuwa kichwa cha kila mwanamume ni Kristo, na kichwa cha mwanamke ni mwanamume, na kichwa cha Kristo ni Mungu.
1 Wakorintho 11:4 1stCorinthians 11:4
Kila mwanamume, asalipo, au anapohutubu, naye amefunikwa kichwa, yuaaibisha kichwa chake.
1 Wakorintho 11:5 1stCorinthians 11:5
Bali kila mwanamke asalipo, au anapohutubu, bila kufunika kichwa, yuaaibisha kichwa chake; kwa maana ni sawasawa na yule aliyenyolewa.
1 Wakorintho 11:6 1stCorinthians 11:6
Maana mwanamke asipofunikwa na akatwe nywele. Au ikiwa ni aibu mwanamke kukatwa nywele zake au kunyolewa, na afunikwe.
1 Wakorintho 11:7 1stCorinthians 11:7
Kwa maana kweli haimpasi mwanamume kufunikwa kichwa, kwa sababu yeye ni mfano na utukufu wa Mungu. Lakini mwanamke ni utukufu wa mwanamume.
1 Wakorintho 11:8 1stCorinthians 11:8
Maana mwanamume hakutoka katika mwanamke, bali mwanamke katika mwanamume.
1 Wakorintho 11:9 1stCorinthians 11:9
Wala mwanamume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, bali mwanamke kwa ajili ya mwanamume.
1 Wakorintho 11:10 1stCorinthians 11:10
Kwa hiyo imempasa mwanamke awe na dalili ya kumilikiwa kichwani, kwa ajili ya malaika.
1 Wakorintho 11:11 1stCorinthians 11:11
Walakini si mwanamke pasipo mwanamume, wala mwanamume pasipo mwanamke, katika Bwana.
1 Wakorintho 11:12 1stCorinthians 11:12
Maana kama mwanamke alitoka katika mwanamume, vile vile mwanamume naye huzaliwa na mwanamke; na vitu vyote asili yake hutoka kwa Mungu. Hukumuni ninyi wenyewe katika nafsi zenu.
1 Wakorintho 11:13 1stCorinthians 11:13
Je! Inapendeza mwanamke amwombe Mungu asipofunikwa kichwa?
1 Wakorintho 11:14 1stCorinthians 11:14
Je! Hayo maumbile yenyewe hayawafundishi ya kwamba mwanamume akiwa na nywele ndefu ni aibu kwake?
1 Wakorintho 11:15 1stCorinthians 11:15
Lakini mwanamke akiwa na nywele ndefu ni fahari kwake. Kwa sababu amepewa zile nywele ndefu ili ziwe badala ya mavazi.
1 Wakorintho 11:16 1stCorinthians 11:16
Lakini mtu ye yote akitaka kuleta fitina, sisi hatuna desturi kama hiyo, wala makanisa ya Mungu.
1 Wakorintho 11:17 1stCorinthians 11:17
Lakini katika kuagiza haya, siwasifu, ya kwamba mnakusanyika, si kwa faida bali kwa hasara.
1 Wakorintho 11:18 1stCorinthians 11:18
Kwa maana kwanza mkutanikapo kanisani nasikia kuna faraka kwenu; nami nusu nasadiki;
1 Wakorintho 11:19 1stCorinthians 11:19
kwa maana lazima kuwapo na uzushi kwenu, ili waliokubaliwa wawe dhahiri kwenu.
1 Wakorintho 11:20 1stCorinthians 11:20
Basi mkutanikapo pamoja haiwezekani kula chakula cha Bwana;
1 Wakorintho 11:21 1stCorinthians 11:21
kwa maana kila mmoja hutangulia kutwaa chakula chake katika kule kula; hata huyu ana njaa, na huyu amelewa.
1 Wakorintho 11:22 1stCorinthians 11:22
Je! Hamna nyumba za kulia na kunywea? Au mnalidharau kanisa la Mungu, na kuwatahayarisha hao wasio na kitu? Niwaambieni? Niwasifu? La! Siwasifu kwa ajili ya hayo.
1 Wakorintho 11:23 1stCorinthians 11:23
Kwa maana mimi nalipokea kwa Bwana niliyowapa nanyi, ya kuwa Bwana Yesu usiku ule aliotolewa alitwaa mkate,
1 Wakorintho 11:24 1stCorinthians 11:24
naye akiisha kushukuru akaumega, akasema, Huu ndio mwili wangu ulio kwa ajili yenu; fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.
1 Wakorintho 11:25 1stCorinthians 11:25
Na vivi hivi baada ya kula akakitwaa kikombe, akisema, Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu; fanyeni hivi kila mnywapo, kwa ukumbusho wangu.
1 Wakorintho 11:26 1stCorinthians 11:26
Maana kila mwulapo mkate huu na kukinywea kikombe hiki, mwaitangaza mauti ya Bwana hata ajapo.
1 Wakorintho 11:27 1stCorinthians 11:27
Basi kila aulaye mkate huo, au kukinywea kikombe hicho cha Bwana isivyostahili, atakuwa amejipatia hatia ya mwili na damu ya Bwana.
1 Wakorintho 11:28 1stCorinthians 11:28
Lakini mtu ajihoji mwenyewe, na hivyo aule mkate, na kukinywea kikombe.
1 Wakorintho 11:29 1stCorinthians 11:29
Maana alaye na kunywa, hula na kunywa hukumu ya nafsi yake, kwa kutokuupambanua ule mwili.
1 Wakorintho 11:30 1stCorinthians 11:30
Kwa sababu hiyo wako wengi kwenu walio hawawezi na dhaifu, na watu kadha wa kadha wamelala.
1 Wakorintho 11:31 1stCorinthians 11:31
Lakini kama tungejipambanua nafsi zetu, tusingehukumiwa.
1 Wakorintho 11:32 1stCorinthians 11:32
Ila tuhukumiwapo, twarudiwa na Bwana, isije ikatupasa adhabu pamoja na dunia.
1 Wakorintho 11:33 1stCorinthians 11:33
Kwa hiyo, ndugu zangu, mkutanikapo mpate kula, mngojaneni;
1 Wakorintho 11:34 1stCorinthians 11:34
mtu akiwa na njaa, na ale nyumbani kwake; msipate kukutanika kwa hukumu. Na hayo yaliyosalia nijapo nitayatengeneza.