1 Wakorintho Mlango 1 1st Corinthians

1 Wakorintho 1:1 1stCorinthians 1:1

Paulo, aliyeitwa kuwa mtume wa Yesu Kristo kwa mapenzi ya Mungu, na Sosthene ndugu yetu,

1 Wakorintho 1:2 1stCorinthians 1:2

kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, wale waliotakaswa katika Kristo Yesu, walioitwa wawe watakatifu, pamoja na wote wanaoliitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo kila mahali, Bwana wao na wetu.

1 Wakorintho 1:3 1stCorinthians 1:3

Neema na iwe kwenu na amani, zitokazo kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana Yesu Kristo.

1 Wakorintho 1:4 1stCorinthians 1:4

Namshukuru Mungu sikuzote kwa ajili yenu, kwa sababu ya neema ya Mungu mliyopewa katika Kristo Yesu;

1 Wakorintho 1:5 1stCorinthians 1:5

kwa kuwa katika kila jambo mlitajirika katika yeye, katika maneno yote, na maarifa yote;

1 Wakorintho 1:6 1stCorinthians 1:6

kama ushuhuda wa Kristo ulivyothibitika kwenu;

1 Wakorintho 1:7 1stCorinthians 1:7

hata hamkupungukiwa na karama yo yote, mkikutazamia sana kufunuliwa kwake Bwana wetu Yesu Kristo;

1 Wakorintho 1:8 1stCorinthians 1:8

ambaye atawathibitisha hata mwisho, ili msilaumiwe siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo.

1 Wakorintho 1:9 1stCorinthians 1:9

Mungu ni mwaminifu ambaye mliitwa na yeye mwingie katika ushirika wa Mwanawe, Yesu Kristo Bwana wetu.

1 Wakorintho 1:10 1stCorinthians 1:10

Basi ndugu, nawasihi, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba nyote mnene mamoja; wala pasiwe kwenu faraka, bali mhitimu katika nia moja na shauri moja.

1 Wakorintho 1:11 1stCorinthians 1:11

Kwa maana, ndugu zangu, nimearifiwa habari zenu na wale walio wa nyumbani mwa Kloe, ya kwamba iko fitina kwenu.

1 Wakorintho 1:12 1stCorinthians 1:12

Basi, maana yangu ni hii, ya kwamba kila mtu wa kwenu kusema, Mimi ni wa Paulo, na, Mimi ni wa Apolo, na, Mimi ni wa Kefa, na, Mimi ni wa Kristo.

1 Wakorintho 1:13 1stCorinthians 1:13

Je! Kristo amegawanyika? Je! Paulo alisulibiwa kwa ajili yenu? Au je! Mlibatizwa kwa jina la Paulo?

1 Wakorintho 1:14 1stCorinthians 1:14

Nashukuru, kwa sababu sikumbatiza mtu kwenu, ila Krispo na Gayo;

1 Wakorintho 1:15 1stCorinthians 1:15

mtu asije akasema kwamba mlibatizwa kwa jina langu.

1 Wakorintho 1:16 1stCorinthians 1:16

Tena naliwabatiza watu wa nyumbani mwa Stefana; zaidi ya hao, sijui kama nalimbatiza mtu ye yote mwingine.

1 Wakorintho 1:17 1stCorinthians 1:17

Maana Kristo hakunituma ili nibatize, bali niihubiri Habari Njema; wala si kwa hekima ya maneno, msalaba wa Kristo usije ukabatilika.

1 Wakorintho 1:18 1stCorinthians 1:18

Kwa sababu neno la msalaba kwao wanaopotea ni upuzi, bali kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu.

1 Wakorintho 1:19 1stCorinthians 1:19

Kwa kuwa imeandikwa, Nitaiharibu hekima yao wenye hekima, Na akili zao wenye akili nitazikataa.

1 Wakorintho 1:20 1stCorinthians 1:20

Yu wapi mwenye hekima? Yu wapi mwandishi? Yu wapi mlete hoja wa zamani hizi? Je! Mungu hakuifanya hekima ya dunia kuwa ni upumbavu?

1 Wakorintho 1:21 1stCorinthians 1:21

Kwa maana katika hekima ya Mungu, dunia isipopata kumjua Mungu kwa hekima yake, Mungu alipenda kuwaokoa waaminio kwa upuzi wa lile neno linalohubiriwa.

1 Wakorintho 1:22 1stCorinthians 1:22

Kwa sababu Wayahudi wanataka ishara, na Wayunani wanatafuta hekima;

1 Wakorintho 1:23 1stCorinthians 1:23

bali sisi tunamhubiri Kristo, aliyesulibiwa; kwa Wayahudi ni kikwazo, na kwa Wayunani ni upuzi;

1 Wakorintho 1:24 1stCorinthians 1:24

bali kwao waitwao, Wayahudi kwa Wayunani, ni Kristo, nguvu ya Mungu, na hekima ya Mungu.

1 Wakorintho 1:25 1stCorinthians 1:25

Kwa sababu upumbavu wa Mungu una hekima zaidi ya wanadamu, na udhaifu wa Mungu una nguvu zaidi ya wanadamu.

1 Wakorintho 1:26 1stCorinthians 1:26

Maana, ndugu zangu, angalieni mwito wenu, ya kwamba si wengi wenye hekima ya mwilini, si wengi wenye nguvu, si wengi wenye cheo walioitwa;

1 Wakorintho 1:27 1stCorinthians 1:27

bali Mungu aliyachagua mambo mapumbavu ya dunia awaaibishe wenye hekima; tena Mungu alivichagua vitu dhaifu vya dunia ili aviaibishe vyenye nguvu;

1 Wakorintho 1:28 1stCorinthians 1:28

tena Mungu alivichagua vitu vinyonge vya dunia na vilivyodharauliwa, naam, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko;

1 Wakorintho 1:29 1stCorinthians 1:29

mwenye mwili awaye yote asije akajisifu mbele za Mungu.

1 Wakorintho 1:30 1stCorinthians 1:30

Bali kwa yeye ninyi mmepata kuwa katika Kristo Yesu, aliyefanywa kwetu hekima itokayo kwa Mungu, na haki, na utakatifu, na ukombozi;

1 Wakorintho 1:31 1stCorinthians 1:31

kusudi, kama ilivyoandikwa, Yeye aonaye fahari na aone fahari juu ya Bwana.