1 Wakorintho Mlango 1 1st Corinthians
1 Wakorintho 1:1 1stCorinthians 1:1
Paulo, aliyeitwa kuwa mtume wa Yesu Kristo kwa mapenzi ya Mungu, na Sosthene ndugu yetu,
1 Wakorintho 1:2 1stCorinthians 1:2
kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, wale waliotakaswa katika Kristo Yesu, walioitwa wawe watakatifu, pamoja na wote wanaoliitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo kila mahali, Bwana wao na wetu.
1 Wakorintho 1:3 1stCorinthians 1:3
Neema na iwe kwenu na amani, zitokazo kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana Yesu Kristo.
1 Wakorintho 1:4 1stCorinthians 1:4
Namshukuru Mungu sikuzote kwa ajili yenu, kwa sababu ya neema ya Mungu mliyopewa katika Kristo Yesu;
1 Wakorintho 1:5 1stCorinthians 1:5
kwa kuwa katika kila jambo mlitajirika katika yeye, katika maneno yote, na maarifa yote;
1 Wakorintho 1:6 1stCorinthians 1:6
kama ushuhuda wa Kristo ulivyothibitika kwenu;
1 Wakorintho 1:7 1stCorinthians 1:7
hata hamkupungukiwa na karama yo yote, mkikutazamia sana kufunuliwa kwake Bwana wetu Yesu Kristo;
1 Wakorintho 1:8 1stCorinthians 1:8
ambaye atawathibitisha hata mwisho, ili msilaumiwe siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo.
1 Wakorintho 1:9 1stCorinthians 1:9
Mungu ni mwaminifu ambaye mliitwa na yeye mwingie katika ushirika wa Mwanawe, Yesu Kristo Bwana wetu.
1 Wakorintho 1:10 1stCorinthians 1:10
Basi ndugu, nawasihi, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba nyote mnene mamoja; wala pasiwe kwenu faraka, bali mhitimu katika nia moja na shauri moja.
1 Wakorintho 1:11 1stCorinthians 1:11
Kwa maana, ndugu zangu, nimearifiwa habari zenu na wale walio wa nyumbani mwa Kloe, ya kwamba iko fitina kwenu.
1 Wakorintho 1:12 1stCorinthians 1:12
Basi, maana yangu ni hii, ya kwamba kila mtu wa kwenu kusema, Mimi ni wa Paulo, na, Mimi ni wa Apolo, na, Mimi ni wa Kefa, na, Mimi ni wa Kristo.
1 Wakorintho 1:13 1stCorinthians 1:13
Je! Kristo amegawanyika? Je! Paulo alisulibiwa kwa ajili yenu? Au je! Mlibatizwa kwa jina la Paulo?
1 Wakorintho 1:14 1stCorinthians 1:14
Nashukuru, kwa sababu sikumbatiza mtu kwenu, ila Krispo na Gayo;
1 Wakorintho 1:15 1stCorinthians 1:15
mtu asije akasema kwamba mlibatizwa kwa jina langu.
1 Wakorintho 1:16 1stCorinthians 1:16
Tena naliwabatiza watu wa nyumbani mwa Stefana; zaidi ya hao, sijui kama nalimbatiza mtu ye yote mwingine.
1 Wakorintho 1:17 1stCorinthians 1:17
Maana Kristo hakunituma ili nibatize, bali niihubiri Habari Njema; wala si kwa hekima ya maneno, msalaba wa Kristo usije ukabatilika.
1 Wakorintho 1:18 1stCorinthians 1:18
Kwa sababu neno la msalaba kwao wanaopotea ni upuzi, bali kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu.
1 Wakorintho 1:19 1stCorinthians 1:19
Kwa kuwa imeandikwa, Nitaiharibu hekima yao wenye hekima, Na akili zao wenye akili nitazikataa.
1 Wakorintho 1:20 1stCorinthians 1:20
Yu wapi mwenye hekima? Yu wapi mwandishi? Yu wapi mlete hoja wa zamani hizi? Je! Mungu hakuifanya hekima ya dunia kuwa ni upumbavu?
1 Wakorintho 1:21 1stCorinthians 1:21
Kwa maana katika hekima ya Mungu, dunia isipopata kumjua Mungu kwa hekima yake, Mungu alipenda kuwaokoa waaminio kwa upuzi wa lile neno linalohubiriwa.
1 Wakorintho 1:22 1stCorinthians 1:22
Kwa sababu Wayahudi wanataka ishara, na Wayunani wanatafuta hekima;
1 Wakorintho 1:23 1stCorinthians 1:23
bali sisi tunamhubiri Kristo, aliyesulibiwa; kwa Wayahudi ni kikwazo, na kwa Wayunani ni upuzi;
1 Wakorintho 1:24 1stCorinthians 1:24
bali kwao waitwao, Wayahudi kwa Wayunani, ni Kristo, nguvu ya Mungu, na hekima ya Mungu.
1 Wakorintho 1:25 1stCorinthians 1:25
Kwa sababu upumbavu wa Mungu una hekima zaidi ya wanadamu, na udhaifu wa Mungu una nguvu zaidi ya wanadamu.
1 Wakorintho 1:26 1stCorinthians 1:26
Maana, ndugu zangu, angalieni mwito wenu, ya kwamba si wengi wenye hekima ya mwilini, si wengi wenye nguvu, si wengi wenye cheo walioitwa;
1 Wakorintho 1:27 1stCorinthians 1:27
bali Mungu aliyachagua mambo mapumbavu ya dunia awaaibishe wenye hekima; tena Mungu alivichagua vitu dhaifu vya dunia ili aviaibishe vyenye nguvu;
1 Wakorintho 1:28 1stCorinthians 1:28
tena Mungu alivichagua vitu vinyonge vya dunia na vilivyodharauliwa, naam, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko;
1 Wakorintho 1:29 1stCorinthians 1:29
mwenye mwili awaye yote asije akajisifu mbele za Mungu.
1 Wakorintho 1:30 1stCorinthians 1:30
Bali kwa yeye ninyi mmepata kuwa katika Kristo Yesu, aliyefanywa kwetu hekima itokayo kwa Mungu, na haki, na utakatifu, na ukombozi;
1 Wakorintho 1:31 1stCorinthians 1:31
kusudi, kama ilivyoandikwa, Yeye aonaye fahari na aone fahari juu ya Bwana.