1 Wakorintho Mlango 9 1st Corinthians
1 Wakorintho 9:1 1stCorinthians 9:1
Je! Mimi si huru? Mimi si mtume? Mimi sikumwona Yesu Bwana wetu? Ninyi si kazi yangu katika Bwana?
1 Wakorintho 9:2 1stCorinthians 9:2
Kwa maana ikiwa mimi si mtume kwa wengine, lakini ni mtume kwenu ninyi; kwa maana ninyi ndinyi muhuri ya utume wangu katika Bwana.
1 Wakorintho 9:3 1stCorinthians 9:3
Hilo ndilo jawabu langu kwa wale wanaoniuliza.
1 Wakorintho 9:4 1stCorinthians 9:4
Je! Hatuna uwezo wa kula na kunywa?
1 Wakorintho 9:5 1stCorinthians 9:5
Hatuna uwezo kuchukua pamoja nasi mke aliye ndugu, kama wao mitume wengine, na ndugu wa Bwana, na Kefa?
1 Wakorintho 9:6 1stCorinthians 9:6
Au je! Ni mimi peke yangu na Barnaba tusio na uwezo wa kutokufanya kazi?
1 Wakorintho 9:7 1stCorinthians 9:7
Ni askari gani aendaye vitani wakati wo wote kwa gharama zake mwenyewe? Ni nani apandaye mizabibu asiyekula katika matunda yake? Au ni nani achungaye kundi, asiyekunywa katika maziwa ya kundi?
1 Wakorintho 9:8 1stCorinthians 9:8
Je! Ninanena hayo kwa kibinadamu? Au torati nayo haisemi yayo hayo?
1 Wakorintho 9:9 1stCorinthians 9:9
Kwa maana katika torati ya Musa imeandikwa, Usimfunge kinywa ng'ombe apurapo nafaka. Je! Hapo Mungu aangalia mambo ya ng'ombe?
1 Wakorintho 9:10 1stCorinthians 9:10
Au yamkini anena hayo kwa ajili yetu? Naam, yaliandikwa kwa ajili yetu; kwa kuwa alimaye nafaka ni haki yake kulima kwa matumaini, naye apuraye nafaka ni haki yake kutumaini kupata sehemu yake.
1 Wakorintho 9:11 1stCorinthians 9:11
Ikiwa sisi tuliwapandia ninyi vitu vya rohoni, je! Ni neno kubwa tukivuna vitu vyenu vya mwilini?
1 Wakorintho 9:12 1stCorinthians 9:12
Ikiwa wengine wanashiriki uwezo huu juu yenu, sisi si zaidi? Lakini hatukuutumia uwezo huo; bali twayavumilia mambo yote tusije tukaizuia Habari Njema ya Kristo.
1 Wakorintho 9:13 1stCorinthians 9:13
Hamjui ya kuwa wale wazifanyao kazi za hekaluni hula katika vitu vya hekalu, na wale waihudumiao madhabahu huwa na fungu lao katika vitu vya madhabahu?
1 Wakorintho 9:14 1stCorinthians 9:14
Na Bwana vivyo hivyo ameamuru kwamba wale waihubirio Injili wapate riziki kwa hiyo Injili.
1 Wakorintho 9:15 1stCorinthians 9:15
Lakini mimi sikutumia mambo hayo hata moja. Wala siyaandiki hayo ili iwe hivyo kwangu mimi; maana ni heri nife kuliko mtu awaye yote abatilishe huku kujisifu kwangu.
1 Wakorintho 9:16 1stCorinthians 9:16
Maana, ijapokuwa naihubiri Injili, sina la kujisifia; maana nimewekewa sharti; tena ole wangu nisipoihubiri Injili!
1 Wakorintho 9:17 1stCorinthians 9:17
Maana nikiitenda kazi hii kwa hiari yangu nina thawabu; ila ikiwa si kwa hiari yangu, nimeaminiwa uwakili.
1 Wakorintho 9:18 1stCorinthians 9:18
Basi thawabu yangu ni nini? Ni hii, ya kuwa nihubiripo, nitaitoa Injili bila gharama, bila kutumia kwa utimilifu uwezo wangu nilio nao katika Injili.
1 Wakorintho 9:19 1stCorinthians 9:19
Maana, ingawa nimekuwa huru kwa watu wote, nalijifanya mtumwa wa wote, ili nipate watu wengi zaidi.
1 Wakorintho 9:20 1stCorinthians 9:20
Nalikuwa kama Myahudi kwa Wayahudi, ili niwapate Wayahudi; kwa wale walio chini ya sheria, nalikuwa kama chini ya sheria, (ingawa mimi mwenyewe si chini ya sheria), ili niwapate walio chini ya sheria.
1 Wakorintho 9:21 1stCorinthians 9:21
Kwa wale wasio na sheria nalikuwa kama sina sheria, (si kwamba sina sheria mbele za Mungu, bali mwenye sheria mbele za Kristo), ili niwapate hao wasio na sheria.
1 Wakorintho 9:22 1stCorinthians 9:22
Kwa wanyonge nalikuwa mnyonge, ili niwapate wanyonge. Nimekuwa hali zote kwa watu wote, ili kwa njia zote nipate kuwaokoa watu.
1 Wakorintho 9:23 1stCorinthians 9:23
Nami nafanya mambo yote kwa ajili ya Injili ili kuishiriki pamoja na wengine.
1 Wakorintho 9:24 1stCorinthians 9:24
Je! Hamjui, ya kuwa wale washindanao kwa kupiga mbio, hupiga mbio wote, lakini apokeaye tuzo ni mmoja? Pigeni mbio namna hiyo, ili mpate.
1 Wakorintho 9:25 1stCorinthians 9:25
Na kila ashindanaye katika michezo hujizuia katika yote; basi hao hufanya hivyo kusudi wapokee taji iharibikayo; bali sisi tupokee taji isiyoharibika.
1 Wakorintho 9:26 1stCorinthians 9:26
Hata mimi napiga mbio vivyo hivyo, si kama asitaye; napigana ngumi vivyo hivyo, si kama apigaye hewa;
1 Wakorintho 9:27 1stCorinthians 9:27
bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa.