1 Wakorintho Mlango 5 1st Corinthians
1 Wakorintho 5:1 1stCorinthians 5:1
Yakini habari imeenea ya kuwa kwenu kuna zinaa, na zinaa ya namna isiyokuwako hata katika Mataifa, kwamba mtu awe na mke wa babaye.
1 Wakorintho 5:2 1stCorinthians 5:2
Nanyi mwajivuna, wala hamkusikitika, ili kwamba aondolewe miongoni mwenu huyo aliyetenda jambo hilo.
1 Wakorintho 5:3 1stCorinthians 5:3
Kwa maana kweli, nisipokuwapo kwa mwili, lakini nikiwapo kwa roho, mimi mwenyewe nimekwisha kumhukumu yeye aliyetenda jambo hilo, kana kwamba nikiwapo.
1 Wakorintho 5:4 1stCorinthians 5:4
Katika jina la Bwana wetu Yesu, ninyi mkiwa mmekusanyika pamoja na roho yangu, pamoja na uweza wa Bwana wetu Yesu;
1 Wakorintho 5:5 1stCorinthians 5:5
kumtolea Shetani mtu huyo, ili mwili uadhibiwe, ili na roho iokolewe katika siku ya Bwana Yesu.
1 Wakorintho 5:6 1stCorinthians 5:6
Kujisifu kwenu si kuzuri. Hamjui kwamba chachu kidogo hulichachusha donge zima?
1 Wakorintho 5:7 1stCorinthians 5:7
Basi, jisafisheni, mkatoe ile chachu ya kale, mpate kuwa donge jipya, kama vile mlivyo hamkutiwa chachu. Kwa maana Pasaka wetu amekwisha kutolewa kuwa sadaka, yaani, Kristo;
1 Wakorintho 5:8 1stCorinthians 5:8
basi na tuifanye karamu, si kwa chachu ya kale, wala kwa chachu ya uovu na ubaya, bali kwa yasiyochachika, ndio weupe wa moyo na kweli.
1 Wakorintho 5:9 1stCorinthians 5:9
Naliwaandikia katika waraka wangu, kwamba msichangamane na wazinzi.
1 Wakorintho 5:10 1stCorinthians 5:10
Sisemi msichangamane kabisa na wazinzi wa dunia hii, au na wenye kutamani, au na wanyang'anyi, au na wenye kuabudu sanamu; maana hapo ingewalazimu kutoka katika dunia.
1 Wakorintho 5:11 1stCorinthians 5:11
Lakini, mambo yalivyo, naliwaandikia kwamba msichangamane na mtu aitwaye ndugu, akiwa ni mzinzi au mwenye kutamani au mwenye kuabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang'anyi; mtu wa namna hii msikubali hata kula naye.
1 Wakorintho 5:12 1stCorinthians 5:12
Maana yanihusu nini kuwahukumu wale walio nje? Ninyi hamwahukumu hao walio ndani?
1 Wakorintho 5:13 1stCorinthians 5:13
Lakini hao walio nje Mungu atawahukumu. Ninyi mwondoeni yule mbaya miongoni mwenu.