Kumbukumbu la Torati Mlango 8 Deuteronomy

Kumbukumbu la Torati 8:1 Deuteronomy 8:1

Amri hii ninayokuamuru leo mtaishika kuitenda, mpate kuishi na kuongezeka, na kuingia katika nchi ile ambayo Bwana aliwaapia baba zenu; nanyi mtaimiliki.

Kumbukumbu la Torati 8:2 Deuteronomy 8:2

Nawe utaikumbuka njia ile yote Bwana, Mungu wako aliyokuongoza miaka hii arobaini katika jangwa, ili akutweze, kukujaribu kuyajua yaliyo moyoni mwako, kwamba utashika amri zake, au sivyo.

Kumbukumbu la Torati 8:3 Deuteronomy 8:3

Akakutweza, akakuacha uone njaa, akakulisha kwa mana, usiyoijua wewe wala baba zako hawakuijua; apate kukujulisha ya kuwa mwanadamu haishi kwa mkate tu, bali huishi kwa kila litokalo katika kinywa cha Bwana.

Kumbukumbu la Torati 8:4 Deuteronomy 8:4

Mavazi yako hayakuchakaa, wala mguu wako haukuvimba, miaka hiyo arobaini.

Kumbukumbu la Torati 8:5 Deuteronomy 8:5

Nawe fikiri moyoni mwako, ya kuwa kama vile baba amrudivyo mwanawe, ndivyo Bwana, Mungu wako, akurudivyo.

Kumbukumbu la Torati 8:6 Deuteronomy 8:6

Nawe uzishike amri za Bwana, Mungu wako, upate kwenda katika njia zake, na kumcha.

Kumbukumbu la Torati 8:7 Deuteronomy 8:7

Kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yuakuingiza katika nchi nzuri, nchi yenye vijito vya maji, na chemchemi, na visima, vibubujikavyo katika mabonde na milima;

Kumbukumbu la Torati 8:8 Deuteronomy 8:8

nchi ya ngano na shayiri, na mizabibu, na mitini, na mikomamanga; nchi ya mizeituni yenye mafuta, na asali;

Kumbukumbu la Torati 8:9 Deuteronomy 8:9

nchi utakayokula mikate humo, pasina shida, hutapungukiwa na kitu ndani yake; nchi ambayo mawe yake ni chuma, na milima yake yafukuka shaba.

Kumbukumbu la Torati 8:10 Deuteronomy 8:10

Nawe utakula ushibe, utamshukuru Bwana, Mungu wako, kwa nchi nzuri aliyokupa.

Kumbukumbu la Torati 8:11 Deuteronomy 8:11

Jihadhari, usije ukamsahau Bwana, Mungu wako, kwa kutozishika amri zake, na hukumu zake, na sheria zake, ninazokuamuru leo.

Kumbukumbu la Torati 8:12 Deuteronomy 8:12

Angalia, utakapokuwa umekula na kushiba, na kujenga nyumba nzuri na kukaa ndani yake;

Kumbukumbu la Torati 8:13 Deuteronomy 8:13

na makundi yako ya ng'ombe na kondoo yatakapoongezeka, na fedha yako na dhahabu yako itakapoongezeka, na kila kitu ulicho nacho kitakapoongezeka;

Kumbukumbu la Torati 8:14 Deuteronomy 8:14

basi hapo moyo wako usiinuke, ukamsahau Bwana, Mungu wako, aliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa;

Kumbukumbu la Torati 8:15 Deuteronomy 8:15

aliyekuongoza katika jangwa lile kubwa lenye kitisho, lenye nyoka za moto na nge, nchi ya kiu isiyokuwa na maji; aliyekutolea maji katika mwamba mgumu,

Kumbukumbu la Torati 8:16 Deuteronomy 8:16

aliyekulisha jangwani kwa mana, wasiyoijua baba zako; apate kukutweza, apate kukujaribu, ili kukutendea mema mwisho wako.

Kumbukumbu la Torati 8:17 Deuteronomy 8:17

Hapo usiseme moyoni mwako, Nguvu zangu na uwezo wa mkono wangu ndio ulionipatia utajiri huo.

Kumbukumbu la Torati 8:18 Deuteronomy 8:18

Bali utamkumbuka Bwana, Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri; ili alifanye imara agano lake alilowapa baba zako, kama hivi leo.

Kumbukumbu la Torati 8:19 Deuteronomy 8:19

Lakini itakuwa, kama ukimsahau Bwana, Mungu wako, na kuiandama miungu mingine, na kuitumikia na kuiabudu, nawashuhudia leo ya kuwa mtaangamia bila shaka.

Kumbukumbu la Torati 8:20 Deuteronomy 8:20

Kama vile mataifa yale ambayo Bwana anawaangamiza mbele yenu, ndivyo mtakavyoangamia; kwa sababu hamkutaka kuisikiliza sauti ya Bwana, Mungu wenu.