Kumbukumbu la Torati Mlango 6 Deuteronomy
Kumbukumbu la Torati 6:1 Deuteronomy 6:1
Na hii ndiyo sheria, na amri, na hukumu, alizoziamuru Bwana, Mungu wenu, mfundishwe, mpate kuzitenda katika nchi ile mnayoivukia kuimiliki;
Kumbukumbu la Torati 6:2 Deuteronomy 6:2
upate kumcha Bwana, Mungu wako, kushika amri zake zote, na sheria zake, ninazokuamuru, wewe na mwanao, na mwana wa mwanao, siku zote za maisha yako; tena siku zako ziongezwe.
Kumbukumbu la Torati 6:3 Deuteronomy 6:3
Sikiza basi, Ee Israeli, ukaangalie kuzitenda; upate kufanikiwa, mpate kuongezeka sana, kama Bwana, Mungu wa baba zako, alivyokuahidi, katika nchi ijaayo maziwa na asali.
Kumbukumbu la Torati 6:4 Deuteronomy 6:4
Sikiza, Ee Israeli; Bwana, Mungu wetu, Bwana ndiye mmoja.
Kumbukumbu la Torati 6:5 Deuteronomy 6:5
Nawe mpende Bwana, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote.
Kumbukumbu la Torati 6:6 Deuteronomy 6:6
Na maneno haya ninayokuamuru leo, yatakuwa katika moyo wako;
Kumbukumbu la Torati 6:7 Deuteronomy 6:7
nawe uwafundishe watoto wako kwa bidii, na kuyanena uketipo katika nyumba yako, na utembeapo njiani, na ulalapo, na uondokapo.
Kumbukumbu la Torati 6:8 Deuteronomy 6:8
Yafunge yawe dalili juu ya mkono wako, nayo yatakuwa kama utepe katikati ya macho yako.
Kumbukumbu la Torati 6:9 Deuteronomy 6:9
Tena yaandike juu ya miimo ya nyumba yako, na juu ya malango yako.
Kumbukumbu la Torati 6:10 Deuteronomy 6:10
Tena itakuwa atakapokwisha Bwana, Mungu wako, kukuleta katika nchi aliyowaapia babu zako, Ibrahimu na Isaka na Yakobo, ya kuwa atakupa; miji mikubwa mizuri usiyoijenga wewe,
Kumbukumbu la Torati 6:11 Deuteronomy 6:11
na nyumba zimejaa vitu vyema vyote usizojaza wewe, na visima vimefukuliwa usivyofukua wewe, mashamba ya mizabibu na mizeituni usiyoipanda wewe, nawe utakula na kushiba;
Kumbukumbu la Torati 6:12 Deuteronomy 6:12
ndipo ujitunze, usije ukamsahau Bwana aliyekutoa nchi ya Misri, nyumba ya utumwa.
Kumbukumbu la Torati 6:13 Deuteronomy 6:13
Mche Bwana, Mungu wako; ndiye utakayemtumikia, na kuapa kwa jina lake.
Kumbukumbu la Torati 6:14 Deuteronomy 6:14
Msifuate miungu mingine katika miungu ya mataifa wawazungukao;
Kumbukumbu la Torati 6:15 Deuteronomy 6:15
kwani Bwana, Mungu wako, aliye katikati yako ni Mungu mwenye wivu; isije ikawaka juu yako hasira ya Bwana, Mungu wako, akakuangamiza kutoka juu ya uso wa nchi.
Kumbukumbu la Torati 6:16 Deuteronomy 6:16
Msimjaribu Bwana, Mungu wenu, kama mlivyomjaribu huko Masa.
Kumbukumbu la Torati 6:17 Deuteronomy 6:17
Zishikeni kwa bidii sheria za Bwana, Mungu wenu, na mashuhudizo yake, na amri zake alizokuagiza.
Kumbukumbu la Torati 6:18 Deuteronomy 6:18
Nawe fanya yaliyo sawa, na mema, machoni pa Bwana; ili mpate kufanikiwa, nawe upate kuingia na kuimiliki nchi nzuri Bwana aliyowaapia baba zako,
Kumbukumbu la Torati 6:19 Deuteronomy 6:19
ya kuwa atawasukumia nje adui zako wote mbele yako, kama alivyosema Bwana.
Kumbukumbu la Torati 6:20 Deuteronomy 6:20
Na zamani zijazo atakapokuuliza mwanao, akikuambia, N'nini mashuhudizo, na amri, na hukumu, alizowaagiza Bwana, Mungu wetu?
Kumbukumbu la Torati 6:21 Deuteronomy 6:21
Ndipo umwambie mwanao, Tulikuwa watumwa wa Farao huko Misri; Bwana, akatutoa kutoka Misri kwa mkono wa nguvu;
Kumbukumbu la Torati 6:22 Deuteronomy 6:22
Bwana akaonya ishara na maajabu, makubwa, mazito, juu ya Misri, na juu ya Farao, na juu ya nyumba yake yote, mbele ya macho yetu;
Kumbukumbu la Torati 6:23 Deuteronomy 6:23
akatutoa huko ili kututia huku, apate kutupa nchi aliyowaapia baba zetu.
Kumbukumbu la Torati 6:24 Deuteronomy 6:24
Bwana akatuamuru kuzifanya amri hizi zote, tumche Bwana, Mungu wetu, tuone mema sikuzote ili atuhifadhi hai kama hivi leo.
Kumbukumbu la Torati 6:25 Deuteronomy 6:25
Tena itakuwa haki kwetu, tukitunza kufanya maagizo haya yote mbele ya Bwana, Mungu wetu, kama alivyotuagiza.