Kumbukumbu la Torati Mlango 33 Deuteronomy

Kumbukumbu la Torati 33:1 Deuteronomy 33:1

Hii ndiyo baraka ya Musa, huyo mtu wa Mungu, aliyowabarikia wana wa Israeli kabla ya kufa kwake.

Kumbukumbu la Torati 33:2 Deuteronomy 33:2

Akasema,Bwana alitoka Sinai,Akawaondokea kutoka Seiri;Aliangaza katika kilima cha Parani,Akaja Meribath-Kadeshi.Upande wake wa kuume Palikuwa na sheria ya moto-moto kwao.

Kumbukumbu la Torati 33:3 Deuteronomy 33:3

Hakika awapenda hayo makabila ya watu; Watakatifu wake wote wamo mkononi mwako; Nao waliketi miguuni pako; Watapokea kila mmoja katika maneno yako.

Kumbukumbu la Torati 33:4 Deuteronomy 33:4

Musa alituagiza torati, Ni urithi kwa mkutano wa Yakobo.

Kumbukumbu la Torati 33:5 Deuteronomy 33:5

Akawa mfalme katika Yeshuruni, Walipokutanika wakuu wa watu, Makabila yote ya Israeli pamoja.

Kumbukumbu la Torati 33:6 Deuteronomy 33:6

Reubeni na aishi, asife; Lakini watu wake na wawe wachache.

Kumbukumbu la Torati 33:7 Deuteronomy 33:7

Na baraka ya Yuda ni hii; akasema, Isikize, Ee Bwana, sauti ya Yuda, Umlete ndani kwa watu wake; Alijitetea kwa mikono yake; Nawe utakuwa msaada juu ya adui zake.

Kumbukumbu la Torati 33:8 Deuteronomy 33:8

Akamnena Lawi, Thumimu yako na Urimu yako vina mtakatifu wako, Uliyemjaribu huko Masa; Ukateta naye kwenye maji ya Meriba.

Kumbukumbu la Torati 33:9 Deuteronomy 33:9

Aliyemtaja baba yake na mama yake, Mimi sikumwona; Wala nduguze hakuwakubali; Wala hakuwajua watoto wake mwenyewe; Maana wameliangalia neno lako, Wamelishika agano lako.

Kumbukumbu la Torati 33:10 Deuteronomy 33:10

Watamfundisha Yakobo hukumu zako, Na Israeli torati yako, Wataweka uvumba mbele zako, Na sadaka nzima za kuteketezwa madhabahuni mwako.

Kumbukumbu la Torati 33:11 Deuteronomy 33:11

Ee Bwana, ubariki mali zake, Utakabali kazi ya mikono yake; Uwapige viuno vyao waondokao juu yake, Na wenye kumchukia, wasiinuke tena.

Kumbukumbu la Torati 33:12 Deuteronomy 33:12

Akamnena Benyamini, Mpenzi wa Bwana atakaa salama kwake; Yuamfunika mchana kutwa, Naye hukaa kati ya mabega yake.

Kumbukumbu la Torati 33:13 Deuteronomy 33:13

Na Yusufu akamnena, Nchi yake na ibarikiwe na Bwana; Kwa vitu vya thamani vya mbinguni, kwa huo umande, Na kwa kilindi kilalacho chini,

Kumbukumbu la Torati 33:14 Deuteronomy 33:14

Na kwa vitu vilivyo bora vya matunda ya jua, Na kwa vitu vilivyo bora vya maongeo ya miezi,

Kumbukumbu la Torati 33:15 Deuteronomy 33:15

Na kwa vitu viteule vya milima ya kale, Na kwa vitu vilivyo bora vya vilima vya milele,

Kumbukumbu la Torati 33:16 Deuteronomy 33:16

Na kwa vitu vilivyo bora vya nchi, na kujaa kwake, Na uradhi wake aliyekaa ndani ya kile kijiti; Na ije baraka juu ya kichwa chake Yusufu, Juu ya utosi wa kichwa chake aliyetengwa na nduguze.

Kumbukumbu la Torati 33:17 Deuteronomy 33:17

Mzaliwa wa kwanza wa ng'ombe wake mume, enzi ni yake; Na pembe zake ni pembe za nyati; Kwa hizo atayasukuma mataifa yote, hata ncha za nchi; Nao ni makumi ya maelfu ya Efraimu, Nao ni maelfu ya Manase.

Kumbukumbu la Torati 33:18 Deuteronomy 33:18

Na Zabuloni akamnena, Furahi Zabuloni, katika kutoka kwako;

Kumbukumbu la Torati 33:19 Deuteronomy 33:19

Watayaita mataifa waje mlimani; Wakasongeze huko sadaka za haki; Kwa kuwa watanyonya wingi wa bahari, Na akiba zilizofichamana za mchangani.

Kumbukumbu la Torati 33:20 Deuteronomy 33:20

Na Gadi akamnena, Na abarikiwe amwongezaye Gadi; Yeye hukaa kama simba mke, Hurarua mkono, naam, na utosi wa kichwa.

Kumbukumbu la Torati 33:21 Deuteronomy 33:21

Akajichagulia sehemu ya kwanza, Kwani ndiko lilikowekwa fungu la mtoa-sheria; Akaja pamoja na wakuu wa watu, Akaitekeleza haki ya Bwana, Na hukumu zake kwa Israeli.

Kumbukumbu la Torati 33:22 Deuteronomy 33:22

Na Dani akamnena, Dani ni mwana-simba, Arukaye kutoka Bashani.

Kumbukumbu la Torati 33:23 Deuteronomy 33:23

Na Naftali akamnena, Ee Naftali, uliyeshiba fadhili, Uliyejawa na baraka ya Bwana; Umiliki magharibi na kusini.

Kumbukumbu la Torati 33:24 Deuteronomy 33:24

Na Asheri akamnena, Na abarikiwe Asheri kwa watoto; Na akubaliwe katika nduguze, Na achovye mguu wake katika mafuta.

Kumbukumbu la Torati 33:25 Deuteronomy 33:25

Makomeo yako yatakuwa ya chuma na shaba; Na kadiri ya siku zako ndivyo zitakavyokuwa nguvu zako.

Kumbukumbu la Torati 33:26 Deuteronomy 33:26

Hapana aliyefanana na Mungu, Ee Yeshuruni, Ajaye amepanda juu ya mbingu ili akusaidie. Na juu ya mawingu katika utukufu wake.

Kumbukumbu la Torati 33:27 Deuteronomy 33:27

Mungu wa milele ndiye makazi yako, Na mikono ya milele i chini yako. Na mbele yako amemsukumia mbali adui; Akasema, Angamiza.

Kumbukumbu la Torati 33:28 Deuteronomy 33:28

Na Israeli anakaa salama, Chemchemi ya Yakobo peke yake, Katika nchi ya ngano na divai; Naam, mbingu zake zadondoza umande.

Kumbukumbu la Torati 33:29 Deuteronomy 33:29

U heri, Israeli. Ni nani aliye kama wewe, taifa lililookolewa na Bwana! Ndiye ngao ya msaada wako, Na upanga wa utukufu wako; Na adui zako watajitiisha chini yako, Nawe utapakanyaga mahali pao pa juu.