Kumbukumbu la Torati Mlango 11 Deuteronomy

Kumbukumbu la Torati 11:1 Deuteronomy 11:1

Kwa ajili hii mpende Bwana, Mungu wako, na kushika sikuzote mausia yake, na amri zake, na hukumu zake, na maagizo yake.

Kumbukumbu la Torati 11:2 Deuteronomy 11:2

Nanyi leo jueni; kwa kuwa sisemi sasa na vijana vyenu, ambao hawakujua, wala hawakuona adhabu ya Bwana, Mungu wenu, ukuu wake, na mkono wake wa nguvu, na mkono wake ulionyoka,

Kumbukumbu la Torati 11:3 Deuteronomy 11:3

na ishara zake, na kazi zake alizomfanya Farao mfalme wa Misri, na nchi yake yote, katikati ya Misri;

Kumbukumbu la Torati 11:4 Deuteronomy 11:4

na alivyolifanya jeshi la Misri, farasi zao, na magari yao; na alivyowafunikiza maji ya Bahari ya Shamu walipokuwa wakiwaandamia, na alivyowaangamiza Bwana hata hivi leo;

Kumbukumbu la Torati 11:5 Deuteronomy 11:5

na mambo aliyowafanyia ninyi barani, hata mkaja mahali hapa;

Kumbukumbu la Torati 11:6 Deuteronomy 11:6

na alivyowafanya Dathani, na Abiramu, wana wa Eliabu mwana wa Reubeni; nchi ilivyofunua kinywa chake, ikawameza, na walio nyumbani mwao, na mahema yao, na kila kitu kilichokuwa hai kikiwafuata, katikati ya Israeli yote;

Kumbukumbu la Torati 11:7 Deuteronomy 11:7

lakini macho yenu yameiona kazi kubwa ya Bwana aliyoifanya, yote.

Kumbukumbu la Torati 11:8 Deuteronomy 11:8

Kwa hiyo yaangalieni maagizo yote niwaagizayo leo, mpate kuwa na nguvu, na kuingia mkaimiliki nchi mwivukiayo kuimiliki;

Kumbukumbu la Torati 11:9 Deuteronomy 11:9

nanyi mpate kuzifanya siku zenu kuwa nyingi juu ya nchi Bwana aliyowaapia baba zenu, ya kuwa atawapa wao na kizazi chao, nchi imiminikayo maziwa na asali

Kumbukumbu la Torati 11:10 Deuteronomy 11:10

Kwa kuwa nchi mwingiayo kuimiliki, si mfano wa nchi ya Misri mlikotoka, uliyokuwa ukipanda mbegu zako humo na kuinywesheleza kwa mguu wako, kama shamba la mboga;

Kumbukumbu la Torati 11:11 Deuteronomy 11:11

lakini nchi mwivukiayo kuimiliki ni nchi ya vilima na mabonde, nayo hunyweshwa maji ya mvua ya mbinguni;

Kumbukumbu la Torati 11:12 Deuteronomy 11:12

nayo ni nchi itunzwayo na Bwana, Mungu wako; macho ya Bwana Mungu wako, ya juu yake, tangu mwanzo wa mwaka hata mwisho wa mwaka.

Kumbukumbu la Torati 11:13 Deuteronomy 11:13

Tena itakuwa, mtakaposikiza kwa bidii maagizo yangu niwaagizayo leo, kwa kumpenda Bwana, Mungu wenu, na kumtumikia kwa mioyo yenu yote na roho zenu zote,

Kumbukumbu la Torati 11:14 Deuteronomy 11:14

ndipo nitakapowapa mvua ya nchi yenu kwa wakati wake, mvua ya masika, na mvua ya vuli, upate kuvuna nafaka yako, na divai yako, na mafuta yako.

Kumbukumbu la Torati 11:15 Deuteronomy 11:15

Nami nitakupa nyasi katika mavue yako kulisha wanyama wako wa mifugo, nawe utakula na kushiba.

Kumbukumbu la Torati 11:16 Deuteronomy 11:16

Jitunzeni nafsi zenu, mioyo yenu isije ikadanganywa, mkageuka na kutumikia miungu mingine na kuiabudu;

Kumbukumbu la Torati 11:17 Deuteronomy 11:17

hasira za Bwana zikawaka juu yenu, naye akafunga mbingu kusiwe na mvua, wala nchi isitoe matunda yake; mkaangamia kwa upesi mtoke katika nchi nzuri awapayo Bwana.

Kumbukumbu la Torati 11:18 Deuteronomy 11:18

Kwa hiyo yawekeni maneno yangu mioyoni mwenu na rohoni mwenu; yafungeni yawe dalili juu ya mikono yenu, nayo yatakuwa kama utepe katikati ya macho yenu.

Kumbukumbu la Torati 11:19 Deuteronomy 11:19

Nayo wafunzeni vijana vyenu kwa kuyazungumza uketipo katika nyumba yako, na utembeapo njiani, na ulalapo, na uondokapo.

Kumbukumbu la Torati 11:20 Deuteronomy 11:20

Tena yaandike juu ya miimo ya nyumba yako, na juu ya malango yako;

Kumbukumbu la Torati 11:21 Deuteronomy 11:21

ili siku zenu zifanywe nyingi, na za vijana vyenu nao, juu ya nchi Bwana aliyowaapia baba zenu kuwa atawapa, kama zilivyo siku za mbingu juu ya nchi.

Kumbukumbu la Torati 11:22 Deuteronomy 11:22

Kwa kuwa kwamba mtayashika kwa bidii maagizo haya yote niwaagizayo, kuyafanya; kumpenda Bwana, Mungu wenu, na kutembea katika njia zake zote, na kushikamana naye;

Kumbukumbu la Torati 11:23 Deuteronomy 11:23

ndipo Bwana atakapowafukuza mataifa haya yote mbele yenu, nanyi mtamiliki mataifa makubwa yenye nguvu kuwapita ninyi.

Kumbukumbu la Torati 11:24 Deuteronomy 11:24

Kila mahali mtakapokanyaga kwa nyayo za miguu yenu patakuwa penu; tokea hilo jangwa, na Lebanoni, na tokea mto wa Frati, mpaka bahari ya magharibi, itakuwa ndiyo mipaka yenu.

Kumbukumbu la Torati 11:25 Deuteronomy 11:25

Hapatakuwa na mtu atakayeweza kusimama mbele yenu; Bwana, Mungu wenu, ataweka utisho wenu na kuhofiwa kwenu juu ya nchi yote mtakayoikanyaga, kama alivyowaambia.

Kumbukumbu la Torati 11:26 Deuteronomy 11:26

Angalieni, nawawekea mbele yenu hivi leo baraka na laana;

Kumbukumbu la Torati 11:27 Deuteronomy 11:27

baraka ni hapo mtakapoyasikiza maagizo ya Bwana, Mungu wenu, niwaagizayo leo;

Kumbukumbu la Torati 11:28 Deuteronomy 11:28

na laana ni hapo msiposikiza maagizo ya Bwana, Mungu wenu, mkikengeuka katika njia niwaagizayo leo, kwa kuandama miungu mingine msiyoijua.

Kumbukumbu la Torati 11:29 Deuteronomy 11:29

Tena itakuwa, atakapokuleta Bwana, Mungu wako, na kukutia katika nchi uendeayo kuimiliki, ndipo uiweke baraka juu ya mlima wa Gerizimu, na laana uiweke juu ya mlima wa Ebali.

Kumbukumbu la Torati 11:30 Deuteronomy 11:30

Je! Haiwi ng'ambo ya Yordani? Nyuma ya njia ya machweo ya jua, katika nchi ya Wakanaani waketio katika Araba kuelekea Gilgali, kando ya hiyo mialoni ya More?

Kumbukumbu la Torati 11:31 Deuteronomy 11:31

Kwani ninyi mtavuka Yordani mwingie kuimiliki nchi awapayo Bwana, Mungu wenu, nanyi muimiliki na kuketi humo.

Kumbukumbu la Torati 11:32 Deuteronomy 11:32

Nanyi angalieni mzifanye amri na hukumu zote niwawekeazo leo mbele yenu.