Kumbukumbu la Torati Mlango 31 Deuteronomy

Kumbukumbu la Torati 31:1 Deuteronomy 31:1

Musa akaenda akawaambia Waisraeli maneno haya yote.

Kumbukumbu la Torati 31:2 Deuteronomy 31:2

Akawaambia, Mimi leo ni mwenye miaka mia na ishirini; siwezi tena kutoka na kuingia, na Bwana ameniambia, Hutavuka mto huu Yordani.

Kumbukumbu la Torati 31:3 Deuteronomy 31:3

Bwana Mungu wako, ndiye atakayevuka mbele yako, atawaangamiza mataifa haya mbele yako, nawe utawamiliki; na Yoshua atavuka mbele yako, kama Bwana alivyonena.

Kumbukumbu la Torati 31:4 Deuteronomy 31:4

Na Bwana atawatenda hao kama vile alivyowatenda Sihoni na Ogu, wafalme wa Waamori, na nchi yao, ambao aliwaharibu.

Kumbukumbu la Torati 31:5 Deuteronomy 31:5

Naye Bwana atawatia mikononi mwenu, nanyi mtawatenda kadiri ya amri ile niliyowaamuru.

Kumbukumbu la Torati 31:6 Deuteronomy 31:6

Iweni hodari na moyo wa ushujaa, msiogope wala msiwahofu; kwa maana Bwana, Mungu wako, yeye ndiye anayekwenda pamoja nawe, hatakupungukia wala kukuacha.

Kumbukumbu la Torati 31:7 Deuteronomy 31:7

Musa akamwita Yoshua, akamwambia machoni pa Israeli wote, Uwe hodari na moyo wa ushujaa, maana utakwenda pamoja na watu hawa hata nchi Bwana aliyowaapia baba zao, ya kwamba atawapa; nawe utawarithisha.

Kumbukumbu la Torati 31:8 Deuteronomy 31:8

Naye Bwana, yeye ndiye atakayekutangulia, atakuwa pamoja nawe, hatakupungukia wala kukuacha; usiogope wala usifadhaike.

Kumbukumbu la Torati 31:9 Deuteronomy 31:9

Musa akaiandika torati hii, akawapa makuhani, wana wa Lawi, waliolichukua sanduku la agano la Bwana, na wazee wote wa Israeli.

Kumbukumbu la Torati 31:10 Deuteronomy 31:10

Musa, akawaamuru, akasema, Mwisho wa kila mwaka wa saba, wakati wa maachilio, wakati ulioamriwa wa sikukuu ya vibanda,

Kumbukumbu la Torati 31:11 Deuteronomy 31:11

Israeli wote wafikapo ili kuonekana mbele za Bwana, Mungu wako, mahali pale atakapopachagua, uisome torati hii mbele ya Israeli wote masikioni mwao.

Kumbukumbu la Torati 31:12 Deuteronomy 31:12

Wakusanye watu, wanaume na wanawake na watoto, na mgeni wako aliyemo malangoni mwako wapate kusikia na kujifunza, na kumcha Bwana, Mungu wenu, na kuangalia kutenda maneno yote ya torati hii;

Kumbukumbu la Torati 31:13 Deuteronomy 31:13

na watoto wao wasiojua, wapate kusikia na kujifunza kumcha Bwana, Mungu wenu, siku zote mtakazokaa katika nchi mnayoivukia Yordani ili kuimiliki.

Kumbukumbu la Torati 31:14 Deuteronomy 31:14

Bwana akamwambia Musa, Tazama, siku zako za kufa zinakaribia, umwite Yoshua, nanyi mkajihudhurishe katika hema ya kukutania, ili nipate kumwagiza kazi. Musa na Yoshua wakaenda, wakajihudhurisha ndani ya hema ya kukutania.

Kumbukumbu la Torati 31:15 Deuteronomy 31:15

Bwana akaonekana katika Hema katika nguzo ya wingu; na ile nguzo ya wingu ikasimama juu ya mlango wa Hema.

Kumbukumbu la Torati 31:16 Deuteronomy 31:16

Bwana akamwambia Musa, Angalia, wewe utalala na baba zako; na watu hawa wataondoka, wataifuata kwa ukahaba miungu ya kigeni ya nchi waiendeayo kuwa kati yao, nao wataniacha mimi na kulivunja agano langu, nililofanya nao.

Kumbukumbu la Torati 31:17 Deuteronomy 31:17

Ndipo hasira yangu itakapowaka juu yao siku hiyo, nami nitawaacha, nitawaficha uso wangu, nao wataliwa, tena watajiliwa na mambo maovu mengi na mashaka; hata waseme siku hiyo, Je! Kujiliwa kwetu na maovu haya si kwa sababu Mungu wetu hayumo kati yetu?

Kumbukumbu la Torati 31:18 Deuteronomy 31:18

Nami nitawaficha uso wangu kwa kweli siku hiyo, kwa maovu yote waliyoyafanya, kwa kuigeukia hiyo miungu mingine.

Kumbukumbu la Torati 31:19 Deuteronomy 31:19

Basi sasa jiandikieni wimbo huu, uwafundishe wana wa Israeli; kawatie vinywani mwao, ili uwe shahidi kwangu wimbo huu, juu ya wana wa Israeli.

Kumbukumbu la Torati 31:20 Deuteronomy 31:20

Kwa kuwa nitakapokwisha kuwatia katika nchi niliyowaapia baba zao, imiminikayo maziwa na asali; nao watakapokwisha kula na kushiba, na kuwanda; ndipo watakapoigeukia hiyo miungu mingine, na kuitumikia, na kunidharau mimi, na kulivunja agano langu.

Kumbukumbu la Torati 31:21 Deuteronomy 31:21

Tena itakuwa, wakiisha kujiliwa na mambo maovu mengi na mashaka, utashuhudia wimbo huu mbele yao kama shahidi, kwa maana hautasahauliwa katika vinywa vya uzao wao; kwani nayajua mawazo yao wayawazayo, hata sasa kabla sijawatia katika nchi niliyoapa.

Kumbukumbu la Torati 31:22 Deuteronomy 31:22

Basi Musa akauandika wimbo huu siku iyo hiyo, akawafundisha wana wa Israeli.

Kumbukumbu la Torati 31:23 Deuteronomy 31:23

Akamwagiza Yoshua, mwana wa Nuni, akamwambia, Uwe hodari na moyo mkuu, kwa kuwa utawapeleka wana wa Israeli katika nchi niliyowaapia; nami nitakuwa pamoja nawe.

Kumbukumbu la Torati 31:24 Deuteronomy 31:24

Basi ikawa hapo Musa alipomaliza kuandika maneno ya torati hii katika chuo, hata yakaisha,

Kumbukumbu la Torati 31:25 Deuteronomy 31:25

ndipo Musa akawaamuru Walawi waliokuwa wakilichukua sanduku la agano la Bwana akawaambia,

Kumbukumbu la Torati 31:26 Deuteronomy 31:26

Twaeni chuo hiki cha torati, mkiweke kando ya sanduku la agano la Bwana, Mungu wenu, ili kiwepo kama shahidi juu yako.

Kumbukumbu la Torati 31:27 Deuteronomy 31:27

Kwa kuwa uasi wako naujua, na shingo yako ngumu; angalieni, mimi nikali hai pamoja nanyi leo, mmekuwa waasi juu ya Bwana; siuze nitakapokwisha kufa!

Kumbukumbu la Torati 31:28 Deuteronomy 31:28

Nikutanishieni wazee wote wa kabila zenu, na maakida yenu, ili niseme maneno haya masikioni mwao, na kuwashuhudizia mbingu na nchi juu yao.

Kumbukumbu la Torati 31:29 Deuteronomy 31:29

Kwa sababu najua baada ya kufa kwangu mtajiharibu kabisa, na kukengeuka katika njia niliyowaamuru; nayo mabaya yatawapata siku za mwisho, kwa vile mtakavyofanya maovu machoni pa Bwana kumtia kasirani kwa kazi ya mikono yenu.

Kumbukumbu la Torati 31:30 Deuteronomy 31:30

Musa akasema maneno ya wimbo huu masikioni mwa kusanyiko la wana wa Israeli hata yakaisha.