Mithali Mlango 21 Proverbs

Mithali 21:1 Proverbs 21:1

Moyo wa mfalme huwa katika mkono wa Bwana; Kama mifereji ya maji huugeuza po pote apendapo.

Mithali 21:2 Proverbs 21:2

Kila njia ya mtu ni sawa machoni pake mwenyewe; Bali Bwana huipima mioyo.

Mithali 21:3 Proverbs 21:3

Kutenda haki na hukumu Humpendeza Bwana kuliko kutoa sadaka.

Mithali 21:4 Proverbs 21:4

Macho yenye kiburi, na moyo wa kutakabari, Hata ukulima wa waovu, ni dhambi.

Mithali 21:5 Proverbs 21:5

Mawazo ya wenye bidii huuelekea utajiri tu; Bali kila mwenye pupa huuelekea uhitaji.

Mithali 21:6 Proverbs 21:6

Kupata akiba ya mali kwa ulimi wa uongo Ni moshi upeperushwao; ni kutafuta mauti.

Mithali 21:7 Proverbs 21:7

Jeuri ya wabaya itawaondolea mbali; Kwa sababu wamekataa kutenda hukumu.

Mithali 21:8 Proverbs 21:8

Njia yake aliyelemewa na dhambi imepotoka sana; Bali mtu aliye safi, kazi yake ni sawasawa.

Mithali 21:9 Proverbs 21:9

Ni afadhali kukaa katika pembe ya darini, Kuliko katika nyumba pana pamoja na mwanamke mgomvi.

Mithali 21:10 Proverbs 21:10

Nafsi ya mtu mbaya hutamani uovu; Jirani yake hapati fadhili machoni pake.

Mithali 21:11 Proverbs 21:11

Mwenye mzaha aadhibiwapo, mjinga hupata hekima; Na mwenye hekima afundishwapo, hupokea maarifa.

Mithali 21:12 Proverbs 21:12

Mwenye haki huitafakari nyumba ya mtu mbaya; Jinsi wabaya waangushwavyo wakaangamia.

Mithali 21:13 Proverbs 21:13

Azibaye masikio yake asisikie kilio cha maskini, Yeye naye atalia, lakini hatasikiwa.

Mithali 21:14 Proverbs 21:14

Kipawa cha siri hutuliza hasira; Na rushwa bindoni humliza ghadhabu kali.

Mithali 21:15 Proverbs 21:15

Ni furaha yao wenye haki kutenda hukumu; Lakini ni uharibifu kwao watendao maovu.

Mithali 21:16 Proverbs 21:16

Mtu aikosaye njia ya busara Atakaa katika mkutano wao waliokufa.

Mithali 21:17 Proverbs 21:17

Mtu apendaye anasa atakuwa maskini; Apendaye mvinyo na mafuta hatakuwa tajiri.

Mithali 21:18 Proverbs 21:18

Mtu asiye haki ni fidia ya wenye haki; Naye afanyaye hila ni badala ya watu wa adili.

Mithali 21:19 Proverbs 21:19

Ni afadhali kukaa katika nchi ya nyika; Kuliko na mwanamke mgomvi, mchokozi.

Mithali 21:20 Proverbs 21:20

Kuna hazina ya thamani na mafuta katika maskani ya mwenye hekima; Bali mwanadamu aliye mpumbavu huyameza.

Mithali 21:21 Proverbs 21:21

Aandamaye haki na fadhili, Ataona uhai na haki na heshima.

Mithali 21:22 Proverbs 21:22

Mwenye hekima huupandia mji wao wenye nguvu; Na kuziangusha nguvu za tumaini lao.

Mithali 21:23 Proverbs 21:23

Mtu azuiaye kinywa chake na ulimi wake, Atajilinda nafsi yake na taabu.

Mithali 21:24 Proverbs 21:24

Mwenye kiburi na kutakabari, jina lake ni mbishi; Hutenda mambo katika majivuno ya kiburi chake.

Mithali 21:25 Proverbs 21:25

Matakwa yake mtu mvivu humfisha, Kwa maana mikono yake hukataa kufanya kazi.

Mithali 21:26 Proverbs 21:26

Kuna atamaniye kwa choyo mchana kutwa; Bali mwenye haki hutoa wala hanyimi.

Mithali 21:27 Proverbs 21:27

Sadaka ya wasio haki ni chukizo; Si zaidi sana ailetapo mwenye nia mbaya!

Mithali 21:28 Proverbs 21:28

Shahidi wa uongo atapotea; Bali mtu asikiaye atasema maneno yadumuyo.

Mithali 21:29 Proverbs 21:29

Asiye haki huufanya uso wake kuwa mgumu; Bali mtu mnyofu huzifikiri njia zake.

Mithali 21:30 Proverbs 21:30

Hapana hekima, wala ufahamu, Wala shauri, juu ya Bwana.

Mithali 21:31 Proverbs 21:31

Farasi huwekwa tayari kwa siku ya vita; Lakini Bwana ndiye aletaye wokovu.