Mithali Mlango 10 Proverbs

Mithali 10:1 Proverbs 10:1

Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye; Bali mwana mpumbavu ni mzigo wa mamaye.

Mithali 10:2 Proverbs 10:2

Hazina za uovu hazifaidii kitu; Bali haki huokoa na mauti.

Mithali 10:3 Proverbs 10:3

Bwana hataiacha nafsi ya mwenye haki ife na njaa; Bali tamaa ya mtu mwovu huisukumia mbali.

Mithali 10:4 Proverbs 10:4

Atendaye mambo kwa mkono mlegevu huwa maskini; Bali mkono wake aliye na bidii hutajirisha.

Mithali 10:5 Proverbs 10:5

Akusanyaye wakati wa hari ni mwana mwenye hekima; Bali asinziaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.

Mithali 10:6 Proverbs 10:6

Baraka humkalia mwenye haki kichwani; Bali jeuri hufunika kinywa chake mtu mwovu.

Mithali 10:7 Proverbs 10:7

Kuwakumbuka wenye haki huwa na baraka; Bali jina la mtu mwovu litaoza.

Mithali 10:8 Proverbs 10:8

Aliye na akili moyoni mwake atapokea agizo; Bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataanguka.

Mithali 10:9 Proverbs 10:9

Aendaye kwa unyofu huenda salama; Bali apotoshaye njia zake atajulikana.

Mithali 10:10 Proverbs 10:10

Akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko; Bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataanguka.

Mithali 10:11 Proverbs 10:11

Kinywa chake mwenye haki ni chemchemi ya uzima; Bali jeuri hufunika kinywa chake mtu mwovu,

Mithali 10:12 Proverbs 10:12

Kuchukiana huondokesha fitina; Bali kupendana husitiri makosa yote.

Mithali 10:13 Proverbs 10:13

Hekima hupatikana midomoni mwa mwenye ufahamu; Bali fimbo hufaa kwa mgongo wake asiye na ufahamu.

Mithali 10:14 Proverbs 10:14

Watu wenye akili huweka akiba ya maarifa; Bali kinywa cha mpumbavu ni uangamivu ulio karibu.

Mithali 10:15 Proverbs 10:15

Mali ya mtu tajiri ni mji wake wa nguvu; Uangamivu wa maskini ni umaskini wao.

Mithali 10:16 Proverbs 10:16

Kazi yake mwenye haki huuelekea uzima; Mazao ya wabaya huuelekea dhambi.

Mithali 10:17 Proverbs 10:17

Akubaliye kurudiwa huwa katika njia ya uzima; Bali yeye aachaye maonyo hukosa.

Mithali 10:18 Proverbs 10:18

Yeye afichaye chuki ana midomo ya uongo, Na yeye asingiziaye ni mpumbavu.

Mithali 10:19 Proverbs 10:19

Katika wingi wa maneno hapakosi kuwa na maovu; Bali yeye azuiaye midomo yake hufanya akili.

Mithali 10:20 Proverbs 10:20

Ulimi wa mwenye haki ni kama fedha teule; Moyo wa mtu mbaya haufai kitu.

Mithali 10:21 Proverbs 10:21

Midomo ya mwenye haki hulisha watu wengi; Bali wapumbavu hufa kwa kuwa hawana ufahamu.

Mithali 10:22 Proverbs 10:22

Baraka ya Bwana hutajirisha, Wala hachanganyi huzuni nayo.

Mithali 10:23 Proverbs 10:23

Kwa mpumbavu kutenda maovu ni kama mchezo; Bali mtu mwenye ufahamu ana hekima.

Mithali 10:24 Proverbs 10:24

Aogopacho mtu asiye haki ndicho kitakachomjilia; Na wenye haki watapewa matakwa yao.

Mithali 10:25 Proverbs 10:25

Kisulisuli kikiisha pita asiye haki hayuko tena; Bali mwenye haki ni msingi wa milele.

Mithali 10:26 Proverbs 10:26

Kama siki menoni, na kama moshi machoni, Ndivyo alivyo mtu mvivu kwao wamtumao.

Mithali 10:27 Proverbs 10:27

Kumcha Bwana kwaongeza siku za mtu; Bali miaka yao wasio haki itapunguzwa.

Mithali 10:28 Proverbs 10:28

Matumaini yao wenye haki yatakuwa furaha; Bali kutaraji kwao wasio haki kutapotea.

Mithali 10:29 Proverbs 10:29

Njia ya Bwana ni kimbilio lake mtu mkamilifu; Bali ni uharibifu kwao watendao maovu.

Mithali 10:30 Proverbs 10:30

Mwenye haki hataondolewa milele; Bali wasio haki hawatakaa katika nchi.

Mithali 10:31 Proverbs 10:31

Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima; Bali ulimi wa ukaidi utakatiliwa mbali.

Mithali 10:32 Proverbs 10:32

Midomo ya mwenye haki huyajua yatakayokubaliwa; Bali kinywa chao wasio haki hunena ukaidi.