Mithali Mlango 28 Proverbs

Mithali 28:1 Proverbs 28:1

Waovu hukimbia wasipofuatiwa na mtu; Bali wenye haki ni wajasiri kama simba.

Mithali 28:2 Proverbs 28:2

Kwa sababu ya maasi ya nchi wakuu wake huwa wengi; Bali kwa wenye ufahamu na maarifa hali ya nchi hudumishwa

Mithali 28:3 Proverbs 28:3

Mtu mhitaji awaoneaye maskini, Ni kama mvua ya dhoruba isiyosaza chakula.

Mithali 28:4 Proverbs 28:4

Wao waiachao sheria huwasifu waovu; Bali wao waishikao hushindana nao.

Mithali 28:5 Proverbs 28:5

Watu wabaya hawaelewi na hukumu; Bali wamtafutao Bwana huelewa na yote.

Mithali 28:6 Proverbs 28:6

Afadhali maskini aendaye katika unyofu wake, Kuliko mpotofu wa njia angawa ni tajiri.

Mithali 28:7 Proverbs 28:7

Yeye aishikaye sheria ni mwana mwenye hekima; Bali aliye rafiki wa walafi humwaibisha babaye.

Mithali 28:8 Proverbs 28:8

Yeye azidishaye mali yake kwa riba na faida, Humkusanyia mtu awahurumiaye maskini.

Mithali 28:9 Proverbs 28:9

Yeye aligeuzaye sikio lake asiisikie sheria, Hata sala yake ni chukizo.

Mithali 28:10 Proverbs 28:10

Kila mtu awapotezaye wenye haki katika njia mbaya, Ataanguka katika rima lake mwenyewe; Bali wakamilifu watarithi mema.

Mithali 28:11 Proverbs 28:11

Mtu tajiri ana hekima machoni pake mwenyewe; Bali maskini mwenye ufahamu humchunguza sana.

Mithali 28:12 Proverbs 28:12

Wenye haki washindapo, uko utukufu mwingi; Bali waovu waondokapo, watu hujificha.

Mithali 28:13 Proverbs 28:13

Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema.

Mithali 28:14 Proverbs 28:14

Mwanadamu mwenye kicho yu heri sikuzote; Bali mshupavu wa moyo ataangukia madhara.

Mithali 28:15 Proverbs 28:15

Kama simba angurumaye, na dubu mwenye njaa; Ndivyo alivyo mtu mbaya awatawalaye maskini.

Mithali 28:16 Proverbs 28:16

Mkuu aliyepungukiwa na akili huwaonea watu sana; Bali achukiaye kutamani ataongeza siku zake.

Mithali 28:17 Proverbs 28:17

Aliyelemewa na damu ya mtu Atalikimbilia shimo; wala mtu asimzuie.

Mithali 28:18 Proverbs 28:18

Aendaye kwa unyofu ataokolewa; Bali mkaidi wa njia zake ataanguka mara.

Mithali 28:19 Proverbs 28:19

Alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele; Bali afuataye mambo ya upuzi atapata umaskini wa kumtosha.

Mithali 28:20 Proverbs 28:20

Mtu mwaminifu atakuwa na baraka tele; Lakini afanyaye haraka kuwa tajiri hakosi ataadhibiwa.

Mithali 28:21 Proverbs 28:21

Kupendelea watu si kwema; Wala mtu kuasi kwa ajili ya kipande cha mkate.

Mithali 28:22 Proverbs 28:22

Mwenye husuda afanya haraka kuwa tajiri; Wala haufikiri uhitaji utakaomjilia.

Mithali 28:23 Proverbs 28:23

Amkemeaye mwenzake hatimaye atapata kibali; Zaidi ya mtu ajipendekezaye kwa ulimi wake.

Mithali 28:24 Proverbs 28:24

Aibaye mali ya babaye au mamaye, na kusema, Si kosa; Mwana huyo ni rafiki wa mtu mharibifu.

Mithali 28:25 Proverbs 28:25

Mwenye nafsi ya kutamani huchochea fitina; Bali amtumainiye Bwana atawandishwa.

Mithali 28:26 Proverbs 28:26

Mwenye kujitumainia moyo wake ni mjinga; Bali yeye aendaye kwa busara ataokolewa.

Mithali 28:27 Proverbs 28:27

Mwenye kuwagawia maskini hatahitaji kitu; Bali afichaye macho yake atakuwa na laana nyingi.

Mithali 28:28 Proverbs 28:28

Wasio haki wainukapo, wanadamu hujificha; Bali waangamiapo, wenye haki huongezeka.