Luka Mlango 20 Luke

Luka 20:1 Luke 20:1

Ikawa siku moja, alipokuwa akiwafundisha watu hekaluni, na kuihubiri habari njema, wakuu wa makuhani na waandishi pamoja na wazee walimtokea ghafula;

Luka 20:2 Luke 20:2

wakamwambia, wakisema, Tuambie, unatenda mambo hayo kwa mamlaka gani? Tena, ni nani aliyekupa mamlaka hii?

Luka 20:3 Luke 20:3

Akajibu akawaambia, Nami nitawauliza ninyi neno moja; niambieni,

Luka 20:4 Luke 20:4

Ubatizo wa Yohana, je! Ulitoka mbinguni au kwa wanadamu?

Luka 20:5 Luke 20:5

Wakahojiana wao kwa wao, wakisema, Kama tukisema ulitoka mbinguni, atasema, Basi, mbona hamkumwamini?

Luka 20:6 Luke 20:6

Na tukisema ulitoka kwa wanadamu, watu wote watatupiga kwa mawe, kwa kuwa wamemkubali Yohana kuwa ni nabii.

Luka 20:7 Luke 20:7

Wakajibu, kwamba, Hatujui ulikotoka.

Luka 20:8 Luke 20:8

Yesu akawaambia, Wala mimi siwaambii ninyi ni kwa mamlaka gani ninatenda mambo haya.

Luka 20:9 Luke 20:9

Akaanza kuwaambia watu mfano huu; Mtu mmoja alipanda shamba la mizabibu; akapangisha wakulima, akaenda akakaa katika nchi nyingine muda mrefu.

Luka 20:10 Luke 20:10

Na wakati wa mavuno alituma mtumwa kwa wale wakulima ili wampe baadhi ya matunda ya mizabibu; wakulima wakampiga wakamfukuza mikono mitupu.

Luka 20:11 Luke 20:11

Akatuma na mtumwa mwingine. Wakampiga huyu naye, wakamwaibisha wakamfukuza mikono mitupu.

Luka 20:12 Luke 20:12

Akamtuma na wa tatu; huyu naye wakamtia jeraha, wakamtupa nje.

Luka 20:13 Luke 20:13

Basi, bwana wa shamba la mizabibu alisema, Nifanyeje? Nitamtuma mwanangu, mpendwa wangu; yamkini watamheshimu yeye.

Luka 20:14 Luke 20:14

Lakini, wale wakulima walipomwona, walishauriana wao kwa wao, wakisema, Huyu ndiye mrithi; haya, na tumwue, ili urithi uwe wetu.

Luka 20:15 Luke 20:15

Wakamtupa nje ya shamba la mizabibu, wakamwua. Basi, bwana wa shamba la mizabibu atawatendeje?

Luka 20:16 Luke 20:16

Atakuja na kuwaangamiza wakulima wale, na lile shamba la mizabibu atawapa wengine. Waliposikia hayo walisema, Hasha! Yasitukie haya!

Luka 20:17 Luke 20:17

Akawakazia macho akasema, Maana yake nini basi neno hili lililoandikwa, Jiwe walilolikataa waashi, Hilo limekuwa jiwe kuu la pembeni?

Luka 20:18 Luke 20:18

Kila mtu aangukaye juu ya jiwe hilo atavunjika-vunjika; na ye yote ambaye litamwangukia litamsaga kabisa.

Luka 20:19 Luke 20:19

Nao waandishi na wakuu wa makuhani walitafuta kumkamata saa iyo hiyo, wakawaogopa watu, maana walitambua ya kwamba mfano huu amewanenea wao.

Luka 20:20 Luke 20:20

Wakamvizia-vizia, wakatuma wapelelezi waliojifanya kuwa watu wa haki, ili wamnase katika maneno yake, wapate kumtia katika enzi na mamlaka ya liwali.

Luka 20:21 Luke 20:21

Wakamwuliza, wakisema, Mwalimu, twajua ya kwamba wasema na kufundisha yaliyo ya haki, wala hujali cheo cha mtu, bali unafundisha njia ya Mungu kwa kweli.

Luka 20:22 Luke 20:22

Je! Ni halali tumpe Kaisari kodi, au sivyo?

Luka 20:23 Luke 20:23

Lakini yeye alitambua hila yao, akawaambia,

Luka 20:24 Luke 20:24

Nionyesheni dinari. Ina sura na anwani ya nani? Wakamjibu, Ya Kaisari.

Luka 20:25 Luke 20:25

Akawaambia, Basi, vya Kaisari mpeni Kaisari, na vya Mungu mpeni Mungu.

Luka 20:26 Luke 20:26

Wala hawakuweza kumshitaki kwa maneno yake mbele ya watu; wakastaajabia majibu yake, wakanyamaa.

Luka 20:27 Luke 20:27

Kisha baadhi ya Masadukayo wakamwendea, wale wasemao ya kwamba hakuna ufufuo, wakamwuliza,

Luka 20:28 Luke 20:28

wakisema, Mwalimu, Musa alituandikia ya kuwa, mtu akifiwa na ndugu yake mwenye mke, lakini hana mtoto na amtwae huyu mke, ampatie ndugu yake mzao.

Luka 20:29 Luke 20:29

Basi, kulikuwa na ndugu saba. Wa kwanza alioa mke, akafa hana mtoto;

Luka 20:30 Luke 20:30

na wa pili [akamtwaa yule mke, akafa hana mtoto;]

Luka 20:31 Luke 20:31

hata wa tatu akamwoa, na kadhalika wote saba, wakafa, wasiache watoto.

Luka 20:32 Luke 20:32

Mwisho akafa yule mke naye.

Luka 20:33 Luke 20:33

Basi, katika ufufuo atakuwa mke wa yupi? Maana aliolewa na wote saba.

Luka 20:34 Luke 20:34

Yesu akawaambia, Wana wa ulimwengu huu huoa na kuolewa;

Luka 20:35 Luke 20:35

lakini, wale wahesabiwao kuwa wamestahili kuupata ulimwengu ule, na kule kufufuka katika wafu, hawaoi wala hawaolewi;

Luka 20:36 Luke 20:36

wala hawawezi kufa tena; kwa sababu huwa sawasawa na malaika, nao ni wana wa Mungu, kwa vile walivyo wana wa ufufuo.

Luka 20:37 Luke 20:37

Lakini, ya kuwa wafu hufufuliwa, hata na Musa alionyesha katika sura ya Kijiti, hapo alipomtaja Bwana kuwa ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo.

Luka 20:38 Luke 20:38

Naye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai; kwa kuwa wote huishi kwake.

Luka 20:39 Luke 20:39

Waandishi wengine wakajibu wakamwambia, Mwalimu, umesema vema;

Luka 20:40 Luke 20:40

wala hawakuthubutu kumwuliza neno baada ya hayo.

Luka 20:41 Luke 20:41

Akawaambia, Wasemaje watu kwamba Kristo ni Mwana wa Daudi?

Luka 20:42 Luke 20:42

Maana, Daudi mwenyewe asema katika chuo cha Zaburi, Bwana alimwambia Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume,

Luka 20:43 Luke 20:43

Hata niwaweke adui zako Kuwa kiti cha kuwekea miguu yako.

Luka 20:44 Luke 20:44

Basi Daudi amwita Bwana; amekuwaje mwana wake?

Luka 20:45 Luke 20:45

Na watu wote walipokuwa wakimsikiliza, aliwaambia wanafunzi wake,

Luka 20:46 Luke 20:46

Jilindeni na waandishi, wapendao kutembea wamevaa mavazi marefu, na kusalimiwa masokoni, na kuketi mbele katika masinagogi, na viti vya mbele karamuni.

Luka 20:47 Luke 20:47

Wanakula nyumba za wajane, na kwa unafiki husali sala ndefu. Hao watapata hukumu iliyo kuu.