Luka Mlango 23 Luke

Luka 23:1 Luke 23:1

Wakasimama mkutano wote, wakampeleka kwa Pilato.

Luka 23:2 Luke 23:2

Wakaanza kumshitaki, wakisema, Tumemwona huyu akipotosha taifa letu, na kuwazuia watu wasimpe Kaisari kodi, akisema kwamba yeye mwenyewe ni Kristo, mfalme.

Luka 23:3 Luke 23:3

Pilato akamwuliza, akisema, Wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi? Akajibu akamwambia, Wewe wasema.

Luka 23:4 Luke 23:4

Pilato akawaambia wakuu wa makuhani na makutano, Sioni neno lililo ovu katika mtu huyu.

Luka 23:5 Luke 23:5

Nao walikaza sana, wakisema, Huwataharakisha watu, akifundisha katika Uyahudi yote, tokea Galilaya mpaka huku.

Luka 23:6 Luke 23:6

Pilato aliposikia hayo aliuliza kama huyu ni mtu wa Galilaya.

Luka 23:7 Luke 23:7

Na alipopata habari ya kuwa yu chini ya mamlaka ya Herode, alimpeleka kwa Herode, kwa kuwa yeye naye alikuwapo Yerusalemu siku zile.

Luka 23:8 Luke 23:8

Na Herode alipomwona Yesu alifurahi sana, kwa sababu alikuwa akitaka sana kumwona tangu siku nyingi, maana amesikia habari zake, akataraji kuona ishara iliyofanywa na yeye.

Luka 23:9 Luke 23:9

Akamwuliza maneno mengi, yeye asimjibu lo lote.

Luka 23:10 Luke 23:10

Wakuu wa makuhani na waandishi wakasimama wakamshitaki kwa nguvu sana.

Luka 23:11 Luke 23:11

Basi Herode akamfanya duni, pamoja na askari zake, akamdhihaki, na kumvika mavazi mazuri; kisha akamrudisha kwa Pilato.

Luka 23:12 Luke 23:12

Basi siku ile ile Herode na Pilato walipatana kwa urafiki kwa maana hapo kwanza walikuwa na uadui wao kwa wao.

Luka 23:13 Luke 23:13

Na Pilato akawakutanisha wakuu wa makuhani, na wakubwa, na watu,

Luka 23:14 Luke 23:14

akawaambia, Mtu huyu mmemleta kwangu kana kwamba anapotosha watu; nami, tazama, nimeamua mambo yake mbele yenu, ila sikuona kwake kosa lo lote katika mambo hayo mliyomshitaki;

Luka 23:15 Luke 23:15

wala hata Herode, kwa maana amemrudisha kwetu; basi tazama, hakuna neno lo lote alilolitenda lipasalo kufa.

Luka 23:16 Luke 23:16

Kwa hiyo nitamrudi, kisha nitamfungua. [

Luka 23:17 Luke 23:17

Maana ilimlazimu kuwafungulia mfungwa mmoja wakati wa sikukuu.]

Luka 23:18 Luke 23:18

Wakapiga kelele wote pamoja, wakisema, Mwondoe huyu, utufungulie Baraba.

Luka 23:19 Luke 23:19

Naye ni mtu aliyetupwa gerezani kwa ajili ya fitina iliyotokea mjini, na kwa uuaji

Luka 23:20 Luke 23:20

Basi Pilato alisema nao mara ya pili, kwa vile alivyotaka kumfungua Yesu.

Luka 23:21 Luke 23:21

Lakini wakapiga kelele, wakisema, Msulibishe. Msulibishe.

Luka 23:22 Luke 23:22

Akawaambia mara ya tatu, Kwa sababu gani? Huyu ametenda uovu gani? Sikuona kwake hata neno lipasalo kufa. Basi nikiisha kumrudi nitamfungua.

Luka 23:23 Luke 23:23

Lakini wakatoa sauti zao kwa nguvu sana, wakitaka asulibiwe. Sauti zao zikashinda.

Luka 23:24 Luke 23:24

Pilato akahukumu kwamba haja yao ifanyike.

Luka 23:25 Luke 23:25

Akamfungua yule aliyetupwa gerezani kwa ajili ya fitina na uuaji, yule waliyemtaka, akamtoa Yesu wamfanyie watakavyo.

Luka 23:26 Luke 23:26

Na walipokuwa wakimwondoa walimkamata mtu mmoja, Simoni Mkirene, aliyekuwa ametoka shamba, wakamtwika msalaba, auchukue nyuma yake Yesu.

Luka 23:27 Luke 23:27

Mkutano mkubwa wa watu wakamfuata, na wanawake waliokuwa wakijipiga vifua na kumwombolezea.

Luka 23:28 Luke 23:28

Yesu akawageukia, akasema, Enyi binti za Yerusalemu, msinililie mimi, bali jililieni nafsi zenu na watoto wenu.

Luka 23:29 Luke 23:29

Kwa maana tazama, siku zitakuja watakaposema, Heri walio tasa, na matumbo yasiyozaa, na maziwa yasiyonyonyesha.

Luka 23:30 Luke 23:30

Ndipo watakapoanza kuiambia milima, Tuangukieni, na vilima, Tufunikeni.

Luka 23:31 Luke 23:31

Kwa kuwa kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

Luka 23:32 Luke 23:32

Wakapelekwa na wawili wengine, wahalifu, wauawe pamoja naye.

Luka 23:33 Luke 23:33

Na walipofika mahali paitwapo Fuvu la Kichwa, ndipo walipomsulibisha yeye, na wale wahalifu, mmoja upande wa kuume, na mmoja upande wa kushoto.

Luka 23:34 Luke 23:34

Yesu akasema, Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo. Wakagawa mavazi yake, wakipiga kura.

Luka 23:35 Luke 23:35

Watu wakasimama wakitazama. Wale wakuu nao walikuwa wakimfanyia mzaha, wakisema, Aliokoa wengine; na ajiokoe mwenyewe, kama ndiye Kristo wa Mungu, mteule wake.

Luka 23:36 Luke 23:36

Wale askari nao wakamfanyia dhihaka, wakimwendea na kumletea siki,

Luka 23:37 Luke 23:37

huku wakisema, Kama wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi, ujiokoe mwenyewe.

Luka 23:38 Luke 23:38

Na juu yake palikuwa na anwani; HUYU NDIYE MFALME WA WAYAHUDI.

Luka 23:39 Luke 23:39

Na mmoja wa wale wahalifu waliotungikwa alimtukana, akisema, Je! Wewe si Kristo? Jiokoe nafsi yako na sisi.

Luka 23:40 Luke 23:40

Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, Wewe humwogopi hata Mungu, nawe u katika hukumu iyo hiyo?

Luka 23:41 Luke 23:41

Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa.

Luka 23:42 Luke 23:42

Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.

Luka 23:43 Luke 23:43

Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi.

Luka 23:44 Luke 23:44

Hapo ilikuwa yapata saa sita, kukawa giza juu ya nchi yote hata saa kenda,

Luka 23:45 Luke 23:45

jua limepungua nuru yake; pazia la hekalu likapasuka katikati.

Luka 23:46 Luke 23:46

Yesu akalia kwa sauti kuu, akasema, Ee Baba, mikononi mwako naiweka roho yangu.

Luka 23:47 Luke 23:47

Alipokwisha kusema hayo alikata roho. Yule akida alipoona yaliyotukia, alimtukuza Mungu, akisema, Hakika yake, mtu huyu alikuwa mwenye haki.

Luka 23:48 Luke 23:48

Na makutano yote ya watu waliokuwa wamekutanika kutazama mambo hayo, walipoona yaliyotendeka, wakaenda zao kwao, wakijipiga-piga vifua.

Luka 23:49 Luke 23:49

Na wote waliojuana naye, na wale wanawake walioandamana naye toka Galilaya, wakasimama kwa mbali, wakitazama mambo hayo.

Luka 23:50 Luke 23:50

Na tazama, akatoka mtu mmoja, jina lake Yusufu, ambaye ni mtu wa baraza, mtu mwema, mwenye haki;

Luka 23:51 Luke 23:51

(wala hakulikubali shauri na tendo lao), naye ni mtu wa Arimathaya, mji mmoja wa Wayahudi, tena anautazamia ufalme wa Mungu;

Luka 23:52 Luke 23:52

mtu huyo alikwenda kwa Pilato, akataka kupewa mwili wa Yesu.

Luka 23:53 Luke 23:53

Akaushusha, akauzinga sanda ya kitani, akauweka katika kaburi lililochongwa mwambani, ambalo hajalazwa mtu bado ndani yake.

Luka 23:54 Luke 23:54

Na siku ile ilikuwa siku ya Maandalio, na sabato ikaanza kuingia.

Luka 23:55 Luke 23:55

Na wale wanawake waliokuja naye toka Galilaya walifuata, wakaliona kaburi, na jinsi mwili wake ulivyowekwa.

Luka 23:56 Luke 23:56

Wakarudi, wakafanya tayari manukato na marhamu. Na siku ya sabato walistarehe kama ilivyoamriwa.