Luka Mlango 17 Luke

Luka 17:1 Luke 17:1

Akawaambia wanafunzi wake, Makwazo hayana budi kuja, lakini ole wake mtu yule ambaye yaja kwa sababu yake!

Luka 17:2 Luke 17:2

Ingemfaa zaidi mtu huyo jiwe la kusagia lifungwe shingoni mwake, akatupwe baharini, kuliko kumkosesha mmojawapo wa wadogo hawa.

Luka 17:3 Luke 17:3

Jilindeni; kama ndugu yako akikosa, mwonye; akitubu msamehe.

Luka 17:4 Luke 17:4

Na kama akikukosa mara saba katika siku moja, na kurudi kwako mara saba, akisema, Nimetubu, msamehe.

Luka 17:5 Luke 17:5

Mitume wakamwambia Bwana, Tuongezee imani.

Luka 17:6 Luke 17:6

Bwana akasema, Kama mngekuwa na imani kiasi cha chembe ya haradali, mngeuambia mkuyu huu, Ng'oka, ukapandwe baharini, nao ungewatii.

Luka 17:7 Luke 17:7

Lakini, ni nani kwenu mwenye mtumwa alimaye au achungaye ng'ombe, atakayemwambia mara arudipo kutoka shambani, Njoo upesi, keti, ule chakula?

Luka 17:8 Luke 17:8

Je! Hatamwambia, Nifanyie tayari chakula, nile; jifunge unitumikie, hata niishe kula na kunywa, ndipo nawe utakapokula na kunywa?

Luka 17:9 Luke 17:9

Je! Atampa asante yule mtumwa, kwa sababu ameyafanya aliyoagizwa?

Luka 17:10 Luke 17:10

Vivyo hivyo nanyi, mtakapokwisha kuyafanya yote mliyoagizwa, semeni, Sisi tu watumwa wasio na faida; tumefanya tu yaliyotupasa kufanya.

Luka 17:11 Luke 17:11

Ikawa walipokuwa njiani kwenda Yerusalemu, alikuwa akipita katikati ya Samaria na Galilaya.

Luka 17:12 Luke 17:12

Na alipoingia katika kijiji kimoja, alikutana na watu kumi wenye ukoma; wakasimama mbali,

Luka 17:13 Luke 17:13

wakapaza sauti wakisema, Ee Yesu, Bwana mkubwa, uturehemu!

Luka 17:14 Luke 17:14

Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajionyeshe kwa makuhani. Ikawa walipokuwa wakienda walitakasika.

Luka 17:15 Luke 17:15

Na mmoja wao alipoona kwamba amepona, alirudi, huku akimtukuza Mungu kwa sauti kuu;

Luka 17:16 Luke 17:16

akaanguka kifudifudi miguuni pake, akamshukuru; naye alikuwa Msamaria.

Luka 17:17 Luke 17:17

Yesu akajibu, akanena, Hawakutakaswa wote kumi? Wale kenda wa wapi?

Luka 17:18 Luke 17:18

Je! Hawakuonekana waliorudi kumpa Mungu utukufu ila mgeni huyu?

Luka 17:19 Luke 17:19

Akamwambia, Inuka, enenda zako, imani yako imekuokoa.

Luka 17:20 Luke 17:20

Na alipoulizwa na Mafarisayo, Ufalme wa Mungu utakuja lini? Aliwajibu akawaambia, ufalme wa Mungu hauji kwa kuuchunguza;

Luka 17:21 Luke 17:21

wala hawatasema, Tazama, upo huku, au, kule, kwa maana, tazama, ufalme wa Mungu umo ndani yenu.

Luka 17:22 Luke 17:22

Akawaambia wanafunzi, Siku zitakuja mtakapotamani kuona siku moja katika siku zake Mwana wa Adamu, msiione.

Luka 17:23 Luke 17:23

Tena watawaambia, Tazama, kule! Tazama, huku! Msiondoke mahali mlipo, wala msiwafuate;

Luka 17:24 Luke 17:24

kwa kuwa, kama vile umeme umulikavyo toka upande huu chini ya mbingu hata upande huu chini ya mbingu, ndivyo atakavyokuwa Mwana wa Adamu katika siku yake.

Luka 17:25 Luke 17:25

Lakini kwanza, hana budi kupata mateso mengi, na kukataliwa na kizazi hiki.

Luka 17:26 Luke 17:26

Na kama ilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa katika siku zake Mwana wa Adamu.

Luka 17:27 Luke 17:27

Walikuwa wakila na kunywa, walikuwa wakioa na kuolewa, hata siku ile Nuhu aliyoingia katika safina, gharika ikashuka ikawaangamiza wote.

Luka 17:28 Luke 17:28

Na kadhalika, kama ilivyokuwa katika siku za Lutu, walikuwa wakila na kunywa, walikuwa wakinunua na kuuza, wakipanda na kujenga;

Luka 17:29 Luke 17:29

lakini siku ile Lutu aliyotoka Sodoma kulinyesha moto na kibiriti kutoka mbinguni vikawaangamiza wote.

Luka 17:30 Luke 17:30

Hivyo ndivyo itakavyokuwa siku ile atakayofunuliwa Mwana wa Adamu.

Luka 17:31 Luke 17:31

Katika siku ile, aliye juu ya dari, na vyombo vyake vimo ndani ya nyumba, asishuke ili kuvitwaa; na kadhalika, aliye shambani asirejee nyuma.

Luka 17:32 Luke 17:32

Mkumbukeni mkewe Lutu.

Luka 17:33 Luke 17:33

Mtu ye yote atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza; na ye yote atakayeiangamiza ataiponya.

Luka 17:34 Luke 17:34

Nawaambia, usiku huo watu wawili watakuwa katika kitanda kimoja; mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa.

Luka 17:35 Luke 17:35

Wanawake wawili watakuwa wakisaga pamoja; mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa.

Luka 17:36 Luke 17:36

Watu wawili watakuwa shambani, mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa.]

Luka 17:37 Luke 17:37

Wakajibu, wakamwuliza, Wapi, Bwana? Akawaambia, Ulipo mzoga, ndipo watakapokutanika tai.