Luka Mlango 18 Luke

Luka 18:1 Luke 18:1

Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa.

Luka 18:2 Luke 18:2

Akasema, Palikuwa na kadhi katika mji fulani, hamchi Mungu, wala hajali watu.

Luka 18:3 Luke 18:3

Na katika mji huo palikuwa na mwanamke mjane, aliyekuwa akimwendea-endea, akisema, Nipatie haki na adui wangu.

Luka 18:4 Luke 18:4

Naye kwa muda alikataa; halafu akasema moyoni mwake, Ijapokuwa simchi Mungu wala sijali watu,

Luka 18:5 Luke 18:5

lakini, kwa kuwa mjane huyu ananiudhi, nitampatia haki yake, asije akanichosha kwa kunijia daima.

Luka 18:6 Luke 18:6

Bwana akasema, Sikilizeni asemavyo yule kadhi dhalimu.

Luka 18:7 Luke 18:7

Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao?

Luka 18:8 Luke 18:8

Nawaambia, atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani?

Luka 18:9 Luke 18:9

Akawaambia mfano huu watu waliojikinai ya kuwa wao ni wenye haki, wakiwadharau wengine wote.

Luka 18:10 Luke 18:10

Watu wawili walipanda kwenda hekaluni kusali, mmoja Farisayo, wa pili mtoza ushuru.

Luka 18:11 Luke 18:11

Yule Farisayo akasimama akiomba hivi moyoni mwake; Ee Mungu, nakushukuru kwa kuwa mimi si kama watu wengine, wanyang'anyi, wadhalimu, wazinzi, wala kama huyu mtoza ushuru.

Luka 18:12 Luke 18:12

Mimi nafunga mara mbili kwa juma; hutoa zaka katika mapato yangu yote.

Luka 18:13 Luke 18:13

Lakini yule mtoza ushuru alisimama mbali, wala hakuthubutu hata kuinua macho yake mbinguni, bali alijipiga-piga kifua akisema, Ee Mungu, uniwie radhi mimi mwenye dhambi.

Luka 18:14 Luke 18:14

Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.

Luka 18:15 Luke 18:15

Wakamletea na watoto wachanga ili awaguse; lakini wanafunzi walipoona waliwakemea.

Luka 18:16 Luke 18:16

Bali Yesu akawaita waje kwake, akasema, Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa kuwa watu kama hao ufalme wa Mungu ni wao.

Luka 18:17 Luke 18:17

Amin, nawaambia, Mtu ye yote asiyeupokea ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hauingii kamwe.

Luka 18:18 Luke 18:18

Tena, mtu mkubwa mmoja alimwuliza, akisema, Mwalimu mwema, nifanye nini ili nipate kuurithi uzima wa milele?

Luka 18:19 Luke 18:19

Yesu akamwambia, Mbona unaniita mwema? Hakuna aliye mwema ila mmoja, naye ndiye Mungu.

Luka 18:20 Luke 18:20

Wazijua amri; Usizini, Usiue, Usiibe, Usishuhudie uongo, Waheshimu baba yako na mama yako.

Luka 18:21 Luke 18:21

Akasema, Hayo yote nimeyashika tangu utoto wangu.

Luka 18:22 Luke 18:22

Yesu aliposikia hayo alimwambia, Umepungukiwa na neno moja bado; viuze ulivyo navyo vyote, ukawagawanyie maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha, njoo unifuate.

Luka 18:23 Luke 18:23

Lakini aliposikia hayo alihuzunika sana, maana alikuwa na mali nyingi.

Luka 18:24 Luke 18:24

Yesu alipoona vile alisema, Kwa shida gani wenye mali watauingia ufalme wa Mungu!

Luka 18:25 Luke 18:25

Kwa maana ni vyepesi ngamia kupita katika tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.

Luka 18:26 Luke 18:26

Nao waliosikia walisema, Ni nani basi awezaye kuokoka?

Luka 18:27 Luke 18:27

Akasema, Yasiyowezekana kwa wanadamu yawezekana kwa Mungu.

Luka 18:28 Luke 18:28

Petro akasema, Tazama, sisi tumeviacha vitu vyetu vyote na kukufuata.

Luka 18:29 Luke 18:29

Akawaambia, Hakika nawaambia, hakuna mtu aliyeacha nyumba, au mke, au ndugu, au wazazi, au wana, kwa ajili ya ufalme wa Mungu,

Luka 18:30 Luke 18:30

asiyepokea zaidi mara nyingi katika zamani hizi, na katika ulimwengu ujao uzima wa milele.

Luka 18:31 Luke 18:31

Akawachukua wale Thenashara, akawaambia, Tazameni, tunapanda kwenda Yerusalemu, na mambo yote yatatimizwa, Mwana wa Adamu aliyoandikiwa na manabii.

Luka 18:32 Luke 18:32

Kwa kuwa atatiwa mikononi mwa Mataifa, atafanyiwa dhihaka; atatendwa jeuri, na kutemewa mate;

Luka 18:33 Luke 18:33

nao watampiga mijeledi, kisha watamwua; na siku ya tatu atafufuka.

Luka 18:34 Luke 18:34

Walakini hawakuelewa maneno hayo hata kidogo, na jambo hilo lilikuwa limefichwa kwao, wala hawakufahamu yaliyonenwa.

Luka 18:35 Luke 18:35

Ikawa alipokaribia Yeriko, mtu mmoja kipofu alikuwa ameketi kando ya njia, akiomba sadaka;

Luka 18:36 Luke 18:36

na alipowasikia makutano wakipita, aliuliza, Kuna nini?

Luka 18:37 Luke 18:37

Wakamwambia, Yesu wa Nazareti anapita.

Luka 18:38 Luke 18:38

Akapiga kelele, akisema, Yesu, Mwana wa Daudi, unirehemu.

Luka 18:39 Luke 18:39

Basi wale waliotangulia wakamkemea ili anyamaze; lakini yeye alizidi sana kupaza sauti, Ee Mwana wa Daudi, unirehemu.

Luka 18:40 Luke 18:40

Yesu akasimama, akaamuru aletwe kwake; na alipomkaribia, alimwuliza,

Luka 18:41 Luke 18:41

Wataka nikufanyie nini? Akasema, Bwana, nipate kuona.

Luka 18:42 Luke 18:42

Yesu akamwambia, Upewe kuona; imani yako imekuponya.

Luka 18:43 Luke 18:43

Mara hiyo akapata kuona, akamfuata, huku akimtukuza Mungu. Na watu wote walipoona hayo walimsifu Mungu.