Luka Mlango 4 Luke

Luka 4:1 Luke 4:1

Na Yesu, hali amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Yordani, akaongozwa na Roho muda wa siku arobaini nyikani,

Luka 4:2 Luke 4:2

akijaribiwa na Ibilisi. Na siku hizo alikuwa hali kitu; hata zilipotimia, aliona njaa.

Luka 4:3 Luke 4:3

Ibilisi akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, liambie jiwe hili liwe mkate.

Luka 4:4 Luke 4:4

Yesu akamjibu, Imeandikwa ya kwamba mtu hataishi kwa mkate tu.

Luka 4:5 Luke 4:5

Akampandisha juu, akamwonyesha milki zote za ulimwengu kwa dakika moja.

Luka 4:6 Luke 4:6

Ibilisi akamwambia, Nitakupa wewe enzi hii yote, na fahari yake, kwa kuwa imo mikononi mwangu, nami humpa ye yote kama nipendavyo.

Luka 4:7 Luke 4:7

Basi, wewe ukisujudu mbele yangu yote yatakuwa yako.

Luka 4:8 Luke 4:8

Yesu akajibu akamwambia, Imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake.

Luka 4:9 Luke 4:9

Akamwongoza mpaka Yerusalemu, akamweka juu ya kinara cha hekalu, akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, jitupe chini;

Luka 4:10 Luke 4:10

kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake wakulinde;

Luka 4:11 Luke 4:11

na ya kwamba,mikononi mwao watakuchukua, Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.

Luka 4:12 Luke 4:12

Yesu akajibu akamwambia, Imenenwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako.

Luka 4:13 Luke 4:13

Basi alipomaliza kila jaribu, Ibilisi akamwacha akaenda zake kwa muda.

Luka 4:14 Luke 4:14

Yesu akarudi kwa nguvu za Roho, akenda Galilaya; habari zake zikaenea katika nchi zote za kandokando.

Luka 4:15 Luke 4:15

Naye alikuwa akifundisha katika masinagogi yao, akitukuzwa na watu wote.

Luka 4:16 Luke 4:16

Akaenda Nazareti, hapo alipolelewa; na siku ya sabato akaingia katika sinagogi kama ilivyokuwa desturi yake, akasimama ili asome.

Luka 4:17 Luke 4:17

Akapewa chuo cha nabii Isaya, akakifungua chuo, akatafuta mahali palipoandikwa,

Luka 4:18 Luke 4:18

Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa,

Luka 4:19 Luke 4:19

Na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa.

Luka 4:20 Luke 4:20

Akakifunga chuo, akamrudishia mtumishi, akaketi; na watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho.

Luka 4:21 Luke 4:21

Akaanza kuwaambia, Leo maandiko haya yametimia masikioni mwenu.

Luka 4:22 Luke 4:22

Wakamshuhudia wote, wakiyastaajabia maneno ya neema yaliyotoka kinywani mwake, wakasema, Huyu siye mwana wa Yusufu?

Luka 4:23 Luke 4:23

Akawaambia, Hapana shaka mtaniambia mithali hii, Tabibu, jiponye nafsi yako; mambo yote tuliyosikia kwamba yametendeka Kapernaumu, yatende na hapa pia katika nchi yako mwenyewe.

Luka 4:24 Luke 4:24

Akasema, Amin, nawaambia ya kwamba, Hakuna nabii mwenye kukubaliwa katika nchi yake mwenyewe.

Luka 4:25 Luke 4:25

Lakini, kwa hakika nawaambia, Palikuwa na wajane wengi katika nchi ya Israeli zamani za Eliya, wakati mbingu zilipofungwa miaka mitatu na miezi sita, njaa kuu ikaingia nchi nzima;

Luka 4:26 Luke 4:26

wala Eliya hakutumwa kwa mmojawapo, ila kwa mjane mmoja wa Sarepta katika nchi ya Sidoni.

Luka 4:27 Luke 4:27

Tena, palikuwa na wenye ukoma wengi katika Israeli zamani za nabii Elisha, wala hapana aliyetakaswa ila Naamani, mtu wa Shamu.

Luka 4:28 Luke 4:28

Wakajaa ghadhabu wote waliokuwa katika sinagogi walipoyasikia hayo.

Luka 4:29 Luke 4:29

Wakaondoka wakamtoa nje ya mji, wakampeleka mpaka ukingo wa kilima ambacho mji wao umejengwa juu yake, wapate kumtupa chini;

Luka 4:30 Luke 4:30

lakini yeye alipita katikati yao, akaenda zake.

Luka 4:31 Luke 4:31

Akashuka mpaka Kapernaumu, mji wa Galilaya, akawa akiwafundisha siku ya sabato;

Luka 4:32 Luke 4:32

wakashangaa mno kwa mafundisho yake, kwa kuwa neno lake lilikuwa na uwezo.

Luka 4:33 Luke 4:33

Na ndani ya sinagogi mlikuwa na mtu mwenye roho ya pepo mchafu, akalia kwa sauti kuu,

Luka 4:34 Luke 4:34

akisema, Acha! Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Umekuja kutuangamiza? Nakujua u nani, Mtakatifu wa Mungu.

Luka 4:35 Luke 4:35

Yesu akamkemea, akisema, Fumba kinywa, mtoke. Ndipo yule pepo akamwangusha katikati, akamtoka asimdhuru neno.

Luka 4:36 Luke 4:36

Mshangao ukawashika wote, wakasemezana wakisema, Ni neno gani hili, maana awaamuru pepo wachafu kwa uwezo na nguvu, nao hutoka.

Luka 4:37 Luke 4:37

Habari zake zikaenea kila mahali katika nchi ile.

Luka 4:38 Luke 4:38

Akatoka katika sinagogi, akaingia katika nyumba ya Simoni. Naye mkwewe Simoni, mamaye mkewe, alikuwa ameshikwa na homa kali, wakamwomba kwa ajili yake.

Luka 4:39 Luke 4:39

Akasimama karibu naye, akaikemea ile homa, ikamwacha; mara hiyo akaondoka, akawatumikia.

Luka 4:40 Luke 4:40

Na jua lilipokuwa likichwa, wote waliokuwa na wagonjwa wenye maradhi mbali mbali waliwaleta kwake, akaweka mikono yake juu ya kila mmoja akawaponya.

Luka 4:41 Luke 4:41

Pepo nao waliwatoka watu wengi, wakipiga kelele na kusema, Wewe u Mwana wa Mungu. Akawakemea, asiwaache kunena, kwa sababu walimjua kuwa ndiye Kristo.

Luka 4:42 Luke 4:42

Hata kulipokucha alitoka akaenda mahali pasipokuwa na watu; makutano wakawa wakimtafuta-tafuta, wakafika kwake, wakataka kumzuia asiondoke kwao.

Luka 4:43 Luke 4:43

Akawaambia, Imenipasa kuihubiri habari njema ya ufalme wa Mungu katika miji mingine pia; maana kwa sababu hiyo nalitumwa.

Luka 4:44 Luke 4:44

Basi, alikuwa akihubiri katika masinagogi ya Galilaya.