Luka Mlango 22 Luke

Luka 22:1 Luke 22:1

Ikakaribia sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu, iitwayo Sikukuu ya Pasaka.

Luka 22:2 Luke 22:2

Na wakuu wa makuhani na waandishi walikuwa wakitafuta njia ya kumwua; maana walikuwa wakiwaogopa watu.

Luka 22:3 Luke 22:3

Shetani akamwingia Yuda, aitwaye Iskariote, naye ni mmoja wa wale Thenashara.

Luka 22:4 Luke 22:4

Akaondoka, akaenda akasema na wakuu wa makuhani na majemadari, jinsi atakavyoweza kumtia mikononi mwao.

Luka 22:5 Luke 22:5

Wakafurahi, wakapatana naye kumpa fedha.

Luka 22:6 Luke 22:6

Akakubali, akatafuta nafasi ya kumsaliti kwao pasipokuwapo mkutano.

Luka 22:7 Luke 22:7

Ikafika siku ya mikate isiyotiwa chachu, ambayo ilipasa kuchinja pasaka.

Luka 22:8 Luke 22:8

Akawatuma Petro na Yohana, akisema, Nendeni, mkatuandalie pasaka tupate kuila.

Luka 22:9 Luke 22:9

Wakamwambia, Wataka tuandae wapi?

Luka 22:10 Luke 22:10

Akawaambia, Tazama, mtakapoingia mjini mtakutana na mwanamume akichukua mtungi wa maji; mfuateni mkaingie katika nyumba atakayoingia yeye.

Luka 22:11 Luke 22:11

Na mtamwambia mwenye nyumba, Mwalimu akuambia, Ki wapi chumba cha wageni, nipate kula pasaka humo pamoja na wanafunzi wangu?

Luka 22:12 Luke 22:12

Naye atawaonyesha chumba kikubwa orofani, kimekwisha andikwa; andaeni humo.

Luka 22:13 Luke 22:13

Wakaenda, wakaona kama alivyowaambia, wakaiandaa pasaka.

Luka 22:14 Luke 22:14

Hata saa ilipofika aliketi chakulani, yeye na wale mitume pamoja naye.

Luka 22:15 Luke 22:15

Akawaambia, Nimetamani sana kuila pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu;

Luka 22:16 Luke 22:16

kwa maana nawaambia ya kwamba siili tena hata itakapotimizwa katika ufalme wa Mungu.

Luka 22:17 Luke 22:17

Akapokea kikombe, akashukuru, akasema, Twaeni hiki, mgawanye ninyi kwa ninyi;

Luka 22:18 Luke 22:18

Maana nawaambia ya kwamba tangu sasa sinywi mazao ya mzabibu hata ufalme wa Mungu utakapokuja.

Luka 22:19 Luke 22:19

Akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa, akisema, [Huu ndio mwili wangu unaotolewa kwa ajili yenu; fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.

Luka 22:20 Luke 22:20

Kikombe nacho vivyo hivyo baada ya kula; akisema, Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu, inayomwagika kwa ajili yenu.]

Luka 22:21 Luke 22:21

Walakini, tazama, mkono wake yeye anayenisaliti upo hapa pamoja nami mezani,

Luka 22:22 Luke 22:22

Kwa kuwa Mwana wa Adamu aenda zake kama ilivyokusudiwa; lakini, ole wake mtu yule amsalitiye!

Luka 22:23 Luke 22:23

Wakaanza kuulizana wao kwa wao, ni yupi miongoni mwao atakayelitenda jambo hilo.

Luka 22:24 Luke 22:24

Yakatokea mashindano kati yao, kwamba ni nani anayehesabiwa kuwa mkubwa.

Luka 22:25 Luke 22:25

Akawaambia, Wafalme wa Mataifa huwatawala, na wenye mamlaka juu yao huitwa Wenye fadhili;

Luka 22:26 Luke 22:26

lakini kwenu ninyi sivyo; bali aliye mkubwa kwenu na awe kama aliye mdogo; na mwenye kuongoza kama yule atumikaye.

Luka 22:27 Luke 22:27

Maana aliye mkubwa ni yupi? Yeye aketiye chakulani, au yule atumikaye? Siye yule aketiye chakulani? Lakini mimi kati yenu ni kama atumikaye.

Luka 22:28 Luke 22:28

Nanyi ndinyi mliodumu pamoja nami katika majaribu yangu.

Luka 22:29 Luke 22:29

Nami nawawekea ninyi ufalme, kama vile Baba yangu alivyoniwekea mimi;

Luka 22:30 Luke 22:30

mpate kula na kunywa mezani pangu katika ufalme wangu; na kuketi katika viti vya enzi, huku mkiwahukumu kabila kumi na mbili za Israeli.

Luka 22:31 Luke 22:31

Akasema, Simoni, Simoni, tazama, Shetani amewataka ninyi apate kuwapepeta kama vile ngano;

Luka 22:32 Luke 22:32

lakini nimekuombea wewe ili imani yako isitindike; nawe utakapoongoka waimarishe ndugu zako.

Luka 22:33 Luke 22:33

Akamwambia, Bwana, niwapo pamoja nawe, mimi ni tayari kwenda gerezani au hata kifoni.

Luka 22:34 Luke 22:34

Akasema, Nakuambia, Petro, jogoo hatawika leo, kabla wewe hujanikana mara tatu ya kuwa hunijui.

Luka 22:35 Luke 22:35

Akawauliza, Je! Hapo nilipowatuma hamna mfuko, wala mkoba, wala viatu, mlipungukiwa na kitu? Wakasema, La!

Luka 22:36 Luke 22:36

Akawaambia, Lakini sasa mwenye mfuko na auchukue, na mkoba vivyo hivyo; naye asiye na upanga, na auze joho yake akanunue.

Luka 22:37 Luke 22:37

Kwa kuwa nawaambia, hayo yaliyoandikwa hayana budi kutimizwa kwangu; ya kuwa, Alihesabiwa pamoja na wahalifu. Kwa sababu yanipasayo yanao mwisho wake.

Luka 22:38 Luke 22:38

Wakasema, Bwana, tazama, hapa pana panga mbili. Akawaambia, Basi.

Luka 22:39 Luke 22:39

Akatoka akaenda mpaka mlima wa Mizeituni kama ilivyokuwa desturi yake; wanafunzi wake nao wakafuatana naye.

Luka 22:40 Luke 22:40

Alipofika mahali pale aliwaambia, Ombeni kwamba msiingie majaribuni.

Luka 22:41 Luke 22:41

Mwenyewe akajitenga nao kama kiasi cha kutupa jiwe, akapiga magoti akaomba,

Luka 22:42 Luke 22:42

akisema, Ee Baba, ikiwa ni mapenzi yako, uniondolee kikombe hiki; walakini si mapenzi yangu, bali yako yatendeke.

Luka 22:43 Luke 22:43

Malaika kutoka mbinguni akamtokea akamtia nguvu.

Luka 22:44 Luke 22:44

Naye kwa vile alivyokuwa katika dhiki, akazidi sana kuomba; hari yake ikawa kama matone ya damu yakidondoka nchini.]

Luka 22:45 Luke 22:45

Alipoondoka katika kuomba kwake, akawajia wanafunzi wake, akawakuta wamelala usingizi kwa huzuni.

Luka 22:46 Luke 22:46

Akawaambia, Mbona mmelala usingizi? Ondokeni, mkaombe, msije mkaingia majaribuni.

Luka 22:47 Luke 22:47

Basi alipokuwa katika kusema, tazama, mkutano wa watu, na yule aitwaye Yuda, ambaye ni mmoja wa wale Thenashara, amewatangulia. Akamkaribia Yesu ili kumbusu.

Luka 22:48 Luke 22:48

Yesu akamwambia, Yuda, wamsaliti Mwana wa Adamu kwa kumbusu?

Luka 22:49 Luke 22:49

Na wale waliokuwa karibu naye walipoona yatakayotukia, walisema, Bwana, tuwapige kwa upanga?

Luka 22:50 Luke 22:50

Mmoja wao akampiga mtumwa wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio la kuume.

Luka 22:51 Luke 22:51

Yesu akajibu akasema, Mwe radhi kwa hili. Akamgusa sikio, akamponya.

Luka 22:52 Luke 22:52

Yesu akawaambia wakuu wa makuhani, na maakida wa hekalu, na wazee, waliokuja juu yake, Je! Mmekuja wenye panga na marungu kama kukamata mnyang'anyi?

Luka 22:53 Luke 22:53

Kila siku nilipokuwa pamoja nanyi hekaluni hamkuninyoshea mikono, lakini hii ndiyo saa yenu, na mamlaka ya giza.

Luka 22:54 Luke 22:54

Wakamkamata, wakamchukua, wakaenda naye nyumbani kwa Kuhani Mkuu. Na Petro alimfuata kwa mbali.

Luka 22:55 Luke 22:55

Na walipokwisha washa moto katikati ya kiwanja, waliketi pamoja, naye Petro akaketi kati yao.

Luka 22:56 Luke 22:56

Ndipo mjakazi mmoja akamwona ameketi mwangani, akamkazia macho akasema, Na huyu alikuwa pamoja naye.

Luka 22:57 Luke 22:57

Akakana, akisema, Ee mwanamke, simjui.

Luka 22:58 Luke 22:58

Baadaye kitambo mtu mwingine alimwona akasema, Wewe nawe u mmoja wao. Petro akasema, Ee mtu, si mimi.

Luka 22:59 Luke 22:59

Halafu, yapata saa moja, mtu mwingine alikaza kusema, Hakika na huyu alikuwa pamoja naye, kwa kuwa yeye pia ni Mgalilaya.

Luka 22:60 Luke 22:60

Petro akasema, Ee mtu, sijui usemalo. Na papo hapo alipokuwa katika kusema, jogoo aliwika.

Luka 22:61 Luke 22:61

Bwana akageuka akamtazama Petro. Petro akalikumbuka lile neno la Bwana jinsi alivyomwambia, Leo kabla hajawika jogoo utanikana mara tatu.

Luka 22:62 Luke 22:62

Akatoka nje akalia kwa majonzi.

Luka 22:63 Luke 22:63

Na wale watu waliokuwa wakimshika Yesu walimfanyia dhihaka, wakampiga.

Luka 22:64 Luke 22:64

Wakamfunika macho, kisha wakamwuliza-uliza wakisema, Tabiri, ni nani aliyekupiga?

Luka 22:65 Luke 22:65

Wakamtolea na maneno mengine mengi ya kumtukana.

Luka 22:66 Luke 22:66

Hata kulipokucha, walikutanika jamii ya wazee, na wakuu wa makuhani, na waandishi, wakamleta katika baraza yao, wakisema,

Luka 22:67 Luke 22:67

Kama wewe ndiwe Kristo, tuambie. Akawaambia, Nijapowaambia, hamtasadiki kabisa.

Luka 22:68 Luke 22:68

Tena, nikiwauliza, hamtajibu.

Luka 22:69 Luke 22:69

Lakini tangu sasa Mwana wa Adamu atakuwa ameketi upande wa kuume wa Mungu Mwenyezi.

Luka 22:70 Luke 22:70

Wakasema wote, Basi, wewe ndiwe Mwana wa Mungu? Akawaambia, Ninyi mwasema kwamba mimi ndiye.

Luka 22:71 Luke 22:71

Wakasema, Basi, tuna haja gani tena ya ushuhuda? Maana, sisi wenyewe tumesikia maneno ya kinywa chake.