Luka Mlango 24 Luke

Luka 24:1 Luke 24:1

Hata siku ya kwanza ya juma, ilipoanza kupambazuka, walikwenda kaburini, wakiyaleta manukato waliyoweka tayari.

Luka 24:2 Luke 24:2

Wakalikuta lile jiwe limevingirishwa mbali na kaburi,

Luka 24:3 Luke 24:3

Wakaingia, wasiuone mwili wa Bwana Yesu.

Luka 24:4 Luke 24:4

Ikawa walipokuwa wakifadhaika kwa ajili ya neno hilo, tazama, watu wawili walisimama karibu nao, wamevaa nguo za kumeta-meta;

Luka 24:5 Luke 24:5

nao walipoingiwa na hofu na kuinama kifudifudi hata nchi, hao waliwaambia, Kwa nini mnamtafuta aliye hai katika wafu?

Luka 24:6 Luke 24:6

Hayupo hapa, amefufuka. Kumbukeni alivyosema nanyi alipokuwa akaliko Galilaya,

Luka 24:7 Luke 24:7

akisema, Imempasa Mwana wa Adamu kutiwa mikononi mwa wenye dhambi, na kusulibiwa, na kufufuka siku ya tatu.

Luka 24:8 Luke 24:8

Wakayakumbuka maneno yake.

Luka 24:9 Luke 24:9

Wakaondoka kaburini, wakarudi; wakawaarifu wale kumi na mmoja na wengine wote habari za mambo hayo yote.

Luka 24:10 Luke 24:10

Nao ni Mariamu Magdalene, na Yoana, na Mariamu mamaye Yakobo, na wale wanawake wengine waliokuwa pamoja nao;

Luka 24:11 Luke 24:11

hao waliwaambia mitume habari ya mambo hayo.

Luka 24:12 Luke 24:12

Maneno yao yakaonekana kuwa kama upuzi kwao, wala hawakuwasadiki. Lakini Petro aliondoka akaenda mbio hata kaburini, akainama akachungulia ndani, akaviona vile vitambaa vya sanda tu; akaenda zake akiyastaajabia yaliyotukia.

Luka 24:13 Luke 24:13

Na tazama, siku ile ile watu wawili miongoni mwao walikuwa wakienda kijiji kimoja, jina lake Emau, kilichokuwa mbali na Yerusalemu kama mwendo wa saa mbili.

Luka 24:14 Luke 24:14

Nao walikuwa wakizungumza wao kwa wao habari za mambo hayo yote yaliyotukia.

Luka 24:15 Luke 24:15

Ikawa katika kuzungumza na kuulizana kwao, Yesu mwenyewe alikaribia, akaandamana nao.

Luka 24:16 Luke 24:16

Macho yao yakafumbwa wasimtambue.

Luka 24:17 Luke 24:17

Akawaambia, Ni maneno gani haya mnayosemezana hivi mnapotembea? Wakasimama wamekunja nyuso zao.

Luka 24:18 Luke 24:18

Akajibu mmoja wao, jina lake Kleopa, akamwambia, Je! Wewe peke yako u mgeni katika Yerusalemu, hata huyajui yaliyotukia humo siku hizi?

Luka 24:19 Luke 24:19

Akawauliza, Mambo gani? Wakamwambia, Mambo ya Yesu wa Nazareti, aliyekuwa mtu nabii, mwenye uwezo katika kutenda na kunena mbele za Mungu na watu wote;

Luka 24:20 Luke 24:20

tena jinsi wakuu wa makuhani na wakubwa wetu walivyomtia katika hukumu ya kufa, wakamsulibisha.

Luka 24:21 Luke 24:21

Nasi tulikuwa tukitumaini ya kuwa yeye ndiye atakayewakomboa Israeli. Zaidi ya hayo yote, leo ni siku ya tatu tangu yalipotendeka mambo hayo;

Luka 24:22 Luke 24:22

tena, wanawake kadha wa kadha wa kwetu walitushitusha, waliokwenda kaburini asubuhi na mapema,

Luka 24:23 Luke 24:23

wasiuone mwili wake; wakaja wakasema ya kwamba wametokewa na malaika waliosema kwamba yu hai.

Luka 24:24 Luke 24:24

Na wengine waliokuwa pamoja nasi walikwenda kaburini wakaona vivyo hivyo kama wale wanawake walivyosema, ila yeye hawakumwona.

Luka 24:25 Luke 24:25

Akawaambia, Enyi msiofahamu, wenye mioyo mizito ya kuamini yote waliyoyasema manabii!

Luka 24:26 Luke 24:26

Je! Haikumpasa Kristo kupata mateso haya na kuingia katika utukufu wake?

Luka 24:27 Luke 24:27

Akaanza kutoka Musa na manabii wote, akawaeleza katika maandiko yote mambo yaliyomhusu yeye mwenyewe.

Luka 24:28 Luke 24:28

Wakakikaribia kile kijiji walichokuwa wakienda, naye alifanya kama anataka kuendelea mbele.

Luka 24:29 Luke 24:29

Wakamshawishi wakisema, Kaa pamoja nasi, kwa kuwa kumekuchwa, na mchana unakwisha. Akaingia ndani kukaa nao.

Luka 24:30 Luke 24:30

Ikawa alipokuwa ameketi nao chakulani, alitwaa mkate, akaubariki, akaumega, akawapa.

Luka 24:31 Luke 24:31

Yakafumbuliwa macho yao, wakamtambua; kisha akatoweka mbele yao.

Luka 24:32 Luke 24:32

Wakaambiana, Je! Mioyo yetu haikuwaka ndani yetu hapo alipokuwa akisema nasi njiani, na kutufunulia maandiko?

Luka 24:33 Luke 24:33

Wakaondoka saa ile ile, wakarejea Yerusalemu, wakawakuta wale kumi na mmoja wamekutanika, wao na wale waliokuwa pamoja nao,

Luka 24:34 Luke 24:34

wakisema, Bwana amefufuka kweli kweli, naye amemtokea Simoni.

Luka 24:35 Luke 24:35

Nao waliwapa habari ya mambo yale ya njiani, na jinsi alivyotambulikana nao katika kuumega mkate.

Luka 24:36 Luke 24:36

Na walipokuwa katika kusema habari hiyo, yeye mwenyewe alisimama katikati yao, akawaambia, Amani iwe kwenu.

Luka 24:37 Luke 24:37

Wakashituka, wakaogopa sana, wakidhani ya kwamba wanaona roho.

Luka 24:38 Luke 24:38

Akawaambia, Mbona mnafadhaika? Na kwa nini mnaona shaka mioyoni mwenu?

Luka 24:39 Luke 24:39

Tazameni mikono yangu na miguu yangu, ya kuwa ni mimi mwenyewe. Nishikenishikeni, mwone; kwa kuwa roho haina mwili na mifupa kama mnavyoniona mimi kuwa nayo.

Luka 24:40 Luke 24:40

Na baada ya kusema hayo aliwaonyesha mikono yake na miguu yake.

Luka 24:41 Luke 24:41

Basi walipokuwa hawajaamini kwa furaha, huku wakistaajabu, aliwaambia, Mna chakula cho chote hapa?

Luka 24:42 Luke 24:42

Wakampa kipande cha samaki wa kuokwa.

Luka 24:43 Luke 24:43

Akakitwaa, akala mbele yao.

Luka 24:44 Luke 24:44

Kisha akawaambia, Hayo ndiyo maneno yangu niliyowaambia nilipokuwa nikali pamoja nanyi, ya kwamba ni lazima yatimizwe yote niliyoandikiwa katika Torati ya Musa, na katika Manabii na Zaburi.

Luka 24:45 Luke 24:45

Ndipo akawafunulia akili zao wapate kuelewa na maandiko.

Luka 24:46 Luke 24:46

Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu;

Luka 24:47 Luke 24:47

na kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu.

Luka 24:48 Luke 24:48

Nanyi ndinyi mashahidi wa mambo haya.

Luka 24:49 Luke 24:49

Na tazama, nawaletea juu yenu ahadi ya Baba yangu; lakini kaeni humu mjini, hata mvikwe uwezo utokao juu.

Luka 24:50 Luke 24:50

Akawaongoza mpaka Bethania, akainua mikono yake akawabariki.

Luka 24:51 Luke 24:51

Ikawa katika kuwabariki, alijitenga nao; akachukuliwa juu mbinguni.

Luka 24:52 Luke 24:52

Wakamwabudu; kisha wakarudi Yerusalemu wenye furaha kuu.

Luka 24:53 Luke 24:53

Nao walikuwa daima ndani ya hekalu, wakimsifu Mungu.