Ezekieli Mlango 15 Ezekiel

Ezekieli 15:1 Ezekiel 15:1

Neno la Bwana likanijia, kusema,

Ezekieli 15:2 Ezekiel 15:2

Mwanadamu, mzabibu una sifa gani kuliko mti mwingine, au tawi la mzabibu lililokuwa kati ya miti ya msituni?

Ezekieli 15:3 Ezekiel 15:3

Je! Mti wake waweza kutwaliwa, ili kufanya kazi yo yote? Watu waweza kufanya chango kwa huo, ili kutundika chombo cho chote?

Ezekieli 15:4 Ezekiel 15:4

Tazama, watupwa motoni kwa kuni moto umeziteketeza ncha zake zote mbili, nao umeteketea katikati, je! Wafaa kwa kazi yo yote?

Ezekieli 15:5 Ezekiel 15:5

Tazama, ulipokuwa mzima, haukufaa kwa kazi yo yote; sembuse ukiisha kuliwa na moto, na kuteketea; je! Waweza kufaa kwa kazi yo yote?

Ezekieli 15:6 Ezekiel 15:6

Basi Bwana MUNGU asema hivi; Kama mzabibu kati ya miti ya msituni, niliyoupa moto uwe kuni, ndivyo nitakavyowatoa wakaao Yerusalemu.

Ezekieli 15:7 Ezekiel 15:7

Nami nitaukaza uso wangu juu yao; nao watatoka motoni, lakini moto utawateketeza; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, nitakapoukaza uso wangu juu yao.

Ezekieli 15:8 Ezekiel 15:8

Nami nitaifanya nchi kuwa ukiwa, kwa sababu wamekosa, asema Bwana MUNGU.