Mathayo Mlango 18 Matthew

Mathayo 18:1 Matthew 18:1

Saa ile wanafunzi wakamwendea Yesu wakisema,

Mathayo 18:2 Matthew 18:2

Ni nani basi aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni? Akaita mtoto mmoja, akamweka katikati yao,

Mathayo 18:3 Matthew 18:3

akasema, Amin, nawaambia, Msipoongoka na kuwa kama vitoto, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.

Mathayo 18:4 Matthew 18:4

Basi, ye yote ajinyenyekeshaye mwenyewe kama mtoto huyu, huyo ndiye aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni.

Mathayo 18:5 Matthew 18:5

Na ye yote atakayempokea mtoto mmoja mfano wa huyu kwa jina langu, anipokea mimi;

Mathayo 18:6 Matthew 18:6

bali atakayemkosesha mmojawapo wa wadogo hawa waniaminio, yamfaa afungiwe shingoni jiwe kubwa la kusagia, na kutoswa katika kilindi cha bahari.

Mathayo 18:7 Matthew 18:7

Ole ni wa ulimwengu kwa sababu ya mambo ya kukosesha! Maana hayana budi kuja mambo ya kukosesha; lakini ole wake mtu yule aliletaye jambo la kukosesha!

Mathayo 18:8 Matthew 18:8

Basi mkono wako au mguu wako ukikukosesha, ukate ukautupe mbali nawe; ni afadhali kuingia katika uzima hali umepungukiwa na mkono au mguu, kuliko kuwa na mikono miwili au miguu miwili, na kutupwa katika moto wa milele.

Mathayo 18:9 Matthew 18:9

Na jicho lako likikukosesha, ling'oe, ukalitupe mbali nawe; ni afadhali kuingia katika uzima una chongo, kuliko kuwa na macho mawili, na kutupwa katika jehanum ya moto.

Mathayo 18:10 Matthew 18:10

Angalieni msidharau mmojawapo wadogo hawa; kwa maana nawaambia ya kwamba malaika wao mbinguni siku zote huutazama uso wa Baba yangu aliye mbinguni.

Mathayo 18:11 Matthew 18:11

[Kwa maana Mwana wa Adamu alikuja kukiokoa kilichopotea.]

Mathayo 18:12 Matthew 18:12

Mwaonaje? Mtu akiwa na kondoo mia, mmoja akampotea, je! Hawaachi wale tisa na tisini, akaenda milimani, na kumtafuta yule aliyepotea?

Mathayo 18:13 Matthew 18:13

Hata akipata kumwona, amin, nawaambia, amfurahia huyo zaidi, kuliko wale tisa na tisini wasiopotea.

Mathayo 18:14 Matthew 18:14

Vivyo hivyo haipendezi mbele za Baba yenu aliye mbinguni kwamba mmoja wa wadogo hawa apotee.

Mathayo 18:15 Matthew 18:15

Na ndugu yako akikukosa, enenda ukamwonye, wewe na yeye peke yenu; akikusikia, umempata nduguyo.

Mathayo 18:16 Matthew 18:16

La, kama hasikii, chukua pamoja nawe tena mtu mmoja au wawili, ili kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu kila neno lithibitike.

Mathayo 18:17 Matthew 18:17

Na asipowasikiliza wao, liambie kanisa; na asipolisikiliza kanisa pia, na awe kwako kama mtu wa mataifa na mtoza ushuru.

Mathayo 18:18 Matthew 18:18

Amin, nawaambieni, yo yote mtakayoyafunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni; na yo yote mtakayoyafungua duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni.

Mathayo 18:19 Matthew 18:19

Tena nawaambia, ya kwamba wawili wenu watakapopatana duniani katika jambo lo lote watakaloliomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni.

Mathayo 18:20 Matthew 18:20

Kwa kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao.

Mathayo 18:21 Matthew 18:21

Kisha Petro akamwendea akamwambia, Bwana, ndugu yangu anikose mara ngapi nami nimsamehe? Hata mara saba?

Mathayo 18:22 Matthew 18:22

Yesu akamwambia, Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini.

Mathayo 18:23 Matthew 18:23

Kwa sababu hii ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyetaka kufanya hesabu na watumwa wake.

Mathayo 18:24 Matthew 18:24

Alipoanza kuifanya, aliletewa mtu mmoja awiwaye talanta elfu kumi.

Mathayo 18:25 Matthew 18:25

Naye alipokosa cha kulipa, bwana wake akaamuru auzwe, yeye na mkewe na watoto wake, na vitu vyote alivyo navyo, ikalipwe ile deni.

Mathayo 18:26 Matthew 18:26

Basi yule mtumwa akaanguka, akamsujudia akisema, Bwana, nivumilie, nami nitakulipa yote pia.

Mathayo 18:27 Matthew 18:27

Bwana wa mtumwa yule akamhurumia, akamfungua, akamsamehe ile deni.

Mathayo 18:28 Matthew 18:28

Mtumwa yule akatoka, akamwona mmoja wa wajoli wake, aliyemwia dinari mia akamkamata,akamshika koo,akisema Nilipe uwiwacho.

Mathayo 18:29 Matthew 18:29

Basi mjoli wake akaanguka miguuni pake, akamsihi, akisema, Nivumilie, nami nitakulipa yote pia.

Mathayo 18:30 Matthew 18:30

Lakini hakutaka, akaenda, akamtupa kifungoni, hata atakapoilipa ile deni.

Mathayo 18:31 Matthew 18:31

Basi wajoli wake walipoyaona yaliyotendeka, walisikitika sana, wakaenda wakamweleza bwana wao yote yaliyotendeka.

Mathayo 18:32 Matthew 18:32

Ndipo bwana wake akamwita, akamwambia, Ewe mtumwa mwovu, nalikusamehe wewe deni ile yote, uliponisihi;

Mathayo 18:33 Matthew 18:33

nawe, je! Haikukupasa kumrehemu mjoli wako, kama mimi nilivyokurehemu wewe?

Mathayo 18:34 Matthew 18:34

Bwana wake akaghadhibika, akampeleka kwa watesaji, hata atakapoilipa deni ile yote.

Mathayo 18:35 Matthew 18:35

Ndivyo na Baba yangu wa mbinguni atakavyowatenda ninyi, msiposamehe kwa mioyo yenu kila mtu ndugu yake.