Mathayo Mlango 7 Matthew

Mathayo 7:1 Matthew 7:1

Msihukumu, msije mkahukumiwa ninyi.

Mathayo 7:2 Matthew 7:2

Kwa kuwa hukumu ile mhukumuyo, ndiyo mtakayohukumiwa; na kipimo kile mpimiacho, ndicho mtakachopimiwa.

Mathayo 7:3 Matthew 7:3

Basi, mbona wakitazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe huiangalii?

Mathayo 7:4 Matthew 7:4

Au utamwambiaje nduguyo, Niache nikitoe kibanzi katika jicho lako; na kumbe! Mna boriti ndani ya jicho lako mwenyewe?

Mathayo 7:5 Matthew 7:5

Mnafiki wewe, itoe kwanza ile boriti katika jicho lako mwenyewe; ndipo utakapoona vema kukitoa kile kibanzi katika jicho la ndugu yako.

Mathayo 7:6 Matthew 7:6

Msiwape mbwa kilicho kitakatifu, wala msitupe lulu zenu mbele ya nguruwe, wasije wakazikanyaga chini ya miguu yao, wakageuka na kuwararua.

Mathayo 7:7 Matthew 7:7

Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa;

Mathayo 7:8 Matthew 7:8

kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa.

Mathayo 7:9 Matthew 7:9

Au kuna mtu yupi kwenu, ambaye, mwanawe akimwomba mkate, atampa jiwe?

Mathayo 7:10 Matthew 7:10

Au akiomba samaki, atampa nyoka?

Mathayo 7:11 Matthew 7:11

Basi ikiwa ninyi, mlio waovu, mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Si zaidi sana Baba yenu aliye mbinguni atawapa mema wao wamwombao?

Mathayo 7:12 Matthew 7:12

Basi yo yote myatakayo mtendewe na watu, nanyi watendeeni vivyo hivyo; maana hiyo ndiyo torati na manabii.

Mathayo 7:13 Matthew 7:13

Ingieni kwa kupitia mlango ulio mwembamba; maana mlango ni mpana, na njia ni pana iendayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa mlango huo.

Mathayo 7:14 Matthew 7:14

Bali mlango ni mwembamba, na njia imesonga iendayo uzimani, nao waionao ni wachache.

Mathayo 7:15 Matthew 7:15

Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali.

Mathayo 7:16 Matthew 7:16

Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti?

Mathayo 7:17 Matthew 7:17

Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya.

Mathayo 7:18 Matthew 7:18

Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri.

Mathayo 7:19 Matthew 7:19

Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni.

Mathayo 7:20 Matthew 7:20

Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua.

Mathayo 7:21 Matthew 7:21

Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.

Mathayo 7:22 Matthew 7:22

Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

Mathayo 7:23 Matthew 7:23

Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.

Mathayo 7:24 Matthew 7:24

Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba;

Mathayo 7:25 Matthew 7:25

mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba.

Mathayo 7:26 Matthew 7:26

Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga;

Mathayo 7:27 Matthew 7:27

mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa.

Mathayo 7:28 Matthew 7:28

Ikawa, Yesu alipoyamaliza maneno hayo, makutano walishangaa mno kwa mafundisho yake;

Mathayo 7:29 Matthew 7:29

kwa maana alikuwa akiwafundisha kama mtu mwenye amri, wala si kama waandishi wao.