Mathayo Mlango 6 Matthew

Mathayo 6:1 Matthew 6:1

Angalieni msifanye wema wenu machoni pa watu, kusudi mtazamwe na wao; kwa maana mkifanya kama hayo, hampati thawabu kwa Baba yenu aliye mbinguni.

Mathayo 6:2 Matthew 6:2

Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ili watukuzwe na watu.

Mathayo 6:3 Matthew 6:3

Amin, nawaambieni, Wamekwisha kupata thawabu yao. Bali wewe utoapo sadaka, hata mkono wako wa kushoto usijue ufanyalo mkono wako wa kuume;

Mathayo 6:4 Matthew 6:4

sadaka yako iwe kwa siri; na Baba yako aonaye sirini atakujazi.

Mathayo 6:5 Matthew 6:5

Tena msalipo, msiwe kama wanafiki; kwa maana wao wapenda kusali hali wamesimama katika masinagogi na katika pembe za njia, ili waonekane na watu. Amin, nawaambia, Wamekwisha kupata thawabu yao.

Mathayo 6:6 Matthew 6:6

Bali wewe usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi.

Mathayo 6:7 Matthew 6:7

Nanyi mkiwa katika kusali, msipayuke-payuke, kama watu wa mataifa; maana wao hudhani ya kuwa watasikiwa kwa sababu ya maneno yao kuwa mengi.

Mathayo 6:8 Matthew 6:8

Basi msifanane na hao; maana Baba yenu anajua mnayohitaji kabla ninyi hamjamwomba.

Mathayo 6:9 Matthew 6:9

Basi ninyi salini hivi; Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, Ufalme wako uje,

Mathayo 6:10 Matthew 6:10

Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.

Mathayo 6:11 Matthew 6:11

Utupe leo riziki yetu.

Mathayo 6:12 Matthew 6:12

Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu.

Mathayo 6:13 Matthew 6:13

Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu. [Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.]

Mathayo 6:14 Matthew 6:14

Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi.

Mathayo 6:15 Matthew 6:15

Bali msipowasamehe watu makosa yao, wala Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu.

Mathayo 6:16 Matthew 6:16

Tena mfungapo, msiwe kama wanafiki wenye uso wa kukunjamana; maana hujiumbua nyuso zao, ili waonekane na watu kuwa wanafunga. Amin, nawaambia, wamekwisha kupata thawabu yao.

Mathayo 6:17 Matthew 6:17

Bali wewe ufungapo, jipake mafuta kichwani, unawe uso;

Mathayo 6:18 Matthew 6:18

ili usionekane na watu kuwa unafunga, ila na Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi.

Mathayo 6:19 Matthew 6:19

Msijiwekee hazina duniani, nondo na kutu viharibupo, na wevi huvunja na kuiba;

Mathayo 6:20 Matthew 6:20

bali jiwekeeni hazina mbinguni, kusikoharibika kitu kwa nondo wala kutu, wala wevi hawavunji wala hawaibi;

Mathayo 6:21 Matthew 6:21

kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako.

Mathayo 6:22 Matthew 6:22

Taa ya mwili ni jicho; basi jicho lako likiwa safi, mwili wako wote utakuwa na nuru.

Mathayo 6:23 Matthew 6:23

Lakini jicho lako likiwa bovu, mwili wako wote utakuwa na giza. Basi ile nuru iliyomo ndani yako ikiwa giza; si giza hilo!

Mathayo 6:24 Matthew 6:24

Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili; kwa maana atamchukia huyu, na kumpenda huyu; ama atashikamana na huyu, na kumdharau huyu. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali.

Mathayo 6:25 Matthew 6:25

Kwa sababu hiyo nawaambieni, Msisumbukie maisha yenu, mle nini au mnywe nini; wala miili yenu, mvae nini. Maisha je! Si zaidi ya chakula, na mwili zaidi ya mavazi?

Mathayo 6:26 Matthew 6:26

Waangalieni ndege wa angani, ya kwamba hawapandi, wala hawavuni, wala hawakusanyi ghalani; na Baba yenu wa mbinguni huwalisha hao. Ninyi je! Si bora kupita hao?

Mathayo 6:27 Matthew 6:27

Ni yupi kwenu ambaye akijisumbua aweza kujiongeza kimo chake hata mkono mmoja?

Mathayo 6:28 Matthew 6:28

Na mavazi, ya nini kuyasumbukia? Fikirini maua ya mashamba, jinsi yameavyo; hayafanyi kazi, wala hayasokoti

Mathayo 6:29 Matthew 6:29

nami nawaambia, ya kwamba hata Sulemani katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo la hayo.

Mathayo 6:30 Matthew 6:30

Basi, ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo, na kesho hutupwa kalibuni, je! Hatazidi sana kuwavika ninyi, enyi wa imani haba?

Mathayo 6:31 Matthew 6:31

Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini?

Mathayo 6:32 Matthew 6:32

Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote.

Mathayo 6:33 Matthew 6:33

Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.

Mathayo 6:34 Matthew 6:34

Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake.