Isaya Mlango 12 Isaiah

Isaya 12:1 Isaiah 12:1

Na katika siku hiyo utasema, Ee Bwana, nitakushukuru wewe; Kwa kuwa ijapokuwa ulinikasirikia, Hasira yako imegeukia mbali, Nawe unanifariji moyo.

Isaya 12:2 Isaiah 12:2

Tazama, Mungu ndiye wokovu wangu; Nitatumaini wala sitaogopa; Maana Bwana YEHOVA ni nguvu zangu na wimbo wangu; Naye amekuwa wokovu wangu.

Isaya 12:3 Isaiah 12:3

Basi, kwa furaha mtateka maji katika visima vya wokovu.

Isaya 12:4 Isaiah 12:4

Na katika siku hiyo mtasema, Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake; Yatangazeni matendo yake kati ya mataifa, Litajeni jina lake kuwa limetukuka.

Isaya 12:5 Isaiah 12:5

Mwimbieni Bwana; kwa kuwa ametenda makuu; Na yajulikane haya katika dunia yote.

Isaya 12:6 Isaiah 12:6

Paza sauti, piga kelele, mwenyeji wa Sayuni; Maana Mtakatifu wa Israeli ni mkuu kati yako.