Isaya Mlango 64 Isaiah

Isaya 64:1 Isaiah 64:1

Laiti ungepasua mbingu, na kushuka, ili milima iteteme mbele zako;

Isaya 64:2 Isaiah 64:2

kama vile moto uchomapo vichaka, na moto uchemshapo maji; ili kuwajulisha adui zako jina lako, mataifa wakatetemeke mbele zako!

Isaya 64:3 Isaiah 64:3

Ulipofanya mambo ya kutisha tusiyoyatazamia, ulishuka, milima ikatetema mbele zako.

Isaya 64:4 Isaiah 64:4

Maana tangu zamani za kale watu hawakusikia, wala kufahamu kwa masikio, wala jicho halikuona Mungu, ila wewe, atendaye mambo kwa ajili yake amngojaye.

Isaya 64:5 Isaiah 64:5

Wewe wamlaki yeye afurahiaye yaliyo haki na kuyatenda, watu wale wakukumbukao katika njia zako; tazama, ulikuwa na hasira, nasi tulitenda dhambi; tumekuwa katika mambo haya muda mwingi; nasi, je! Tutaokolewa?

Isaya 64:6 Isaiah 64:6

Kwa maana sisi sote tumekuwa kama mtu aliye mchafu, na matendo yetu yote ya haki yamekuwa kama nguo iliyotiwa unajisi; sisi sote twanyauka kama jani, na maovu yetu yatuondoa, kama upepo uondoavyo.

Isaya 64:7 Isaiah 64:7

Tena hapana aliitiaye jina lako, ajitahidiye akushike; kwa kuwa umetuficha uso wako, nawe umetukomesha kwa njia ya maovu yetu.

Isaya 64:8 Isaiah 64:8

Lakini sasa, Ee Bwana, wewe u baba yetu; sisi tu udongo, nawe u mfinyanzi wetu; sisi sote tu kazi ya mikono yako.

Isaya 64:9 Isaiah 64:9

Ee Bwana, usione hasira nyingi, wala usiukumbuke uovu siku zote; tazama, angalia, twakusihi, sisi sote tu watu wako.

Isaya 64:10 Isaiah 64:10

Miji yako mitakatifu imekuwa jangwa, Sayuni umekuwa jangwa, Yerusalemu umekuwa ukiwa.

Isaya 64:11 Isaiah 64:11

Nyumba yetu takatifu, nzuri, walimokusifu baba zetu, imeteketea moto; vitu vyetu vyote vyenye kupendeza vimeharibika.

Isaya 64:12 Isaiah 64:12

Utajizuia usiyaangalie mambo haya, Ee Bwana? Utanyamaza, na kututesa sana?