Ayabu Mlango 24 Job

Ayabu 24:1 Job 24:1

Mbona nyakati zisiwekwe na Mwenyezi? Na hao wamjuao mbona hawazioni siku zake?

Ayabu 24:2 Job 24:2

Wako waziondoao alama za mipaka; Huyachukua makundi kwa jeuri na kuyalisha.

Ayabu 24:3 Job 24:3

Humfukuza punda wake asiye baba, Humtwaa rehani ng'ombe wake mwanamke mjane.

Ayabu 24:4 Job 24:4

Humgeuza mhitaji aiache njia; Maskini wa nchi hujificha pamoja.

Ayabu 24:5 Job 24:5

Tazama, kama punda-mwitu jangwani Wao hutoka kwenda kazini mwao, wakitafuta chakula kwa bidii; Jangwa huwapa chakula cha watoto wao.

Ayabu 24:6 Job 24:6

Hukata nafaka zao mashambani; Na kuokota zabibu za waovu.

Ayabu 24:7 Job 24:7

Hujilaza usiku kucha uchi pasipo nguo, Wala hawana cha kujifunika baridi.

Ayabu 24:8 Job 24:8

Hutota kwa manyunyo ya milimani, Na kuambatana na jabali kwa kukosa sitara,

Ayabu 24:9 Job 24:9

Wako wamwondoao matitini kwa nguvu huyo asiye na baba, Na kutwaa rehani kwa maskini;

Ayabu 24:10 Job 24:10

Hata wazunguke uchi pasipo mavazi, Nao wakiwa na njaa huchukua miganda;

Ayabu 24:11 Job 24:11

Hushindika mafuta ndani ya makuta ya watu hao; Wakanyaga mashinikizo, nao wana kiu.

Ayabu 24:12 Job 24:12

Watu huugua toka mji ulio na watu wengi, Na roho yake aliyejeruhiwa hupiga ukelele; Wala Mungu hauangalii upumbavu.

Ayabu 24:13 Job 24:13

Hawa ni katika hao waliouasi mwanga; Hawazijui njia zake, Wala hawakai katika mapito yake.

Ayabu 24:14 Job 24:14

Mwuaji huamka asubuhi kukipambauka, huwaua maskini na wahitaji; Tena wakati wa usiku yu kama mwivi.

Ayabu 24:15 Job 24:15

Tena jicho lake mzinifu hungojea wakati wa giza-giza, Akisema, Hapana jicho litakaloniona; Naye huuficha uso wake.

Ayabu 24:16 Job 24:16

Wao hutoboa nyumba gizani; Hujifungia ndani wakati wa mchana; Hawaujui mwanga.

Ayabu 24:17 Job 24:17

Kwani asubuhi kwao wote ni kama giza tupu; Kwani wao wavijua vitisho vya hiyo giza tupu.

Ayabu 24:18 Job 24:18

Mwasema, Yeye ni mwepesi juu ya uso wa gharika; Sehemu yao inalaaniwa duniani; Hageuki kwenda njia ya mizabibuni.

Ayabu 24:19 Job 24:19

Chaka na hari hukausha maji ya theluji; Kuzimu nako hao ambao wamefanya dhambi.

Ayabu 24:20 Job 24:20

Tumbo lililomzaa litamsahau; buu litamla na kuona tamu; Hatakumbukwa tena; Na udhalimu utavunjwa kama mti.

Ayabu 24:21 Job 24:21

Naam, yeye huwala walio tasa wasiozaa; Wala hamtendei mema mwanamke mjane.

Ayabu 24:22 Job 24:22

Lakini Mungu huwadumisha wenye uwezo kwa nguvu zake; Huinuka, wasiokuwa na tumaini la kuishi.

Ayabu 24:23 Job 24:23

Huwapa kuwa na salama, nao wapumzika kwayo; Na macho yake ya juu ya njia zao.

Ayabu 24:24 Job 24:24

Wao wametukuzwa; lakini kitambo kidogo hutoweka; Naam, hushushwa, na kuondolewa njiani kama wengine wote, Nao hukatwa kama vile masuke ya ngano.

Ayabu 24:25 Job 24:25

Na kama sivyo sasa, ni nani atakayenihukumu kuwa ni mwongo, Na kuyafanya maneno yangu kuwa si kitu?