Ayabu Mlango 23 Job

Ayabu 23:1 Job 23:1

Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,

Ayabu 23:2 Job 23:2

Hata leo mashitaka yangu yana uchungu; Pigo langu ni zito zaidi ya kuugua kwangu.

Ayabu 23:3 Job 23:3

Laiti ningejua mahali niwezapo kumwona, Nifike hata hapo anapokaa!

Ayabu 23:4 Job 23:4

Ningeiweka daawa yangu mbele yake, Na kukijaza kinywa changu hoja.

Ayabu 23:5 Job 23:5

Ningeyajua maneno atakayonijibu, Na kuelewa na hayo atakayoniambia.

Ayabu 23:6 Job 23:6

Je! Angeshindana nami kwa ukuu wa uwezo wake? La, lakini angenisikiliza.

Ayabu 23:7 Job 23:7

Hapo walekevu wangepata kuhojiana naye; Basi hivyo ningeachiliwa na mwamuzi wangu milele.

Ayabu 23:8 Job 23:8

Tazama, naenda mbele, wala hayuko; Narudi nyuma, lakini siwezi kumwona;

Ayabu 23:9 Job 23:9

Na mkono wa kushoto, afanyapo kazi, lakini siwezi kumwona; Hujificha upande wa kuume, hata nisimwone.

Ayabu 23:10 Job 23:10

Lakini yeye aijua njia niendeayo; Akisha kunijaribu, nitatoka kama dhahabu.

Ayabu 23:11 Job 23:11

Mguu wangu umeshikamana sana na hatua zake; Njia yake nimeishika, wala sikukengeuka.

Ayabu 23:12 Job 23:12

Sikurudi nyuma kuiacha amri ya midomo yake; Nimeyatunza maneno ya kinywa chake zaidi ya riziki yangu,

Ayabu 23:13 Job 23:13

Lakini yeye ni mmoja, ni nani awezaye kumgeuza? Tena nafsi yake ilitakalo, ndilo afanyalo.

Ayabu 23:14 Job 23:14

Kwani yeye hulitimiliza hilo nililoamuriwa; Tena mambo mengi kama hayo ya pamoja naye.

Ayabu 23:15 Job 23:15

Kwa hiyo naona taabu mbele ya uso wake; Nitakapofikiri, namwogopa.

Ayabu 23:16 Job 23:16

Kwani Mungu ameufanya moyo wangu kuzimia, Naye Mwenyezi amenitaabisha;

Ayabu 23:17 Job 23:17

Maana sikufadhaishwa kwa sababu ya giza, Wala kwa sababu giza kuu limenifunika uso.