Zaburi Mlango 100 Psalms

Zaburi 100:1 Psalms 100:1

Mfanyieni Bwana shangwe, dunia yote;

Zaburi 100:2 Psalms 100:2

Mtumikieni Bwana kwa furaha; Njoni mbele zake kwa kuimba;

Zaburi 100:3 Psalms 100:3

Jueni kwamba Bwana ndiye Mungu; Ndiye aliyetuumba na sisi tu watu wake; Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake.

Zaburi 100:4 Psalms 100:4

Ingieni malangoni mwake kwa kushukuru; Nyuani mwake kwa kusifu; Mshukuruni, lihimidini jina lake;

Zaburi 100:5 Psalms 100:5

Kwa kuwa Bwana ndiye mwema; Rehema zake ni za milele; Na uaminifu wake vizazi na vizazi.