Zaburi Mlango 120 Psalms

Zaburi 120:1 Psalms 120:1

Katika shida yangu nalimlilia Bwana Naye akaniitikia.

Zaburi 120:2 Psalms 120:2

Ee Bwana, uiponye nafsi yangu Na midomo ya uongo na ulimi wa hila.

Zaburi 120:3 Psalms 120:3

Akupe nini, akuzidishie nini, Ewe ulimi wenye hila?

Zaburi 120:4 Psalms 120:4

Mishale ya mtu hodari iliyochongoka, Pamoja na makaa ya mretemu.

Zaburi 120:5 Psalms 120:5

Ole wangu mimi! Kwa kuwa nimekaa katika Mesheki; Na kufanya maskani yangu Katikati ya hema za Kedari.

Zaburi 120:6 Psalms 120:6

Nafsi yangu imekaa siku nyingi, Pamoja naye aichukiaye amani.

Zaburi 120:7 Psalms 120:7

Mimi ni wa amani; Bali ninenapo, wao huelekea vita.