Zaburi Mlango 110 Psalms

Zaburi 110:1 Psalms 110:1

Neno la Bwana kwa Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, Hata niwafanyapo adui zako Kuwa chini ya miguu yako.

Zaburi 110:2 Psalms 110:2

Bwana atainyosha toka Sayuni Fimbo ya nguvu zako. Uwe na enzi kati ya adui zako;

Zaburi 110:3 Psalms 110:3

Watu wako wanajitoa kwa hiari, Siku ya uwezo wako; Kwa uzuri wa utakatifu, Tokea tumbo la asubuhi, Unao umande wa ujana wako.

Zaburi 110:4 Psalms 110:4

Bwana ameapa, Wala hataghairi, Ndiwe kuhani hata milele, Kwa mfano wa Melkizedeki.

Zaburi 110:5 Psalms 110:5

Bwana yu mkono wako wa kuume; Ataseta wafalme, Siku ya ghadhabu yake.

Zaburi 110:6 Psalms 110:6

Atahukumu kati ya mataifa, Ataijaza nchi mizoga; Ataseta kichwa katika nchi nyingi.

Zaburi 110:7 Psalms 110:7

Atakunywa maji ya mto njiani; Kwa hiyo atakiinua kichwa chake.