Zaburi Mlango 141 Psalms

Zaburi 141:1 Psalms 141:1

Ee Bwana, nimekuita, unijie hima, Uisikie sauti yangu nikuitapo.

Zaburi 141:2 Psalms 141:2

Sala yangu ipae mbele zako kama uvumba, Kuinuliwa mikono yangu kama dhabihu ya jioni.

Zaburi 141:3 Psalms 141:3

Ee Bwana, uweke mlinzi kinywani pangu, Mngojezi mlangoni pa midomo yangu.

Zaburi 141:4 Psalms 141:4

Usiuelekeze moyo wangu kunako jambo baya, Nisiyazoelee matendo yasiyofaa, Pamoja na watu watendao maovu; Wala nisile vyakula vyao vya anasa.

Zaburi 141:5 Psalms 141:5

Mwenye haki na anipige, itakuwa fadhili; Anikemee, itakuwa kama mafuta kichwani; Kichwa changu kisikatae, Maana siachi kusali kati ya mabaya yao.

Zaburi 141:6 Psalms 141:6

Makadhi wao wakiangushwa kando ya genge, Watayasikia maneno yangu, maana ni matamu.

Zaburi 141:7 Psalms 141:7

Kama kupasua kuni na kuzichanja juu ya nchi, Ndivyo ilivyo mifupa yetu mdomoni pa kuzimu.

Zaburi 141:8 Psalms 141:8

Macho yangu yanakuelekea Wewe, MUNGU Bwana, Nimekukimbilia Wewe, usiniache nafsi yangu.

Zaburi 141:9 Psalms 141:9

Unilinde na mtego walionitegea, Na matanzi yao watendao maovu.

Zaburi 141:10 Psalms 141:10

Wabaya na waanguke katika nyavu zao wenyewe, Pindi mimi ninapopita salama.