Zaburi Mlango 124 Psalms

Zaburi 124:1 Psalms 124:1

Kama si Bwana aliyekuwa pamoja nasi, Israeli na aseme sasa,

Zaburi 124:2 Psalms 124:2

Kama si Bwana aliyekuwa pamoja nasi, Wanadamu walipotushambulia.

Zaburi 124:3 Psalms 124:3

Papo hapo wangalitumeza hai, Hasira yao ilipowaka juu yetu

Zaburi 124:4 Psalms 124:4

Papo hapo maji yangalitugharikisha, Mto ungalipita juu ya roho zetu;

Zaburi 124:5 Psalms 124:5

Papo hapo yangalipita juu ya nafsi zetu Maji yafurikayo.

Zaburi 124:6 Psalms 124:6

Na ahimidiwe Bwana; Asiyetutoa kuwa mawindo kwa meno yao.

Zaburi 124:7 Psalms 124:7

Nafsi yetu imeokoka kama ndege Katika mtego wa wawindaji, Mtego umevunjika, nasi tumeokoka.

Zaburi 124:8 Psalms 124:8

Msaada wetu u katika jina la Bwana, Aliyezifanya mbingu na nchi.