Zaburi Mlango 13 Psalms

Zaburi 13:1 Psalms 13:1

Ee Bwana, hata lini utanisahau, hata milele? Hata lini utanificha uso wako?

Zaburi 13:2 Psalms 13:2

Hata lini nifanye mashauri nafsini mwangu, Nikihuzunika moyoni mchana kutwa? Hata lini adui yangu atukuke juu yangu?

Zaburi 13:3 Psalms 13:3

Ee Bwana, Mungu wangu, uangalie, uniitikie; Uyatie nuru macho yangu, Nisije nikalala usingizi wa mauti.

Zaburi 13:4 Psalms 13:4

Adui yangu asije akasema, Nimemshinda; Watesi wangu wasifurahi ninapoondoshwa.

Zaburi 13:5 Psalms 13:5

Nami nimezitumainia fadhili zako; Moyo wangu na uufurahie wokovu wako.

Zaburi 13:6 Psalms 13:6

Naam, nimwimbie Bwana, Kwa kuwa amenitendea kwa ukarimu.